< Amos 5 >

1 Heare ye this worde, which I lift vp vpon you, euen a lamentation of the house of Israel.
Sikia neno hili, ee nyumba ya Israeli, ombolezo hili ninalifanya kuwahusu ninyi:
2 The virgine Israel is fallen, and shall no more rise: shee is left vpon her lande, and there is none to raise her vp.
“Bikira Israeli ameanguka, kamwe hatainuka tena, ameachwa pweke katika nchi yake, hakuna yeyote wa kumwinua.”
3 For thus saith ye Lord God, The citie which went out by a thousand, shall leaue an hundreth: and that which went forth by an hundreth, shall leaue ten to the house of Israel.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Wakati mmoja wa miji yako utakapopeleka watu elfu moja vitani kwa ajili ya Israeli, mia moja tu watarudi; wakati mji utakapopeleka mia moja, kumi tu ndio watarudi hai.”
4 For thus saith the Lord vnto the house of Israel, Seeke ye me, and ye shall liue.
Hili ndilo Bwana asemalo kwa nyumba ya Israeli: “Nitafuteni mpate kuishi;
5 But seeke not Beth-el, nor enter into Gilgal, and go not to Beer-sheba: for Gilgal shall goe into captiuitie, and Beth-el shall come to nought.
msitafute Betheli, msiende Gilgali, msisafiri kwenda Beer-Sheba. Kwa maana kwa hakika Gilgali itakwenda uhamishoni, na Betheli itafanywa kuwa si kitu.”
6 Seeke the Lord, and yee shall liue, least he breake out like fire in the house of Ioseph and deuoure it, and there be none to quench it in Beth-el.
Mtafuteni Bwana mpate kuishi, au atafagia nyumba ya Yosefu kama moto; utawateketeza, nayo Betheli haitakuwa na yeyote wa kuuzima.
7 They turne iudgement to wormewood, and leaue off righteousnes in the earth.
Ninyi ambao mnageuza haki kuwa uchungu na kuiangusha haki chini
8 He maketh Pleiades, and Orion, and he turneth the shadowe of death into the morning, and he maketh the day darke as night: he calleth the waters of the sea, and powreth them out vpon the open earth: the Lord is his Name.
(yeye ambaye alifanya Kilimia na Orioni, ambaye hugeuza giza kuwa mapambazuko na mchana kuwa usiku, ambaye huyaita maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake;
9 He strengtheneth the destroyer against the mightie: and the destroyer shall come against the fortresse.
yeye hufanya maangamizo kwenye ngome na kufanya mji uliozungushiwa ngome kuwa ukiwa),
10 They haue hated him, that rebuked in the gate: and they abhorred him that speaketh vprightly.
mnamchukia yule akemeaye mahakamani, na kumdharau yule ambaye husema kweli.
11 Forasmuch then as your treading is vpon the poore, and yee take from him burdens of wheate, ye haue built houses of hewen stone, but ye shall not dwel in them: ye haue plated pleasant vineyards, but ye shall not drinke wine of them.
Mnamgandamiza maskini na kumlazimisha awape nafaka. Kwa hiyo, ingawa mmejenga majumba ya mawe ya fahari, hamtaishi ndani yake; ingawa mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu, hamtakunywa divai yake.
12 For I know your manifold transgressions, and your mightie sinnes: they afflict the iust, they take rewards, and they oppresse the poore in ye gate.
Kwa kuwa ninajua hesabu ya makosa yenu na ukubwa wa dhambi zenu. Mmewaonea wenye haki na kupokea rushwa na kuzuia haki ya maskini mahakamani.
13 Therefore the prudent shall keepe silence in that time, for it is an euill time.
Kwa hiyo mtu mwenye busara hunyamaza kimya nyakati kama hizo, kwa kuwa nyakati ni mbaya.
14 Seeke good and not euil, that ye may liue: and the Lord God of hostes shalbe with you, as you haue spoken.
Tafuteni mema, wala si mabaya, ili mpate kuishi. Ndipo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote atakuwa pamoja nanyi, kama msemavyo yupo nanyi.
15 Hate the euil, and loue the good, and establish iudgement in the gate: it may bee that the Lord God of hostes will be mercifull vnto the remnant of Ioseph.
Yachukieni maovu, yapendeni mema; dumisheni haki mahakamani. Yamkini Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote atawahurumia mabaki ya Yosefu.
16 Therfore the Lord God of hosts, the Lord saith thus, Mourning shalbe in all streetes: and they shall say in al the hie wayes, Alas, alas: and they shall call the husbandman to lamentation, and such as can mourne, to mourning.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Kutakuwepo maombolezo katika barabara zote na vilio vya uchungu katika njia kuu zote. Wakulima wataitwa kuja kulia, na waombolezaji waje kuomboleza.
17 And in al the vines shalbe lamentation: for I wil passe through thee, saith the Lord.
Kutakuwepo kuomboleza katika mashamba yote ya mizabibu, kwa kuwa nitapita katikati yenu,” asema Bwana.
18 Woe vnto you, that desire the day of the Lord: what haue you to do with it? the day of the Lord is darkenes and not light.
Ole wenu ninyi mnaoitamani siku ya Bwana! Kwa nini mnaitamani siku ya Bwana? Siku hiyo itakuwa giza, si nuru.
19 As if a man did flee from a lyon, and a beare met him: or went into the house, and leaned his hand on the wall, and a serpent bit him.
Itakuwa kama vile mtu aliyemkimbia simba kumbe akakutana na dubu, kama vile mtu aliyeingia nyumbani mwake na kuupumzisha mkono wake kwenye ukuta, kumbe akaumwa na nyoka.
20 Shal not the day of the Lord be darkenes, and not light? euen darkenes and no light in it?
Je, siku ya Bwana haitakuwa giza, na si nuru: giza nene, bila mwonzi wa mwanga?
21 I hate and abhorre your feast dayes, and I wil not smelll in your solemne assemblies.
“Ninachukia, ninazidharau sikukuu zenu za dini; siwezi kuvumilia makusanyiko yenu.
22 Though ye offer me burnt offrings and meat offrings, I wil not accept them: neither will I regard the peace offrings of your fat beasts.
Hata ingawa mnaniletea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za nafaka, sitazikubali. Ingawa mnaniletea sadaka nzuri za amani, sitazitambua.
23 Take thou away from me the multitude of thy songs (for I wil not heare the melodie of thy violes)
Niondoleeni kelele za nyimbo zenu! Sitasikiliza sauti za vinubi vyenu.
24 And let iudgement runne downe as waters, and righteousnesse as a mightie riuer.
Lakini acheni haki itiririke kama mto, na uadilifu uwe kama kijito kisichokauka!
25 Haue ye offered vnto me sacrifices and offrings in the wildernesse fourtie yeeres, O house of Israel?
“Je, mliniletea dhabihu na sadaka kwa miaka arobaini kule jangwani, ee nyumba ya Israeli?
26 But you haue borne Siccuth your King, and Chiun your images, and the starre of your gods, which ye made to your selues.
Mmeyainua madhabahu ya mfalme wenu, Sikuthi mungu wenu mtawala, na Kiuni mungu wenu wa nyota, ambao mliwatengeneza wenyewe.
27 Therefore wil I cause you to goe into captiuitie beyond Damascus, saith the Lord, whose Name is the God of hostes.
Kwa sababu hiyo nitawapeleka uhamishoni mbali kupita Dameski,” asema Bwana, ambaye jina lake ni Mungu Mwenye Nguvu Zote.

< Amos 5 >