< 2 Corinthians 9 >

1 For as touching the ministring to the Saints, it is superfluous for me to write vnto you.
Hakuna haja yangu kuwaandikia kuhusu huduma hii itolewayo kwa ajili ya watakatifu.
2 For I knowe your readinesse of minde, whereof I boast my selfe of you vnto them of Macedonia, and say, that Achaia was prepared a yeere agoe, and your zeale hath prouoked many.
Kwa kuwa ninajua mlivyo na shauku ya kusaidia, nami nimekuwa nikijivuna kwa ajili ya jambo hilo kwa watu wa Makedonia, nikiwaambia kuwa ninyi wa Akaya mmekuwa tayari kutoa tangu mwaka jana na shauku yenu imewachochea wengi wao katika kutoa.
3 Nowe haue I sent the brethren, lest our reioycing ouer you shoulde bee in vaine in this behalfe, that yee (as I haue sayde) be readie:
Lakini sasa nawatuma hawa ndugu ili kujivuna kwetu kuhusu mchango wenu kusiwe maneno matupu, bali mpate kuwa tayari kama nilivyosema mngekuwa tayari.
4 Lest if they of Macedonia come with me, and finde you vnprepared, we (that wee may not say, you) should be ashamed in this my constant boasting.
Kwa maana kama nikija na Mmakedonia yeyote na kuwakuta hamjawa tayari, tutaona aibu kusema chochote juu yenu katika matoleo.
5 Wherefore, I thought it necessarie to exhort the brethren to come before vnto you, and to finish your beneuolence appointed afore, that it might be readie, and come as of beneuolence, and not as of niggardlinesse.
Kwa hivyo niliona ni muhimu niwahimize hawa ndugu watangulie kuja huko kwenu kabla yangu, wafanye mipango ya hayo matoleo ya ukarimu mliyokuwa mmeahidi, ili yawe tayari kama matoleo ya hiari wala si kama ya kutozwa kwa nguvu.
6 This yet remember, that he which soweth sparingly, shall reape also sparingly, and hee that soweth liberally, shall reape also liberally.
Kumbukeni kwamba: Yeyote apandaye kwa uchache pia atavuna kwa uchache, naye apandaye kwa ukarimu pia atavuna kwa ukarimu.
7 As euery man wisheth in his heart, so let him giue, not grudgingly, or of necessitie: for God loueth a cheerefull giuer.
Kila mtu atoe kama anavyokusudia moyoni mwake, si kwa uchoyo au kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo mkunjufu.
8 And God is able to make all grace to abound towarde you, that yee alwayes hauing all sufficiencie in all thinges, may abounde in euery good worke,
Naye Mungu aweza kuwapa kila baraka kwa wingi, ili katika mambo yote kila wakati, mwe na kila kitu mnachohitaji, ili mweze kushiriki kwa wingi katika kila kazi njema.
9 (As it is written, He hath sparsed abroad and hath giuen to the poore: his beneuolence remayneth for euer. (aiōn g165)
Kama ilivyoandikwa: “Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele.” (aiōn g165)
10 Also hee that findeth seede to the sower, will minister likewise bread for foode, and multiplie your seede, and increase the fruites of your beneuolence, )
Yeye ampaye mpanzi mbegu kwa ajili ya kupanda na mkate kuwa chakula, atawapa na kuzizidisha mbegu zenu za kupanda na kuongeza mavuno ya haki yenu.
11 That on all partes yee may bee made rich vnto all liberalitie, which causeth through vs thankesgiuing vnto God.
Mtatajirishwa kwa kila namna ili mpate kuwa wakarimu kila wakati, na kupitia kwetu, ukarimu wenu utamletea Mungu shukrani.
12 For the ministration of this seruice not onely supplieth the necessities of the Saintes, but also aboundantly causeth many to giue thankes to God,
Huduma hii mnayofanya si tu kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watakatifu, bali huzidi sana kwa shukrani nyingi apewazo Mungu.
13 (Which by the experiment of this ministration praise God for your voluntarie submission to the Gospell of Christ, and for your liberall distribution to them, and to all men)
Kwa sababu ya huduma ambayo mmejithibitisha wenyewe, watu watamtukuza Mungu kwa ajili ya utiifu ufuatanao na ukiri wenu wa Injili ya Kristo, na kwa ukarimu wenu wa kushiriki pamoja nao na pia wengine wote.
14 And in their praier for you, to log after you greatly, for the aboundant grace of God in you.
Nao katika maombi yao kwenu mioyo yao itawaonea shauku kwa sababu ya neema ipitayo kiasi mliyopewa na Mungu.
15 Thankes therefore bee vnto God for his vnspeakeable gift.
Ashukuriwe Mungu kwa karama yake isiyoelezeka.

< 2 Corinthians 9 >