< 2 Samuel 8 >

1 After this now, Dauid smote the Philistims, and subdued them, and Dauid tooke the bridle of bondage out of the hand of the Philistims.
ikawa baada ya haya Daudi aliwashambulia Wafilisti na kuwashinda. Hivyo Daudi akaichukua Gathi na vijiji vyake kutoka katika mamlaka ya wafilisti.
2 And hee smote Moab, and measured them with a corde, and cast them downe to the ground: he measured them with two cordes to put them to death, and with one full corde to keepe them aliue: so became the Moabites Dauids seruants, and brought giftes.
Kisha akaishinda Moabu na akawapima watu wake kwa mstari kwa kuwafanya walale chini juu ya ardhi. Alipima mistari miwili ya kuua, na mstari mmoja kamili kuwahifadhi hai. Hivyo Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakaanza kumlipa kodi.
3 Dauid smote also Hadadezer the sonne of Rehob King of Zobah, as he went to recouer his border at the riuer Euphrates.
Kisha Daudi akamshinda Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, Hadadezeri aliposafiri kuurudisha ufalme wake katika mto Frati.
4 And Dauid tooke of them a thousand and seuen hundreth horsemen, and twenty thousande footemen, and Dauid destroyed all the charets, but he reserued an hundreth charets of them.
Daudi aliteka magari 1, 700 ya farasi na askari ishirini elfu waendao kwa miguu. Daudi akawakata miguu farasi wa magari, lakini akahifadhi wakutosha magari mia moja.
5 Then came the Aramites of Dammesek to succour Hadadezer king of Zobah, but Dauid slewe of the Aramites two and twenty thousande men.
Wakati Washami wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadeziri mfalme wa Soba, Daudi akaua katika Washami watu ishirini na mbili elfu.
6 And Dauid put a garison in Aram of Damesek: and the Aramites became seruants to Dauid, and brought gifts. And the Lord saued Dauid wheresoeuer he went.
Daudi akaweka ngome huko Shamu ya Dameski, na Washami wakawa watumishi wake na wakaleta kodi. Yahwe akampa Daudi ushindi kila alikokwenda.
7 And Dauid tooke the shieldes of gold that beloged to the seruants of Hadadezer, and brought them to Ierusalem.
Daudi akachukua ngao za dhahabu walizokuwa nazo watumishi wa Hadadezeri naye akazileta Yerusalemu.
8 And out of Betah, and Berothai (cities of Hadadezer) king Dauid brought exceeding much brasse.
Mfalme Daudi akachukua shaba nyingi kutoka Beta na Berosai, miji ya Hadadezeri.
9 Then Toi king of Hamath heard howe Dauid had smitten all the hoste of Hadadezer,
Wakati Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
10 Therefore Toi sent Ioram his sonne vnto King Dauid, to salute him, and to reioyce with him because he had fought against Hadadezer, and beaten him (for Hadadezer had warre with Toi) who brought with him vessels of siluer, and vessels of golde, and vessels of brasse.
Tou akamtuma Hadoramu mwanawe kwa mfalme Daudi kumpa salamu na kumbariki, kwa kuwa Daudi alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumshinda, maana Hadadezeri alikuwa amepiga vita dhidi ya Tou. Hadoramu akaja pamoja na vitu vya fedha, dhahabu, na shaba.
11 And King Dauid did dedicate them vnto the Lord with the siluer and golde that he had dedicate of all the nations, which he had subdued:
Mfalme Daudi akaviweka wakfu vitu hivi kwa ajili ya Yahwe, pamoja na fedha na dhahabu kutoka katika mataifa yote aliyokuwa ameyashinda-
12 Of Aram, and of Moab, and of the children of Ammon, and of the Philistims, and of Amalek, and of the spoyle of Hadadezer ye sonne of Rehob King of Zobah.
kutoka Shamu, Moabu, Waamoni, Wafilist, Waamaleki, pamoja na nyara zote alizoziteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
13 So Dauid gate a name after that hee returned, and had slayne of the Aramites in the valley of salt eighteene thousand men.
Jina la Daudi likajulikana sana alipowashinda washami katika bonde la Chumvi, pamoja na watu wao wapatao elfu kumi na nane.
14 And he put a garison in Edom: throughout all Edom put he souldiers, and all they of Edom became Dauids seruants: and the Lord kept Dauid whithersoeuer he went.
Akaweka ngome katika Edomu yote, na Waedomu wote wakawa watumishi wake. Yahwe akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
15 Thus Dauid reigned ouer all Israel, and executed iudgement and iustice vnto all his people.
Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akatenda kwa haki na usawa kwa watu wote.
16 And Ioab the sonne of Zeruiah was ouer the hoste, and Ioshaphat the sonne of Ahilud was recorder.
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwenye kuandika taarifa.
17 And Zadok the sonne of Ahitub, and Ahimelech the sonne of Abiathar were the Priestes, and Seraiah the Scribe.
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Seraya alikuwa mwandishi.
18 And Benaiah the sonne of Iehoiada and the Cherethites and the Pelethites, and Dauids sonnes were chiefe rulers.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.

< 2 Samuel 8 >