< 2 Timothy 2 >

1 Thou therefore, my sonne, be strong in the grace that is in Christ Iesus.
Basi, wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo ndani ya Kristo Yesu.
2 And what things thou hast heard of me, by many witnesses, ye same deliuer to faithfull men, which shalbe able to teache other also.
Nayo mambo yale uliyonisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu watakaoweza kuwafundisha watu wengine vilevile.
3 Thou therefore suffer affliction as a good souldier of Iesus Christ.
Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu.
4 No man that warreth, entangleth himselfe with the affaires of this life, because he woulde please him that hath chosen him to be a souldier.
Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.
5 And if any man also striue for a Masterie, he is not crowned, except he striue as he ought to doe.
Vivyo hivyo, yeye ashindanaye katika michezo hawezi kupewa tuzo ya ushindi asiposhindana kulingana na kanuni za mashindano.
6 The husbandman must labour before he receiue the fruites.
Mkulima mwenye bidii ya kazi ndiye anayestahili kuwa wa kwanza kupata fungu la mavuno.
7 Consider what I say: and the Lord giue thee vnderstanding in all things:
Fikiri sana kuhusu haya nisemayo, kwa maana Bwana atakupa ufahamu katika mambo hayo yote.
8 Remember that Iesus Christ, made of the seede of Dauid, was raysed againe from the dead according to my Gospel,
Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yeye aliye wa uzao wa Daudi. Hii ndiyo Injili yangu,
9 Wherein I suffer trouble as an euill doer, euen vnto bondes: but the worde of God is not bounde.
ambayo kwayo ninateseka hata kufikia hatua ya kufungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halifungwi.
10 Therefore I suffer all things, for the elects sake, that they might also obtaine the saluation which is in Christ Iesus, with eternall glorie. (aiōnios g166)
Kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi wao nao wapate wokovu ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios g166)
11 It is a true saying, For if we be dead together with him, we also shall liue together with him.
Hili ni neno la kuaminiwa: Kwa maana kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
12 If we suffer, we shall also reigne together with him: if we denie him, he also will denie vs.
Kama tukistahimili, pia tutatawala pamoja naye. Kama tukimkana yeye, naye atatukana sisi.
13 If we beleeue not, yet abideth he faithfull: he cannot denie himselfe.
Kama tusipoamini, yeye hudumu kuwa mwaminifu, kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
14 Of these things put them in remembrance, and protest before the Lord, that they striue not about wordes, which is to no profit, but to the peruerting of the hearers.
Endelea kuwakumbusha mambo haya ukiwaonya mbele za Bwana waache kushindana kwa maneno ambayo hayana faida yoyote bali huwaangamiza tu wale wanaoyasikia.
15 Studie to shewe thy selfe approued vnto God, a workeman that needeth not to be ashamed, diuiding the worde of trueth aright.
Jitahidi kujionyesha kwa Mungu kuwa umekubaliwa naye, mtendakazi asiye na sababu ya kuona aibu, ukilitumia kwa usahihi neno la kweli.
16 Stay prophane, and vaine babblings: for they shall encrease vnto more vngodlinesse.
Jiepushe na maneno mabaya, yasiyo na maana, yasiyo ya utauwa, kwa maana hayo huzidi kuwatosa watu katika kukosa heshima kwa Mungu.
17 And their worde shall fret as a canker: of which sort is Hymeneus and Philetus,
Mafundisho yao yataenea kama kidonda kisichopona. Miongoni mwao wamo Himenayo na Fileto
18 Which as concerning ye trueth haue erred from the marke, saying that the resurrection is past alreadie, and do destroy the faith of certaine.
ambao wameiacha kweli, wakisema kwamba ufufuo wa wafu umekwisha kuwako, nao huharibu imani ya baadhi ya watu.
19 But the foundation of God remaineth sure, and hath this seale, The Lord knoweth who are his: and, Let euery one that calleth on the Name of Christ, depart from iniquitie.
Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, ukiwa na muhuri wenye maandishi haya: “Bwana anawajua walio wake”; tena, “Kila alitajaye jina la Bwana, na auache uovu.”
20 Notwithstanding in a great house are not onely vessels of gold and of siluer, but also of wood and of earth, and some for honour, and some vnto dishonour.
Katika nyumba kubwa si kwamba kuna vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali pia vimo vyombo vya miti na vya udongo; vingine kwa matumizi maalum, na vingine kwa matumizi ya kawaida.
21 If any man therefore purge him selfe from these, he shalbe a vessell vnto honour, sanctified, and meete for the Lord, and prepared vnto euery good worke.
Basi ikiwa mtu amejitakasa na kujitenga na hayo niliyoyataja, atakuwa chombo maalum, kilichotengwa na ambacho kinamfaa mwenye nyumba, kimeandaliwa tayari kwa kila kazi njema.
22 Flee also from the lustes of youth, and follow after righteousnes, faith, loue, and peace, with them that call on the Lord with pure heart,
Zikimbie tamaa mbaya za ujana, ufuate haki, imani, upendo na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
23 And put away foolish and vnlearned questions, knowing that they ingender strife.
Jiepushe na mabishano ya kipumbavu na yasiyo na maana, kwa kuwa wajua ya kwamba hayo huzaa magomvi.
24 But the seruant of ye Lord must not striue, but must be gentle toward all men, apt to teache, suffering the euill,
Tena haimpasi mtumishi wa Bwana kuwa mgomvi, bali inampasa awe mwema kwa kila mtu, awezaye kufundisha, tena mvumilivu.
25 Instructing them with meekenesse that are contrary minded, prouing if God at any time will giue them repentance, that they may acknowledge the trueth,
Inampasa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye, kwa matumaini kwamba Mungu atawajalia kutubu na kuijua kweli,
26 And come to amendment out of that snare of the deuil, of whom they are taken prisoners, to doe his will.
ili fahamu zao ziwarudie tena, nao waponyoke katika mtego wa ibilisi ambaye amewateka wapate kufanya mapenzi yake.

< 2 Timothy 2 >