< 2 Chronicles 30 >

1 And Hezekiah sent to all Israel, and Iudah, and also wrote letters to Ephraim and Manasseh, that they should come to the house of the Lord at Ierusalem, to keepe the Passeouer vnto the Lord God of Israel.
Hzekia akatuma wajumbe kwa Israeli wote na Yuda, na pia akawaandikia barua Efraimu na Manase, kwamba waje kwenye nyumba ya Yahwe katika Yerusalemu, kusherekea Pasaka ya Yahwe, Mungu wa Israeli.
2 And the King and his princes and all the Congregation had taken counsel in Ierusalem to keepe the Passeouer in the second moneth.
Kwa maana mfalme, viongozi wake, na kusanyiko lote katika Yerusalemu walikuwa wameshauriana pamoja, wakakubaliana kusherekea Pasaka katika mwezi wa pili.
3 For they could not keepe it at this time, because there were not Priests enow sanctified, neither was the people gathered to Ierusalem.
Hawakuweza kuisherekea mapema kabla ya hapo, kwa sababu hapakuwa na makuhani wa kutosha waliojitakasa wenyewe, wala watu hawakuwa wamekusanyika pamoja Yerusalemu.
4 And the thing pleased the King, and all the Congregation.
Pendekezo hili likaonekana sahihi katika macho ya mfalme na ya kusanyiko lote.
5 And they decreed to make proclamation throughout all Israel from Beersheba euen to Dan, that they should come to keepe the Passeouer vnto the Lord God of Israel at Ierusalem: for they had not done it of a great time, as it was written.
Kwa hiyo wakakubaliana kufanya tangazo katika Israeli yote, kuanzia Beer-sheba hadi Dani, kwamba watu lazima waje kusherehekea Paska ya Yahwe, Mungu wa Israeli, huko Yerusalemu. Kwa maana walikuwa hawakuwa wameisherehekea kwa hesabu kubwa ya watu, kwa mujibu wa jinsi ilivyokuwa imeandikwa.
6 So the postes went with letters by the commission of the King, and his princes, thorowout all Israel and Iudah, and with the commandement of the King, saying, Ye children of Israel, turne againe vnto the Lord God of Abraham, Izhak, and Israel, and he will returne to the remnant that are escaped of you, out of ye hands of the Kings of Asshur.
Hivyo matarishi wakaenda na barua kutoka kwa mfalme na viongozi wake katika Israeli na Yuda yote, kwa agizo la mfalme. wakasema, “Ninyi watu wa Israeli, rudini kwa Yahwe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli, ili kwamba aweze kuwarudia masalia wenu ninyi mlipona kutoka kwenye mkono wa wafalme wa Ashuru.
7 And be not ye like your fathers, and like your brethren, which trespassed against the Lord God of their fathers: and therfore he made them desolate, as ye see.
Msiwe kama babu zenu au ndugu zenu, ambao walimuasi Yahwe, Mungu wa mababu zao, hivyo akawaweka katika kuangamia, kama mnavyoona.
8 Be not ye now stiffenecked like your fathers, but giue the hand to the Lord, and come into his sanctuarie, which he hath sanctified for euer, and serue the Lord your God, and the fiercenesse of his wrath shall turne away from you.
Sasa msiwe wasumbufu, kama babu zenu walivyokuwa; badala yake, jitoeni wenyewe kwa Yahwe na njoeni kwenye sehemu yake takatifu, ambayo ameitakasa milele, na mwabuduni Yahwe Mungu wenu, ili kwamba uso wake wenye hasira uwageukie mbali.
9 For if ye returne vnto the Lord, your brethren and your children shall finde mercy before them that led them captiues, and they shall returne vnto this lande: for the Lord your God is gracious and mercifull, and will not turne away his face from you, if ye conuert vnto him.
Kwa maana ikiwa mtageuka nyuma kwa Yahwe, ndugu zenu na watoto wenu watapata huruma mbele ya hao wanaowaongoza kama wafungwa, na watarudi katika nchi hii. Kwa maana Yahwe Mungu wenu, ni mkarimu na mwenye huruma, na hatawageuzia mbali uso wake, kama mtarudi kwake.”
10 So the postes went from citie to citie thorow the land of Ephraim and Manasseh, euen vnto Zebulun: but they laughed them to scorne, and mocked them.
Kwa hiyo matarishi wakapita mji kwa mji katika majimbo ya Efraimu na Manase, njia yote hadi Zabuloni, lakini watu waliwacheka na kuwazomea.
11 Neuerthelesse diuers of Asher, and Manasseh, and of Zebulun submitted themselues, and came to Ierusalem.
Lakini, watu wengine wa Asheri na Manase na Zabuloni walijinyenyekesha wenyewe na wakaja Yerusalemu.
12 And the hand of God was in Iudah, so that he gaue them one heart to doe the commandement of the King, and of the rulers, according to the worde of the Lord.
Mkono wa Mungu pia ukaja juu ya Yuda, kuwapa moyo mmmoja, ili kulikubali agizo la mfalme na viongozi kwa neno la Yahwe.
13 And there assembled to Ierusalem much people, to keepe the feast of ye vnleauened bread in the second moneth, a very great assemblie.
Watu wengi, kusanyiko kubwa, likakusanyika Yerusalemu kusherehekea Sikukuu ya Mikate Isiyochacha katika mwezi wa pili.
14 And they arose, and tooke away the altars that were in Ierusalem: and all those for incense tooke they away, and cast them into the brooke Kidron.
