< 2 Samuel 14 >

1 Then Ioab the sonne of Zeruiah perceyued, that the Kings heart was toward Absalom,
Yoabu mwana wa Seruya akafahamu kuwa moyo wa mfalme ulikuwa na shauku ya kumwona Absalomu.
2 And Ioab sent to Tekoah, and brought thence a subtile woman, and sayd vnto her, I pray thee, fayne thy selfe to mourne, and nowe put on mourning apparel, and anoynt not thy selfe with oyle: but be as a woman that had now long time mourned for the dead.
Kwa hiyo Yoabu akamtuma mtu fulani kwenda Tekoa na kumleta mwanamke mwenye hekima kutoka huko. Akamwambia huyo mwanamke, “Jifanye uko katika maombolezo. Vaa nguo za kuomboleza, nawe usitumie mafuta yoyote ya uzuri, jifanye kama mwanamke ambaye amekuwa na huzuni kwa siku nyingi kwa ajili ya kufiwa.
3 And come to the King, and speake on this maner vnto him, (for Ioab taught her what she should say).
Kisha nenda kwa mfalme ukazungumze maneno haya.” Naye Yoabu akaweka maneno kinywani mwa yule mwanamke.
4 Then the woman of Tekoah spake vnto the king, and fel downe on her face to the ground, and did obeysance, and sayd, Helpe, O King.
Huyo huyo mwanamke kutoka Tekoa alipofika kwa mfalme, akaanguka kifudifudi kumpa mfalme heshima, akasema, “Ee mfalme, nisaidie!”
5 Then the King sayd vnto her, What aileth thee? And she answered, I am in deede a widow, and mine husband is dead:
Mfalme akamuuliza, “Una shida gani?” Akamwambia, “Mimi ni mjane hasa, mume wangu amekufa.
6 And thine handmayd had two sonnes, and they two stroue together in the fielde: (and there was none to part them) so the one smote the other, and slew him.
Mimi mtumishi wako nilikuwa na wana wawili. Wakapigana wao kwa wao huko shambani wala huko hapakuwa na mtu hata mmoja wa kuwaamua. Mmoja akampiga mwenzake na kumuua.
7 And beholde, the whole familie is risen against thine handmayde, and they sayde, Deliuer him that smote his brother, that we may kill him for the soule of his brother whome hee slewe, that we may destroy the heire also: so they shall quenche my sparkle which is left, and shall not leaue to mine husband neither name nor posteritie vpon the earth.
Sasa ukoo wote umeinuka dhidi ya mtumishi wako, wakisema, ‘Utukabidhi huyo aliyemuua ndugu yake, ili tumuue kwa ajili ya uhai wa ndugu yake ambaye alimuua, nasi hapo tutakuwa tumekatilia mbali na mrithi pia.’ Wakifanya hivyo, watakuwa wamezima tumaini langu lililobaki, mume wangu hataachiwa jina wala mzao katika uso wa dunia.”
8 And the King said vnto the woman, Go to thine house, and I wil giue a charge for thee.
Mfalme akamwambia huyo mwanamke, “Nenda nyumbani, nami nitatoa agizo kwa ajili yako.”
9 Then the woman of Tekoah said vnto the King, My lord, O King, this trespas be on me, and on my fathers house, and the King and his throne be giltlesse.
Lakini huyo mwanamke kutoka Tekoa akamwambia, “Mfalme bwana wangu, lawama na iwe juu yangu na juu ya nyumba ya baba yangu, naye mfalme na kiti chake cha enzi na asiwe na hatia.”
10 And the King sayde, Bring him to me that speaketh against thee, and he shall touche thee no more.
Mfalme akajibu, “Ikiwa mtu yeyote atakusemesha lolote, mlete kwangu, naye hatakusumbua tena.”
11 Then said she, I pray thee, let the King remember the Lord thy God, that thou wouldest not suffer many reuengers of blood to destroy, lest they slay my sonne. And he answered, As the Lord liueth, there shall not one heare of thy sonne fall to the earth.
Huyo mwanamke akasema, “Basi mfalme na amwombe Bwana Mungu wake ili kuzuia mlipiza kisasi cha damu kuongeza juu ya uharibifu, ili kwamba mwanangu asije akaangamizwa.” Mfalme akasema, “Hakika kama aishivyo Bwana, hakuna unywele mmoja wa kichwa cha mwanao utakaoanguka chini.”
