< Acts 4 >

1 And as they spake vnto the people, the Priestes and the Captaine of the Temple, and the Sadduces came vpon them,
Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakizungumza na watu, makuhani na mlinzi wa hekalu na masadukayo waliwaendea.
2 Taking it grieuously that they taught the people, and preached in Iesus Name the resurrection from the dead.
Walikuwa wameudhika sana kwa sababu Petro na Yohana walikuwa wanawafundisha watu kuhusu Yesu na kutangaza juu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
3 And they layde handes on them, and put them in holde, vntill the next day: for it was now euentide.
Waliwakamata na kuwaweka gerezani hadi asubuhi iliyofuata, kwani tayari ilikuwa jioni.
4 Howbeit, many of them which heard the word, beleeued, and the number of the men was about fiue thousand.
Lakini watu wengi waliokuwa wamesikia ujumbe waliamini; na idadi ya wanaume waliokuwa wameamini walikadiliwa kuwa elfu tano.
5 And it came to passe on the morow, that their rulers, and Elders, and Scribes, were gathered together at Hierusalem,
Hata ilipofika asubuhi siku iliyofuata, kwamba wakuu wao, wazee na waandishi, kwa pamoja walikusanyika Yerusalemu.
6 And Annas the chiefe Priest, and Caiaphas, and Iohn, and Alexander, and as many as were of the kindred of the hie Priestes.
Anasi kuhani mkuu alikuwepo, na Kayafa, na Yohana, na Iskanda, na wote waliokuwa ni ndugu wa kuhani mkuu.
7 And whe they had set them before them, they asked, By what power, or in what Name haue ye done this?
Walipokuwa wamewaweka Petro na Yohana katikati yao, waliwauliza, “Kwa uwezo gani, au kwa jina gani mmefanya hili?”
8 Then Peter ful of the holy Ghost, said vnto them, Ye rulers of the people, and Elders of Israel,
Kisha, Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akawaambia, “Ninyi wakuu wa watu, na wazee,
9 For as much as we this day are examined of the good deede done to the impotent man, to wit, by what meanes he is made whole,
kama sisi siku ya leo tunahojiwa kuhusu tendo jema lililofanywa kwa mtu huyu mgonjwa - kwa namna gani mtu huyu alifanywa mzima?
10 Be it knowen vnto you all, and to all the people of Israel, that by the Name of Jesus Christ of Nazareth, whom ye haue crucified, whome God raised againe from the dead, euen by him doth this man stand here before you, whole.
Hebu lijulikane hilo kwenu na kwa watu wote katika Israel, kwamba kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye mlimsulibisha, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, ni kwa njia yake kwamba mtu huyu anasimama hapa mbele yenu akiwa mwenye afya.
11 This is the stone cast aside of you builders which is become the head of the corner.
Yesu Kristo ni jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilidharau, lakini ambalo limefanywa kuwa jiwe kuu la pembeni.
12 Neither is there saluation in any other: for among men there is giuen none other Name vnder heauen, whereby we must be saued.
Hakuna wokovu katika mtu mwingine awaye yote. Kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa watu, ambalo kwa hilo tunaweza kuokolewa.”
13 Now when they sawe the boldnes of Peter and Iohn, and vnderstoode that they were vnlearned men and without knowledge, they marueiled, and knew them, that they had bin with Iesus:
Sasa walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na wakagundua kwamba walikuwa ni watu wakawaida wasio na elimu, walishangaa, wakafahamu kwamba Petro na Yohana wamekuwa pamoja na Yesu.
14 And beholding also the man which was healed standing with them, they had nothing to say against it.
Kwa sababu walimwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuwa na kitu cha kusema dhidi ya hili.
15 Then they commanded them to goe aside out of the Council, and conferred among themselues,
Lakini walipokuwa wamekwisha kuwaamuru mitume waondoke mbele ya mkutano wa baraza, walizungumza wao kwa wao.
16 Saying, What shall we doe to these men? for surely a manifest signe is done by them, and it is openly knowen to all them that dwell in Hierusalem: and we cannot denie it.
Walisema, tutawafanyaje watu hawa? Ni kweli kwamba muujiza wa ajabu umefanyika kupitia wao unajulikana na kila mmoja anayeishi Yerusalemu; hatuwezi kulikataa hilo.
17 But that it be noysed no farther among the people, let vs threaten and charge them, that they speake hencefoorth to no man in this Name.
Lakini, ili kwamba jambo hili lisienee miongoni mwa watu, hebu tuwaonye wasinene tena kwa mtu yeyote kwa jina hili.
18 So they called them, and commanded them, that in no wise they should speake or teach in the Name of Iesus.
Waliwaita Petro na Yohana ndani na kuwaamuru kamwe wasinene wala kufundisha kwa jina la Yesu.
19 But Peter and Iohn answered vnto them, and said, Whether it be right in the sight of God, to obey you rather then God, iudge ye.
