< Acts 13 >

1 There were also in the Church that was at Antiochia, certaine Prophets and teachers, as Barnabas, and Simeon called Niger, and Lucius of Cyrene, and Manahen (which had bin brought vp with Herod the Tetrarche) and Saul.
Katika kanisa huko Antiokia ya Shamu walikuwako manabii na walimu, yaani: Barnaba, Simeoni aitwaye Nigeri, Lukio Mkirene, Manaeni aliyekuwa amelelewa pamoja na Mfalme Herode Agripa, na Sauli.
2 Nowe as they ministred to the Lord, and fasted, the holy Ghost said, Separate me Barnabas and Saul, for the worke whereunto I haue called them.
Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, “Nitengeeni Sauli na Barnaba kwa kazi ile maalum niliyowaitia.”
3 Then fasted they and prayed, and layde their hands on them, and let them goe.
Ndipo baada ya kufunga na kuomba, wakawawekea mikono yao na wakawatuma waende zao.
4 And they, after they were sent foorth of the holy Ghost, came downe vnto Seleucia, and from thence they sayled to Cyprus.
Hivyo, wakiwa wametumwa na Roho Mtakatifu, wakashuka kwenda Seleukia na kutoka huko wakasafiri baharini mpaka kisiwa cha Kipro.
5 And when they were at Salamis, they preached the worde of God in the Synagogues of the Iewes: and they had also Iohn to their minister.
Walipowasili katika mji wa Salami, wakahubiri neno la Mungu katika sinagogi la Wayahudi. Pia walikuwa na Yohana Marko kuwa msaidizi wao.
6 So when they had gone throughout the yle vnto Paphus, they found a certaine sorcerer, a false prophet, being a Iewe, named Bariesus,
Walipokwisha kupita katika nchi zote hizo wakafika Pafo, ambapo walikutana na Myahudi mmoja mchawi aliyekuwa nabii wa uongo, jina lake Bar-Yesu.
7 Which was with the Deputie Sergius Paulus, a prudent man. He called vnto him Barnabas and Saul, and desired to heare the woorde of God.
Mtu huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mtu mwenye hekima aliyekuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala wa kile kisiwa. Sergio Paulo akawaita Sauli na Barnaba akitaka kusikia neno la Mungu.
8 But Elymas, ye sorcerer (for so is his name by interpretation) withstoode them, and sought to turne away the Deputie from the faith.
Lakini Elima yule mchawi (hii ndiyo maana ya jina lake), aliwapinga Barnaba na Sauli na kujaribu kumpotosha yule mkuu wa kile kisiwa aiache imani.
9 Then Saul (which also is called Paul) being full of the holy Ghost, set his eyes on him,
Ndipo Sauli, ambaye pia aliitwa Paulo, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akamkazia macho Elima huyo mchawi,
10 And sayde, O full of all subtiltie and all mischiefe, the childe of the deuill, and enemie of all righteousnesse, wilt thou not cease to peruert the straight waies of the Lord?
akamwambia, “Ewe mwana wa ibilisi, wewe ni adui wa kila kilicho haki! Umejaa kila aina ya udanganyifu na ulaghai. Je, hutaacha kuzipotosha njia za Bwana zilizonyooka?
11 Nowe therefore behold, the hand of the Lord is vpon thee, and thou shalt be blinde, and not see the sunne for a season. And immediately there fel on him a mist and a darknes; and he went about, seeking some to leade him by the hand.
Nawe sasa sikiliza, mkono wa Bwana u dhidi yako. Utakuwa kipofu, wala hutaona jua kwa muda.” Mara ukungu na giza vikamfunika, naye akaenda huku na huko akitafuta mtu wa kumshika mkono ili amwonyeshe njia.
12 Then the Deputie when he sawe what was done, beleeued, and was astonied at the doctrine of the Lord.
Yule mkuu wa kile kisiwa alipoona yaliyotukia, akaamini kwa sababu alistaajabishwa na mafundisho kuhusu Bwana.
13 Nowe when Paul and they that were with him were departed by shippe from Paphus, they came to Perga a citie of Pamphylia: then Iohn departed from them, and returned to Hierusalem.
Kisha Paulo na wenzake wakasafiri toka Pafo wakafika Perga huko Pamfilia. Lakini, Yohana Marko akawaacha huko, akarejea Yerusalemu.
14 But when they departed from Perga, they came to Antiochia a citie of Pisidia, and went into the Synagogue on ye Sabbath day, and sate downe.
Kutoka Perga wakaendelea hadi Antiokia ya Pisidia. Siku ya Sabato wakaingia ndani ya sinagogi, wakaketi.
15 And after the lecture of the Law and Prophets, the rulers of ye Synagogue sent vnto them, saying, Ye men and brethren, if ye haue any word of exhortation for the people, say on.
Baada ya Sheria ya Mose na Kitabu cha Manabii kusomwa, viongozi wa sinagogi wakawatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mna neno la kuwafariji watu hawa, tafadhali lisemeni.”
