< 2 Chronicles 27 >

1 Iotham was fiue and twentie yere olde when he began to reigne, and reigned sixteene yeere in Ierusalem, and his mothers name was Ierushah the daughter of Zadok.
Yothamu alikuwa na umri wa mika ishirini na mitano alipoanza kutawala; alitawala miaka kumi na sita katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Yerusha; alikuwa binti Sadoki.
2 And hee did vprightly in the sight of the Lord according to all that his father Vzziah did, saue that hee entred not into the Temple of the Lord, and the people did yet corrupt their wayes.
Akafanya yaliyomema katika macho ya Yawe, akiufuta mfano wa baba yake, Uzia, katika mabo yote. Pia alijiepusha kuingia katika hekalu la Yahwe. Lakini watu bado walikuwa wanaenda katika njia za uovu.
3 He buylt the hie gate of the house of the Lord, and he buylt very much on the wall of the castle.
Akalijenga tena lango la juu la nyumba ya Yahwe, na juu ya kilima cha Ofeli akajenga sana.
4 Moreouer hee buylt cities in the mountaines of Iudah, and in the forests he buylt palaces and towres.
Vilevile alijenga miji katika kilima cha Yuda, na katika mistu alijenga ngome na minara.
5 And he fought with the King of the children of Ammon, and preuailed against them. And the children of Ammon gaue him the same yere an hundreth talents of siluer, and ten thousande measures of wheate, and ten thousand of barley: this did the children of Ammon giue him both in the second yeere and the third.
Pia alipigana na mfalme wa watu wa Amoni na akawashinda. Katika mwaka huo huo, watu wa Amoni walimpa talanta mia moja za fedha, kori elfu kumi za ngano, kori elfu kumi za shayiri. Watu wa Amoni wakampa hivyo hivyo katika mwaka wa pili na wa tatu.
6 So Iotham became mightie because hee directed his way before the Lord his God.
Kwa hiyo Yothamu akawa na nguvu sana kwa sababu alitembea imara mbele za Yahwe Mungu wake.
7 Concerning the rest of the acts of Iotham, and all his warres and his wayes, loe, they are written in the booke of the Kings of Israel, and Iudah.
Kwa mambo mengine kuhusu Yothamu, vita vyake vyote, na njia zake zote, ona, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
8 He was fiue and twentie yeere olde when he began to reigne, and reigned sixteene yeere in Ierusalem.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; alitawala kwa miaka kumi na sita kataika Yerusalemu.
9 And Iotham slept with his fathers, and they buryed him in the citie of Dauid: and Ahaz his sonne reigned in his stead.
Yothamu akalala pamoja na babu zake, na wakamzika katika mji wa Daudi. Ahazi, mwanaye, akawa mfalme katika nafasi yake.

< 2 Chronicles 27 >