< Acts 11 >

1 Nowe the Apostles and the brethren that were in Iudea, heard, that the Gentiles had also receiued the worde of God.
Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
2 And when Peter was come vp to Hierusalem, they of the circumcision contended against him,
Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
3 Saying, Thou wentest in to men vncircumcised, and hast eaten with them.
“Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
4 Then Peter beganne, and expounded the thing in order to them, saying,
Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
5 I was in the citie of Ioppa, praying, and in a trance I sawe this vision, A certaine vessell comming downe as it had bene a great sheete, let downe from heauen by the foure corners, and it came to me.
“Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
6 Towarde the which when I had fastened mine eyes, I considered, and sawe foure footed beastes of the earth, and wilde beastes, and creeping things, and foules of the heauen.
Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
7 Also I heard a voyce, saying vnto me, Arise, Peter: slay and eate.
Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8 And I said, God forbid, Lord: for nothing polluted or vncleane hath at any time entred into my mouth.
Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9 But the voyce answered me the seconde time from heauen, The things that God hath purified, pollute thou not.
Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10 And this was done three times, and all were taken vp againe into heauen.
Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11 Then behold, immediatly there were three men already come vnto the house where I was, sent from Cesarea vnto me.
Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12 And the Spirit saide vnto me, that I should go with them, without doubting: moreouer these sixe brethren came with me, and we entred into the mans house.
Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
13 And he shewed vs, howe he had seene an Angel in his house, which stoode and said to him, Send men to Ioppa, and call for Simon, whose surname is Peter.
Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
14 He shall speake wordes vnto thee, whereby both thou and all thine house shalbe saued.
Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
15 And as I began to speake, the holy Ghost fell on them, euen as vpon vs at the beginning.
Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
16 Then I remembred the word of the Lord, howe he said, Iohn baptized with water, but ye shalbe baptized with the holy Ghost.
Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
17 For as much then as God gaue them a like gift, as he did vnto vs, when we beleeued in the Lord Iesus Christ, who was I, that I coulde let God?
Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?”
18 When they heard these things, they helde their peace, and glorified God, saying, Then hath God also to the Gentiles graunted repentance vnto life.
Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, “Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!”
19 And they which were scattered abroade because of the affliction that arose about Steuen, went throughout till they came vnto Phenice and Cyprus, and Antiochia, preaching the worde to no man, but vnto the Iewes onely.
Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
20 Now some of them were men of Cyprus and of Cyrene, which when they were come into Antiochia, spake vnto the Grecians, and preached the Lord Iesus.
Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21 And the hand of the Lord was with them, so that a great number beleeued and turned vnto the Lord.
Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
22 Then tydings of those things came vnto the eares of the Church, which was in Hierusalem, and they sent foorth Barnabas, that he should goe vnto Antiochia.
Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23 Who when he was come and had seene the grace of God, was glad, and exhorted all, that with purpose of heart they would continue in the Lord.
Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24 For he was a good man, and full of the holy Ghost, and faith, and much people ioyned them selues vnto the Lord.
Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25 Then departed Barnabas to Tarsus to seeke Saul:
Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26 And when he had founde him, he brought him vnto Antiochia: and it came to passe that a whole yere they were conuersant with ye Church, and taught much people, in so much that the disciples were first called Christians in Antiochia.
Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
27 In those dayes also came Prophets from Hierusalem vnto Antiochia.
Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28 And there stoode vp one of them named Agabus, and signified by the Spirit, that there should be great famine throughout all the world, which also came to passe vnder Claudius Cesar.
Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29 Then the disciples, euery man according to his ability, purposed to sende succour vnto the brethren which dwelt in Iudea.
Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30 Which thing they also did, and sent it to the Elders, by the hand of Barnabas and Saul.
Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.

< Acts 11 >