< 2 Samuel 23 >

1 These also be the last wordes of Dauid, Dauid the sonne of Ishai saith, euen the man who was set vp on hie, the Anointed of the God of Iacob, and the sweete singer of Israel saith,
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi-Daudi mwana wa Yese, mtu aliyeheshimiwa sana, aliyetiwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwandishi mzuri wa zaburi wa Israeli.
2 The Spirit of the Lord spake by me, and his worde was in my tongue.
“Roho ya Yahwe alisema nami, na neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
3 The God of Israel spake to me, ye strength of Israel saide, Thou shalt beare rule ouer men, being iust, and ruling in the feare of God.
Mungu wa Israeli alinena, Mwamba wa Israeli aliniambia, “Atawalaye kwa haki juu yangu, atawalaye katika hofu ya Mungu.
4 Euen as the morning light when the sunne riseth, the morning, I say, without cloudes, so shall mine house be, and not as the grasse of the earth is by the bright raine.
Atakuwa kama nuru ya asubuhi jua linapochomoza, asubuhi isiyo na mawingu, wakati mche mwororo unapochipua kutoka ardhini kupitia mwangaza wa mng'ao wa jua baada ya mvua.
5 For so shall not mine house be with God: for he hath made with me an euerlasting couenant, perfite in all pointes, and sure: therefore all mine health and whole desire is, that he will not make it growe so.
Hakika, je familia yangu haiko hivi mbele za Mungu? Je hajafanya nami agano la milele, taratibu la uhakika kwa kila njia? Je yeye haongezi wokovu wangu na kutimiza kila hitaji langu?
6 But the wicked shalbe euery one as thornes thrust away, because they can not be taken with handes.
Lakini yasiyofaa yote yatakuwa kama miiba na kutupwa mbali, kwa maana haiwezekani kukusanywa kwa mikono.
7 But the man that shall touch them, must be defensed with yron, or with the shaft of a speare: and they shall be burnt with fire in the same place.
Ayagusaye ni lazima atumie chombo cha chuma au au fumo la mkuki. Ni lazima yachomwe mahali yalipo.
8 These be the names of the mightie men whome Dauid had. He that sate in the seate of wisedome, being chiefe of the princes, was Adino of Ezni, he slewe eight hundreth at one time.
Haya ni majina ya askari wa Daudi: Yashobeamu Mhakmoni alikuwa kiongozi wa mashujaa. Aliua watu mia nne wakati mmoja.
9 And after him was Eleazar the sonne of Dodo, the sonne of Ahohi, one of the three worthies with Dauid, when they defied the Philistims gathered there to battel, when the men of Israel were gone vp.
Baada yake alikuwa Elieza mwana wa Dodo, mwana wa mwahohi, mmoja wa mashujaa watatu wa Daudi. Alikuwepo walipowashinda Wafilisti waliokuwa wamekusanyika kwa vita, na wakati watu wa Israeli walipokuwa wamekimbia.
10 He arose and smote the Philistims vntill his hande was wearie, and his hande claue vnto the sworde: and the Lord gaue great victorie the same day, and the people returned after him onely to spoyle.
Elieza akasimama na kuwapiga Wafilisti mpaka mkono wake ukachoka, mpaka mkono wake ukang'ang'ania mpini wa upanga wake. Siku hiyo Yahwe akatoa ushindi mkuu. Jeshi likarejea kwa ajili ya kuteka tu nyara za waliouawa na Elieza.
11 After him was Shammah the sonne of Age the Hararite: for the Philistims assembled at a towne, where was a piece of a fielde full of lentils, and the people fled from the Philistims.
Baada yake alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti wakajikusanya pamoja palipokuwa na shamba la dengu, na jeshi likawakimbia.
12 But he stoode in the middes of the fielde, and defended it, and slewe the Philistims: so the Lord gaue great victorie.
Lakini Shama akasimama katikati ya shamba na kulitetea. Aliwauwa Wafilisti, na Yahwe akaleta ushindi mkuu.
13 Afterward three of the thirtie captaines went downe, and came to Dauid in the haruest time vnto the caue of Adullam, and the hoste of the Philistims pitched in the valley of Rephaim.
Watatu kati ya askari thelathini walishuka kwa Daudi nyakati za mavuno, katika pango la Adulamu. Jeshi la Wafilisti lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Mrefai.
14 And Dauid was then in an holde, and the garison of ye Philistims was then in Beth-lehem.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, wakati Wafilisti walikuwa wanaimilk Bethlehemu.
15 And Dauid longed, and said, Oh, that one would giue me to drinke of the water of the well of Beth-lehem, which is by the gate.
Daudi alitamani maji na akasema, “Kama ingekuwa mtu mmoja angenipa maji ya kunywa kutoka kisima kilichopo Bethlehemu, kisima kilichopo langoni!”
16 The the three mightie brake into the host of the Philistims, and drew water out of the well of Beth-lehem that was by the gate, and tooke and brought it to Dauid, who woulde not drinke thereof, but powred it for an offring vnto ye Lord,
Hivyo mashujaa hawa watatu wakapita kati ya jeshi la Wafilisti na kuchota maji katika kisima cha Bethlehemu, kilichopo langoni. Wakachukua maji na kuyaleta kwa Daudi, lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake akayamwaga mbele za Yahwe.