12 Then the woman said, I pray thee, let thine handmayde speake a worde to my lord the King. And he sayd, Say on.
Ndipo huyo mwanamke akasema, “Mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa mfalme bwana wangu.” Mfalme akajibu, “Sema.”
13 Then the woman sayde, Wherefore then hast thou thought such a thing against the people of God? or why doeth the King, as one which is faultie, speake this thing, that he will not bring againe his banished?
Huyo mwanamke akasema, “Mbona basi wewe umewaza jambo kama hili dhidi ya watu wa Mungu? Je, mfalme asemapo hili, hajitii hatiani mwenyewe, kwa maana mfalme hajamrudisha mwanawe aliyefukuziwa mbali?
14 For we must needes dye, and we are as water spilt on the ground, which cannot be gathered vp againe: neither doeth God spare any person, yet doeth he appoynt meanes, not to cast out from him, him that is expelled.
Kama vile maji yaliyomwagika ardhini, yasivyoweza kuzoleka tena, hivyo sisi kufa ni lazima. Lakini Mungu haondoi uhai, badala yake, yeye hufanya njia ili kwamba aliyefukuzwa asibaki akiwa amefarikishwa naye.
15 Nowe therefore that I am come to speake of this thing vnto my lord the King, the cause is that the people haue made me afrayd: therefore thine handmayde sayd, Nowe will I speake vnto the King: it may be that the King will perfourme the request of his handmayde.
“Nami sasa nimekuja kusema hili kwa bwana wangu mfalme kwa sababu watu wameniogopesha. Mtumishi wako alifikiri, ‘Nitanena na mfalme, labda mfalme atamfanyia mtumishi wake kile anachoomba.
16 For the King wil heare, to deliuer his handmayde out of the hande of the man that woulde destroy mee, and also my sonne from the inheritance of God.
Labda mfalme atakubali kumwokoa mtumishi wake kutoka mkononi mwa mtu anayejaribu kunikatilia mbali, mimi na mwanangu, kutoka kwenye urithi Mungu aliotupatia.’
17 Therefore thine handmaid sayd, The word of my lord the King shall now be comfortable: for my lorde the King is euen as an Angel of God in hearing of good and bad: therefore the Lord thy God be with thee.
“Basi sasa mtumishi wako anasema, ‘Neno la bwana wangu mfalme na linipatie pumziko, kwa maana bwana wangu mfalme ni kama malaika wa Mungu katika kutambua jema na baya. Bwana Mungu wako na awe pamoja nawe.’”
18 Then the King answered, and said vnto the woman, Hide not from me, I pray thee, the thing that I shall aske thee. And the woman sayde, Let my lord the King now speake.
Basi mfalme akamwambia huyo mwanamke, “Usinifiche jibu kuhusu hilo nitakalokuuliza.” Huyo mwanamke akasema, “Mfalme bwana wangu na aseme.”
19 And the King said, Is not the hand of Ioab with thee in all this? Then the woman answered, and sayd, As thy soule liueth, my lord the King, I will not turne to the right hande nor to the left, from ought that my lorde the King hath spoken: for euen thy seruant Ioab bade mee, and he put all these wordes in the mouth of thine handmayde.
Mfalme akauliza, “Je, mkono wa Yoabu haupo pamoja nawe katika jambo hilo lote?” Huyo mwanamke akajibu, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu mfalme, hakuna yeyote anayeweza kugeuka kulia wala kushoto kutokana na chochote anachosema bwana wangu mfalme. Naam, ni mtumishi wako Yoabu ndiye alinifundisha kufanya hivi, naye ndiye aliweka maneno haya yote kinywani mwa mtumishi wako.
20 For to the intent that I should chage the forme of speach, thy seruant Ioab hath done this thing: but my lord is wise according to the wisdome of an Angel of God to vnderstande all things that are in the earth.
Mtumishi wako Yoabu amefanya hivi ili kubadili hali iliyopo. Bwana wangu ana hekima kama ile ya malaika wa Mungu, hufahamu kila kitu kinachotokea katika nchi.”
21 And the King sayde vnto Ioab, Beholde nowe, I haue done this thing: go then, and bring the yong man Absalom againe.
Mfalme akamwambia Yoabu, “Vyema sana, nitalifanya jambo hili. Nenda, ukamlete kijana Absalomu.”
22 And Ioab fell to the grounde on his face, and bowed himselfe, and thanked the King. Then Ioab sayde, This day thy seruant knoweth, that I haue found grace in thy sight, my lord the King, in that the King hath fulfilled the request of his seruant.