16 Then Paul stoode vp and beckened with the hand, and sayde, Men of Israel, and yee that feare God, hearken.
Paulo akasimama, akawapungia mkono na kusema: “Enyi wanaume wa Israeli na ninyi nyote mnaomcha Mungu.
17 The God of this people of Israel chose our fathers, and exalted the people when they dwelt in the land of Egypt, and with an high arme brought them out thereof.
Mungu wa watu hawa wa Israeli aliwachagua baba zetu, akawafanya kustawi walipokuwa huko Misri, kwa uwezo mwingi akawaongoza na kuwatoa katika nchi ile.
18 And about the time of fourtie yeeres, suffered he their maners in the wildernesse.
Kwa muda wa miaka arobaini alivumilia matendo yao walipokuwa jangwani.
19 And he destroied seuen nations in the land of Chanaan, and deuided their lad to them by lot.
Naye baada ya kuyaangamiza mataifa saba waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, akawapa Waisraeli nchi yao iwe urithi wao.
20 Then afterward he gaue vnto them Iudges about foure hundreth and fiftie yeeres, vnto the time of Samuel the Prophet.
Haya yote yalichukua kama muda wa miaka 450. “Baada ya haya, Mungu akawapa waamuzi mpaka wakati wa nabii Samweli.
21 So after that, they desired a King, and God gaue vnto them Saul, the sonne of Cis, a man of ye tribe of Beniamin, by the space of fourty yeres.
Ndipo watu wakaomba wapewe mfalme, naye Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi wa kabila la Benyamini, aliyetawala kwa miaka arobaini.
22 And after he had taken him away, he raised vp Dauid to be their King, of whom he witnessed, saying, I haue found Dauid the sonne of Iesse, a man after mine owne heart, which will doe all things that I will.
Baada ya kumwondoa Sauli katika ufalme, akawainulia Daudi kuwa mfalme wao. Mungu pia alimshuhudia, akisema, ‘Nimemwona Daudi mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayetimiza mapenzi yangu yote.’
23 Of this mans seede hath God according to his promise raised vp to Israel, ye Sauiour Iesus:
“Kutoka uzao wa mtu huyu, Mungu amewaletea Israeli Mwokozi Yesu, kama alivyoahidi.
24 When Iohn had first preached before his coming the baptisme of repentance to all the people of Israel.
Kabla ya kuja kwa Yesu, Yohana alihubiri toba na ubatizo kwa watu wote wa Israeli.
25 And when Iohn had fulfilled his course, he saide, Whom ye thinke that I am, I am not he: but beholde, there commeth one after me, whose shooe of his feete I am not worthy to loose.
Yohana alipokuwa anakamilisha kazi yake, alisema: ‘Ninyi mnadhani mimi ni nani? Mimi si yeye. La hasha, lakini yeye yuaja baada yangu, ambaye mimi sistahili kufungua kamba za viatu vya miguu yake.’
26 Yee men and brethren, children of the generation of Abraham, and whosoeuer among you feareth God, to you is the woorde of this saluation sent.
“Ndugu zangu, wana wa Abrahamu, nanyi watu wa Mataifa mnaomcha Mungu, ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
27 For the inhabitants of Hierusalem, and their rulers, because they knewe him not, nor yet the woordes of the Prophets, which are read euery Sabbath day, they haue fulfilled them in condemning him.
Kwa sababu wakaao Yerusalemu na viongozi wao hawakumtambua wala kuelewa maneno ya manabii yasomwayo kila Sabato, bali waliyatimiza maneno hayo kwa kumhukumu yeye.
28 And though they found no cause of death in him, yet desired they Pilate to kill him.
Ijapokuwa hawakupata sababu yoyote ya kumhukumu kifo, walimwomba Pilato aamuru auawe.
29 And when they had fulfilled all things that were written of him, they tooke him downe from the tree, and put him in a sepulchre.
Walipokwisha kufanya yale yote yaliyoandikwa kumhusu, walimshusha kutoka msalabani na kumzika kaburini.
30 But God raised him vp from the dead.
Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu.
31 And hee was seene many dayes of them, which came vp with him from Galile to Hierusalem, which are his witnesses vnto the people.
Naye kwa siku nyingi akawatokea wale waliokuwa pamoja naye kuanzia Galilaya hadi Yerusalemu. Nao sasa wamekuwa mashahidi wake kwa watu wetu.
32 And we declare vnto you, that touching the promise made vnto the fathers,
“Nasi tunawaletea habari njema, kwamba yale Mungu aliyowaahidi baba zetu
33 God hath fulfilled it vnto vs their children, in that he raised vp Iesus, euen as it is written in the seconde Psalme, Thou art my Sonne: this day haue I begotten thee.
sasa ameyatimiza kwetu sisi watoto wao, kwa kumfufua Yesu, kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili: “‘Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa.’
34 Nowe as concerning that he raised him vp from the dead, no more to returne to corruption, he hath said thus, I wil giue you the holy things of Dauid, which are faithfull.
Kwa kuwa Mungu alimfufua kutoka kwa wafu asioze kamwe, alitamka maneno haya: “‘Nitakupa wewe baraka takatifu zilizo za hakika nilizomwahidi Daudi.’