17 And said, O Lord, be it farre from me, that I should doe this. Is not this the blood of the men that went in ieopardie of their liues? therefore he woulde not drinke it. These things did these three mightie men.
Kisha akasema, “Iwe mbali nami, Yahwe, kwamba niyanywe haya. Je ninywe damu ya watu waliohatarisha maisha yao?” Hivyo akakataa kuyanywa. Haya ni mambo yaliyofanywa na mashujaa watatu.
18 And Abishai the brother of Ioab, the sonne of Zeruiah, was chiefe among the three, and he lifted vp his speare against three hundreth, and slewe them, and he had the name among the three.
Abishai, nduguye Yoabu na mwana wa Seruya, alikuwa akida wa watatu. Alipigana kwa mkuki wake na watu mia tatu na akawauwa wote mara. Mara kwa mara alitajwa kati ya mashujaa watatu.
19 For he was most excellent of the three, and was their captaine, but he attained not vnto the first three.
Hakuwa maarufu kuliko wale watatu? Alifanywa akida wao. Lakini, umaarufu wake haukulingana na umaarufu wa wale mashujaa watatu.
20 And Benaiah the sonne of Iehoiada the sonne of a valiant man, which had done many actes, and was of Kabzeel, slewe two strong men of Moab: he went downe also, and slewe a lyon in the middes of a pit in the time of snowe.
Benaya kutoka Kabseeli mwana wa Yehoyada; alikuwa mtu hodari aliyefanya matendo makuu. Aliwauwa wana wawili wa Arieli wa Moabu. Pia alishuka shimoni na kuuwa simba wakati wa theruji.
21 And he slewe an Egyptian a man of great stature, and the Egyptian had a speare in his hande: but he went downe to him with a staffe, and plucked the speare out of the Egyptians hand, and slewe him with his owne speare.
Na alimwua Mmisri aliyekuwa mtu mnene sana. Mmisri alikuwa na mkuki mkononi, lakini Benaya alipigana naye kwa fimbo tu. Aliuchukua mkuki mkononi mwa Mmisri na kisha kumwua nao.
22 These things did Benaiah the sonne of Iehoiada, and had the name among the three worthies.
Benaya mwana wa Yehoyada alifanya matendo haya, naye alitajwa kati ya mashujaa watatu.
23 He was honourable among thirtie, but he atteined not to the first three: and Dauid made him of his counsell.
Alikuwa na heshima kuliko mashujaa thelathini kwa ujumla wao, lakini hakuwa na heshima kama wale mashujaa watatu. Hata hivyo Daudi alimweka kuwa mlinzi wake.
24 Asahel the brother of Ioab was one of the thirtie: Elhanan the sonne of Dodo of Beth-lehem:
Wafuatao ni wale watu thelathini: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
25 Shammah the Harodite: Elika ye Harodite:
Shama Mharodi, Elika Mharodi,
26 Helez the Paltite: Ira the sonne of Ikkesh the Tekoite:
Helesi Mpeloni, Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi,
27 Abiezer the Anethothite: Mebunnai the Husathite:
Abi Ezeri Mwanathothi, Mebunai Mhushathi,
28 Zalmon an Ahohite: Maharai the Netophathite:
Salmoni Mhahoi, Maharai Mnetofathi;
29 Heleb the sonne of Baanah a Netophathite: Ittai the sonne of Ribai of Gibeah of the children of Beniamin:
Helebu mwana wa Baana, Mnetofathi, Itai mwana wa Rabai kutoka Gibea ya Wabenjamini,
30 Benaiah the Pirathonite: Hiddai of the riuer of Gaash:
Benaya Mpirathoni, Hidai wa mabonde ya Gaashi.
31 Abi-albon the Arbathite: Azmaueth the Barhumite:
Abieliboni Mwarbathi, Azmawethi Mbarhumi,
32 Elihaba the Shaalbonite: of the sonnes of Iashen, Ionathan:
Eliaba Mshalboni, wana wa Yasheni, Yonathani mwana wa Shama Mharari;
33 Shammah the Hararite: Ahiam the sonne of Sharar the Hamrite:
Ahiamu mwana wa Sharari Mharari,
34 Eliphelet the sonne of Ahasbai the sonne of Maachathi: Eliam the sonne of Ahithophel the Gilonite:
Elifeleti mwana wa Ahasbai Mmaakathi, Eliamu mwana wa Ahithofeli Mgiloni,
35 Hezrai the Carmelite: Paarai the Arbite:
Hezro Mkarmeli, Parai Mwarbi,
36 Igal the sonne of Nathan of Zobah: Bani the Gadite:
Igali mwana wa Nathani kutoka Soba, Bani kutoka kabila la Gadi,
37 Zelek the Ammonite: Naharai the Becrothite, the armour bearer of Ioab the sonne of Zeruiah:
Zeleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
38 Ira the Ithrite: Gareb the Ithrite:
Ira Mwithri, Garebu Mwithri,
39 Uriiah the Hittite, thirtie and seuen in all.
Uria Mhiti - jumla yao thelathini na wanane.

< 2 Samuel 23 >