Yoabu akaanguka kifudifudi mpaka ardhini kumpa mfalme heshima, naye akambariki mfalme. Yoabu akasema, “Leo mtumishi wako anajua kuwa amepata kibali machoni pako, bwana wangu mfalme, kwa sababu mfalme amemjalia mtumishi wake ombi lake.”
23 And Ioab arose, and went to Geshur, and brought Absalom to Ierusalem.
Ndipo Yoabu akaenda hadi Geshuri akamrudisha Absalomu Yerusalemu.
24 And the King sayde, Let him turne to his owne house, and not see my face. So Absalom turned to his owne house, and saw not the Kings face.
Lakini mfalme akasema, “Lazima Absalomu aende kwenye nyumba yake mwenyewe; kamwe asiuone uso wangu.” Kwa hiyo Absalomu akaenda kwenye nyumba yake na hakuuona uso wa mfalme.
25 Nowe in all Israel there was none to be so much praysed for beautie as Absalom: from the sole of his foote euen to the toppe of his head there was no blemish in him.
Katika Israeli yote hakuna mtu yeyote aliyesifiwa kwa uzuri wa sura kama Absalomu. Kuanzia utosi wa kichwa chake hadi wayo wa mguu wake hapakuwa na kasoro.
26 And when he polled his head, (for at euery yeeres ende he polled it: because it was too heauie for him, therefore he polled it) he weyghed the heare of his head at two hundreth shekels by the Kings weight.
Kila mara aliponyoa nywele za kichwa chake, kwa kuwa alikuwa akinyoa mara kwa mara zilipokuwa zinamwia nzito, alizipima uzito wake ulikuwa shekeli mia mbili kwa kipimo cha kifalme.
27 And Absalom had three sonnes, and one daughter named Tamar, which was a fayre woman to looke vpon.
Walizaliwa wana watatu na binti mmoja kwa Absalomu. Jina la binti yake aliitwa Tamari, naye akawa mwanamke mzuri wa sura.
28 So Absalom dwelt the space of two yeres in Ierusalem, and saw not the Kings face.
Absalomu akaishi miaka miwili huko Yerusalemu pasipo kuuona uso wa mfalme.
29 Therefore Absalom sent for Ioab to sende him to the King, but he would not come to him: and when he sent againe, he would not come.
Basi Absalomu akamwita Yoabu kwa kusudi la kumtuma kwa mfalme, lakini Yoabu akakataa kuja kwa Absalomu. Ndipo akamwita tena mara ya pili, lakini pia akakataa kuja.
30 Therefore he sayde vnto his seruants, Beholde, Ioab hath a fielde by my place, and hath barley therein: go, and set it on fire: and Absaloms seruants set the field on fire.
Ndipo akawaambia watumishi wake, “Tazama, shamba la Yoabu liko jirani na langu, naye ana shayiri humo. Nendeni mkalitie moto.” Kisha watumishi wa Absalomu wakalitia moto shamba hilo.
31 Then Ioab arose, and came to Absalom vnto his house, and sayd vnto him, Wherefore haue thy seruants burnt my field with fire?
Basi Yoabu akaenda nyumbani kwa Absalomu, akamwambia, “Kwa nini watumishi wako wametia moto shamba langu?”
32 And Absalom answered Ioab, Beholde, I sent for thee, saying, Come thou hither, and I wil send thee to the King for to say, Wherefore am I come from Geshur? It had bene better for me to haue bene there still: nowe therefore let mee see the Kings face: and if there be any trespasse in me, let him kill me.
Absalomu akamwambia Yoabu, “Tazama, nilikutumia ujumbe na kusema, ‘Njoo ili niweze kukutuma kwa mfalme kuuliza, “Kwa nini nimekuja kutoka Geshuri? Ingekuwa bora zaidi kwangu kama ningebaki huko!”’ Sasa basi, nataka kuuona uso wa mfalme, na ikiwa nina hatia ya jambo lolote, basi na aniue.”
33 Then Ioab came to the King, and told him: and he called for Absalom, who came to the King, and bowed himselfe to the grounde on his face before the King, and the King kissed Absalom.
Basi Yoabu akaenda kwa mfalme na kumwambia jambo hili. Kisha mfalme akamwita Absalomu, naye akaingia ndani akasujudu uso wake mpaka ardhini mbele ya mfalme. Naye mfalme akambusu Absalomu.

< 2 Samuel 14 >