35 Wherefore hee sayeth also in another place, Thou wilt not suffer thine Holy one to see corruption.
Kama ilivyosemwa mahali pengine katika Zaburi, “‘Hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu.’
36 Howbeit, Dauid after hee had serued his time by the counsell of God, hee slept, and was laid with his fathers, and sawe corruption.
“Kwa maana Daudi akiisha kulitumikia kusudi la Mungu katika kizazi chake, alilala; akazikwa pamoja na baba zake na mwili wake ukaoza.
37 But he whom God raised vp, sawe no corruption.
Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu hakuona uharibifu.
38 Be it knowen vnto you therefore, men and brethren, that through this man is preached vnto you the forgiuenesse of sinnes.
“Kwa hiyo ndugu zangu, nataka ninyi mjue kwamba kwa kupitia huyu Yesu msamaha wa dhambi unatangazwa kwenu.
39 And from al things, from which ye could not be iustified by the Law of Moses, by him euery one that beleeueth, is iustified.
Kwa kupitia yeye, kila mtu amwaminiye anahesabiwa haki kwa kila kitu ambacho asingeweza kuhesabiwa haki kwa sheria ya Mose.
40 Beware therefore lest that come vpon you, which is spoken of in the Prophets,
Kwa hiyo jihadharini ili yale waliyosema manabii yasiwapate:
41 Behold, ye despisers, and wonder, and vanish away: for I woorke a woorke in your daies, a woorke which yee shall not beleeue, if a man would declare it you.
“‘Angalieni, enyi wenye dhihaka, mkastaajabu, mkaangamie, kwa maana nitatenda jambo wakati wenu ambalo hamtasadiki, hata kama mtu akiwaambia.’”
42 And when they were come out of the Synagogue of the Iewes, the Gentiles besought, that they woulde preach these woordes to them the next Sabbath day.
Paulo na Barnaba walipokuwa wakitoka nje ya sinagogi, watu wakawaomba wazungumze tena mambo hayo Sabato iliyofuata.
43 Nowe when the congregation was dissolued, many of the Iewes and Proselytes that feared God, followed Paul and Barnabas, which spake to them, and exhorted them to continue in the grace of God.
Baada ya kusanyiko la Sinagogi kutawanyika, wengi wa Wayahudi na waongofu wa dini ya Kiyahudi wakawafuata Paulo na Barnaba, wakazungumza nao na kuwahimiza wadumu katika neema ya Mungu.
44 And ye next Sabbath day came almost the whole citie together, to heare the worde of God.
Sabato iliyofuata, karibu watu wote wa mji walikuja kusikiliza neno la Bwana.
45 But when the Iewes saw the people, they were full of enuie, and spake against those things, which were spoken of Paul, contrarying them, and railing on them.
Lakini Wayahudi walipoona ule umati mkubwa wa watu walijawa na wivu, wakayakanusha maneno Paulo aliyokuwa akisema.
46 Then Paul and Barnabas spake boldly, and sayde, It was necessarie that the woorde of God shoulde first haue beene spoken vnto you: but seeing yee put it from you, and iudge your selues vnworthie of euerlasting life, loe, we turne to the Gentiles. (aiōnios g166)
Ndipo Paulo na Barnaba wakawajibu kwa ujasiri, wakisema, “Ilitupasa kunena nanyi neno la Mungu kwanza. Lakini kwa kuwa mmelikataa, mkajihukumu wenyewe kuwa hamstahili uzima wa milele, sasa tunawageukia watu wa Mataifa. (aiōnios g166)
47 For so hath the Lord commanded vs, saying, I haue made thee a light of the Gentiles, that thou shouldest be the saluation vnto the end of the world.
Kwa maana hili ndilo Bwana alilotuamuru: “‘Nimewafanya ninyi kuwa nuru kwa watu wa Mataifa, ili mpate kuuleta wokovu hadi miisho ya dunia.’”
48 And when the Gentiles heard it, they were glad, and glorified the woorde of the Lord: and as many as were ordeined vnto eternall life, beleeued. (aiōnios g166)
Watu wa Mataifa waliposikia haya wakafurahi na kulitukuza neno la Bwana; nao wote waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. (aiōnios g166)
49 Thus the worde of the Lord was published throughout the whole countrey.
Neno la Bwana likaenea katika eneo lile lote.
50 But the Iewes stirred certaine deuoute and honourable women, and the chiefe men of the citie, and raised persecution against Paul and Barnabas, and expelled them out of their coastes.
Lakini Wayahudi wakawachochea wanawake wenye kumcha Mungu, wenye vyeo pamoja na watu maarufu katika mji, wakachochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na kuwafukuza kutoka eneo hilo.
51 But they shooke off the dust of their feete against them, and came vnto Iconium.
Hivyo Paulo na Barnaba wakakungʼuta mavumbi ya miguu yao ili kuwapinga, nao wakaenda Ikonio.
52 And the disciples were filled with ioy, and with the holy Ghost.
Wanafunzi wakajawa na furaha na Roho Mtakatifu.

< Acts 13 >