Waliinuka na kuchukua madhabahu zizilizokuwa Yerusalemu, madhabahu zote kwa ajili ya sadaka za kufukiza; wakazirusha katika kijito Kidroni.
15 Afterwarde they slewe the Passeouer the fourteenth day of the seconde moneth: and the Priestes and Leuites were ashamed, and sanctified themselues, and brought the burnt offrings into the house of the Lord.
Kisha wakamuua mwanakondoo wa Paska katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Makuhani na Walawi wakaona aibu, kwa hiyo wakajitakasa wenyewe na kuleta sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya Yahwe.
16 And they stoode in their place after their maner, according to the Lawe of Moses the man of God: and the Priestes sprinkled the blood, receiued of the handes of the Leuites.
Wakasimama katika sehemu zao katika makaundi yao, wakifuata maelekezo yaliyotolewa na sheria ya Musa, mtu wa Mungu. Makuhani wakainyunyiza damu waliyoipokea kutoka kwenye mikono ya Walawi.
17 Because there were many in the Congregation that were not sanctified, therefore the Leuites had the charge of the killing of ye Passeouer for all that were not cleane, to sanctifie it to the Lord.
Kwa maana walikuwepo wengi katika kusanyikao amaabao hawakuwa wamejitakasa wenyewe. Kwa hiyo Makuhani wakamchinja mwanakondoo wa Pasaka kwa ajili ya kila mmoja ambaye hakuwa amejisafisha na hakuweza kuzitakasa sadaka zake kwa Yahwe.
18 For a multitude of the people, euen a multitude of Ephraim, and Manasseh, Issachar and Zebulun had not cleansed themselues, yet did eate the Passeouer, but not as it was written: wherefore Hezekiah prayed for them, saying, The good Lord be mercifull toward him,
Kwa kuwa wingi wa watu, wengi wao kutoka Efraimu na Manase, Asakari na Zabuloni, hawakuwa wamejitakasa wenyewe, bado waliula mlo wa Paska, kinyume na maelekezo yaliyoandikwa. Kwa kuwa Hezekia alikuwa amewaombea, akisema, “Mungu Yahwe amsamehe kila mmoja
19 That prepareth his whole heart to seeke the Lord God, the God of his fathers, though he be not cleansed, according to the purification of the Sanctuarie.
ambaye anaulekeza moyo wake kumtafuta Mungu, Yahwe, Mungu wa babu zake, hata kama hajasafiswa kwa utakaso wa viwango vya patakatifu.”
20 And the Lord heard Hezekiah, and healed the people.
Kwa hiyo Yahwe akamsikiliza Hezekia na akawaponya watu.
21 And the children of Israel that were present at Ierusalem, kept the feast of the vnleauened bread seuen dayes with great ioye, and the Leuites, and the Priestes praysed the Lord, day by day, singing with loude instruments vnto the Lord.
Watu wa Israeli waliokuwepo Yerusalemu wakaitunza Sikukuu ya Mikaate Isiyochachwa na furaha kubwa kwa siku saba. Walawi na makuhani wakamsifu Yahwe siku baada ya siku, wakiimwimbia Yahwe kwa vyombo vya sauti kuu.
22 And Hezekiah spake comfortably vnto all the Leuites that had good knowledge to sing vnto the Lord: and they did eate in that feast seuen dayes, and offred peace offrings, and praysed the Lord God of their fathers.
Hezekia akazungumza kwa kuwatia moyo Walawi wote walioilewa ibada ya Yahwe, Kwa hiyo wakala kwa kipindi cha siku saba, wakitoa sadaka za amani, na kufanya toba kwa Yahwe, Mungu wa babu zao.
23 And the whole assembly tooke counsel to keepe it other seuen dayes. So they kept it seuen dayes with ioy.
Kusanyiko lote kisha likaamua kusherehekea kwa siku zingine saba, na wakafanya hivyo kwa furaha.
24 For Hezekiah King of Iudah had giuen to the Congregation a thousande bullockes, and seuen thousand sheepe. And the princes had giuen to the Congregation a thousand bullocks, and ten thousand sheepe: and many Priests were sanctified.
Kwa kuwa Hezekia mfalme wa Yuda aliwapa kusanyiko ng'ombe dume elf moja, na kondoo elfu saba kama sadaka; na viongozi wakawapa kusanyiko ng'ombe dume elfu moja na kondoo na mbuzi elfu kumi. Idadi kubwa ya makuhani wakajitakasa wenyewe.
25 And all the Congregation of Iudah reioyced with the Priestes and the Leuites, and all the Congregation that came out of Israel, and the strangers that came out of the land of Israel, and that dwelt in Iudah.
Kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi na watu wote walikuja pamoja kutoka nchi ya Israeli na wale walioishi Yuda—wote wakafurahia.
26 So there was great ioye in Ierusalem: for since the time of Salomon the sonne of Dauid King of Israel there was not the like thing in Ierusalem.
Hivyo kulikuwa na furaha kuu katika Yerusalemu, kwa kuwa tangu wakati wa Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli, hapakuwa na kitu kama hicho katika Yerusalemu.
27 Then the Priests and the Leuites arose, and blessed the people, and their voyce was heard, and their prayer came vp vnto heauen, to his holy habitation.
Kisha makuhani, Walawi, wakainuka na kuwabariki watu. Sauti zao zilisikika na maombi yao yakaenda juu mbinguni, sehemu takatifu ambapo Mungu anaishi.

< 2 Chronicles 30 >