< 2 Chronicles 15 >

1 Then the Spirite of God came vpon Azariah the sonne of Obed.
Roho ya Mungu ikaja juu ya Azaria mwana wa Odedi.
2 And he went out to meete Asa, and said vnto him, O Asa, and all Iudah, and Beniamin, heare ye me. The Lord is with you, while ye be with him: and if ye seeke him, he wil be founde of you, but if ye forsake him, he will forsake you.
Akaenda nje kukutana na Asa na akamwambia, “Nisikilize, Asa, na Yuda wote na Benyamini: Yahwe yuko pamoja nanyi, pale mnapokuwa naye. Kama mtamtafuta, mtampata; lakini kama mtamsahau, atawasahau ninyi.
3 Nowe for a long season Israel hath bene without the true God, and without Priest to teach and without Lawe.
Sasa kwa muda mrefu, Israeli hawakuwa na Mungu wa kweli, bila kuhani wa kufundisha, na bila sheria.
4 But whosoeuer returned in his affliction to the Lord God of Israel, and sought him, he was founde of them.
Lakini katika dhiki yao wakamrudia Yahwe, Mungu wa Israeli, na wakamtafuta, wakamta.
5 And in that time there was no peace to him, that did goe out and goe in: but great troubles were to all the inhabitants of the earth.
Katika nyakati hizo hapakuwa na amani kwake aliyesafiri kwend mbali, wala kwake aliyesafiri kuja hapa; badala yake shsida kubwa zilikuwa juu ya wenyeji wote wa wanchi.
6 For nation was destroyed of nation, and citie of citie: for God troubled them with all aduersitie.
Waligawanyika vikundi vikundi, taifa dhidi ya taifa, na mji dhidi ya mji, kwa maana Mungu aliwapa shsida za kila aina ya kila mateso.
7 Be ye strong therefore, and let not your handes be weake: for your worke shall haue a rewarde.
Lakini muwe hodari, na msiuache mkono wenu kuwa dhaifu, kwa maana kazi yen itapewa thawabu.”
8 And when Asa heard these wordes, and the prophesie of Obed the Prophet, he was encouraged, and tooke away the abominations out of all the lande of Iudah, and Beniamin, and out of the cities which he had taken of mount Ephraim, and he renued the altar of the Lord, that was before the porche of the Lord.
Asa aliposikia maneno haya, unabii wa odedi nabii, akajipa ujasiri na kuviondosha mbali vitu vya kuchukiza kutoka nchi yote ya Yuda na Benyamini, na kutoka miji yote aliyokuwa ameiteka kuanzia kilima cha nchi ya Efraimu, na akaijenga tena madhabahu ya Yahwe, ambayo ilikuwa mbele ya ukumbi wa nyumba ya Yahwe.
9 And he gathered all Iudah and Beniamin, and the strangers with them out of Ephraim, and Manasseh, and out of Simeon: for there fell many to him out of Israel, when they sawe that the Lord his God was with him.
Akawakusanya Yuda wote na Benyamini, na wae waliokaa pamoja nao—watu wa kutoka Efraimu na Manase, na kutoka Simeoni. Kwa maana walikuja kwake katika hesabu kubwa kutoka Israeli, walipoona kwamba Yahwe Mungu wake alikuwa pamoja naye.
10 So they assembled to Ierusalem in the third moneth, in the fifteenth yere of the reigne of Asa.
Kwa hiyo wakakusanyika katika Yerusalemu katika mwezzi wa tatu, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
11 And they offred vnto the Lord the same time of the spoyle, which they had brought, euen seuen hundreth bullockes, and seuen thousande sheepe.
Katika siku hiyo walimtolea Yahwe dhabihu baadhi ya nyara ambazo walikuwa wameleta; ng'mbe wa kulima mia saba na kondoo na mbuzi elfu saba.
12 And they made a couenant to seeke the Lord God of their fathers, with all their heart, and with all their soule.
Wakaingia kataika agano kwa ajili ya kumtafuta Yahwe, Mungu wa babau zao, kwa moyo wao wote na roho yao yote.
13 And whosoeuer will not seeke the Lord God of Israel, shalbe slaine, whether he were small or great, man or woman.
Wakakubaliana kwamba yeyote atakepuuzia kumtafuta Yahwe, Mungu wa Israeli, atapaswa kuuawa, iwe mdogo ama mkubwa, iwe mwanaume ama mwanamke.
14 And they sware vnto the Lord with a loude voyce, and with shouting and with trumpets, and with cornets.
Wakaapa kwa Yahwe kwa sauti kubwa, kwa kelele, na kwa sauti za tarumbeta na baragumu.
15 And all Iudah reioyced at the othe: for they had sworne vnto the Lord with all their heart, and sought him with a whole desire, and he was founde of them. And the Lord gaue them rest rounde about.
Yuda wote wakakifurahia kile kiaapo. kwa maana walikuwa wameapa kwa moyo wao wote, na walimtafuta Mungu kwa nia yao yote, na walimuona. Yahwe akawapa amani pande zote.
16 And King Asa deposed Maachah his mother from her regencie, because she had made an idole in a groue: and Asa brake downe her idole, and stamped it, and burnt it at the brooke Kidron.
Pia akamwondoa Maaka, asiwe malikia, kwa sababu alikuwa amefanya sanamu ya kuchukiza ya Maashera. Asa akaivunja vunja sanamu ya kuchukiza, akaiweka kwenye mavumbi akaichoma moto huko kijitoni Kidroni.
17 But the hie places were not taken away out of Israel: yet the heart of Asa was perfit all his dayes.
Lakini sehemu za juu hazikuwa zimeondolewa nje ya Israeli. Vile vile, Moyo wa Asa ulijitoa kikamilifu siku zake zote.
18 Also he brought into the house of God the things that his father had dedicate, and that he had dedicate, siluer, and golde, and vessels.
Akaleta kwenye nyumba ya Mungu vitu vya baba yake na vitu vyake mwenyewe vilivyokuwa vya Yahwe: vitu vya fedha na dhahabu.
19 And there was no warre vnto the fiue and thirtieth yeere of the reigne of Asa.
Hapakuwa na vita zaidi hadi miaka thelathini na mitano ya utawala wa Asa.

< 2 Chronicles 15 >