Lakini Petro na Yohana walijibu na kuwaambia, “Kama ni sahihi machoni pa Mungu kuwatii ninyi kuliko Mungu, hukumuni wenyewe.
20 For we cannot but speake the things which we haue seene and heard.
Maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.”
21 So they threatened them, and let them goe, and found nothing how to punish them, because of the people: for all men praised God for that which was done.
Baada ya kuwaonya sana Petro na Yohana, waliwaacha waende. Hawakuweza kupata sababu yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetendeka.
22 For the man was aboue fourtie yeeres olde, on whome this miracle of healing was shewed.
Mtu aliyekuwa amepokea muujiza wa uponyaji alipata kuwa na umri zaidi ya miaka arobaini.
23 Then assoone as they were let goe, they came to their fellowes, and shewed all that the hie Priestes and Elders had said vnto them.
Baada ya kuwaacha huru, Petro na Yohana walikuja kwa watu wao na kuwataarifu yote ambayo makuhani wakuu na wazee walikuwa wamewaambia.
24 And when they heard it, they lift vp their voyces to God with one accord, and said, O Lord, thou art the God which hast made the heaue, and the earth, the sea, and all things that are in them,
Walipoyasikia, walipaza sauti zao kwa pamoja kwa Mungu na kusema, “Bwana, wewe uliyeumba mbingu na dunia na bahari na kila kitu ndani yake,
25 Which by the mouth of thy seruant Dauid hast saide, Why did the Gentiles rage, and the people imagine vaine things?
wewe ambaye, kwa Roho Mtakatifu, kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ulisema, “Kwanini watu wa mataifa wamefanya ghasia, na watu wametafakari mambo yasiyofaa?
26 The Kings of the earth assembled, and the rulers came together against the Lord, and against his Christ.
Wafalme wa dunia wamejipanga pamoja, na watawala wamekusanyika kwa pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya masihi wake.”
27 For doutlesse, against thine holy Sonne Iesus, whome thou haddest anoynted, both Herod and Pontius Pilate, with the Gentiles and the people of Israel gathered themselues together,
Ni hakika, wote Herode na Pontio Pilato, pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika kwa pamoja katika mji huu dhidi ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, ambaye ulimpaka mafuta.
28 To doe whatsoeuer thine hand, and thy counsell had determined before to be done.
Walikusanyika kwa pamoja kufanya yote ambayo mkono wako na mapenzi yako yaliyaamuru tangu awali kabla hayajatokea.
29 And nowe, O Lord, beholde their threatnings, and graunt vnto thy seruants with all boldnesse to speake thy word,
Sasa, Bwana, yaangalie matisho yao, na ukawajaalie watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri wote. Ili
30 So that thou stretch forth thine hand, that healing, and signes, and wonders may be done by the Name of thine holy Sonne Iesus.
kwamba unaponyosha mkono wako kuponya, ishara na maajabu viweze kutokea kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.”
31 And when as they had prayed, the place was shaken where they were assembled together, and they were all filled with the holy Ghost, and they spake the word of God boldely.
Walipomaliza kuomba, eneo ambalo walikusanyika kwa pamoja likatikiswa, na wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, na walinena neno la Mungu kwa ujasili.
32 And the multitude of them that beleeued, were of one heart, and of one soule: neither any of them said, that any thing of that which he possessed, was his owne, but they had all thinges common.
Idadi kubwa ya wale walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja: na hakuna hata mmoja wao aliyesema kwamba chochote alichomiliki kilikuwa cha kwake mwenyewe; badala yake walikuwa na vitu vyote shirika.
33 And with great power gaue the Apostles witnes of the resurrection of the Lord Iesus: and great grace was vpon them all.
Kwa nguvu kubwa mitume walikuwa wakiutangaza ushuhuda wao kuhusu ufufuo wa Bwana Yesu, na neema kubwa ilikuwa juu yao wote.
34 Neither was there any among them, that lacked: for as many as were possessours of landes or houses, solde them, and brought the price of the things that were solde,
Hapakuwa na mtu yeyote miongoni mwao aliyepungukiwa na mahitaji, kwa sababu watu wote waliokuwa na hati za viwanja au nyumba, waliviuza na kuleta pesa ya vitu waliyokuwa wameuza
35 And layde it downe at the Apostles feete, and it was distributed vnto euery man, according as he had neede.
na kuviweka chini ya miguu ya mitume. Na mgawanyo ulifanywa kwa kila muumini, kulingana na kila mmoja alivyokuwa na hitaji.
36 Also Ioses which was called of the Apostles, Barnabas (that is by interpretation the sonne of consolation) being a Leuite, and of the countrey of Cyprus,
Yusufu, mlawi, mtu kutoka Kipro, alipewa jina la Barnabasi na mitume (hiyo ikitafasiriwa, ni mwana wa faraja).
37 Where as he had land, solde it, and brought the money, and laid it downe at the Apostles feete.
Akiwa na shamba, aliliuza na akaleta fedha, akaziweka chini ya miguu ya mitume.

< Acts 4 >