< 2 Chronicles 10 >

1 Then Rehoboam went to Shechem: for to Sheche came all Israel to make him king.
Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
2 And when Ieroboam the sonne of Nebat heard it, (which was in Egypt, whither he had fled from the presence of Salomon the King) he returned out of Egypt.
Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
3 And they sent and called him: so came Ieroboam and all Israel, and communed with Rehoboam, saying,
Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
4 Thy father made our yoke grieuous: nowe therefore make thou the grieuous seruitude of thy father, and his sore yoke, that he put vpon vs, lighter, and we will serue thee.
“Baba yako aliweka nira nzito, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
5 And he sayde to them, Depart yet three dayes, then come againe vnto me. And the people departed.
Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
6 And King Rehoboam tooke counsel with the olde men that had stande before Salomon his father, while hee yet liued, saying, What counsell giue ye that I may answere this people?
Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
7 And they spake vnto him, saying, If thou be kinde to this people, and please them, and speake louing words to them, they will be thy seruants for euer.
Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
8 But hee left the counsel of the ancient men that they had giuen him, and tooke counsell of the yong men that were brought vp with him, and waited on him.
Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
9 And he sayd vnto them, What counsel giue ye, that we may answere this people, which haue spoken to mee, saying, Make the yoke which thy father did put vpon vs, lighter?
Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
10 And the yong men that were brought vp with him, spake vnto him, saying, Thus shalt thou answere the people that spake to thee, saying, Thy father made our yoke heauie, but make thou it lighter for vs: thus shalt thou say vnto them, My least part shalbe bigger then my fathers loines.
Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
11 Now whereas my father did burden you with a grieuous yoke, I will yet increase your yoke: my father hath chastised you with roddes, but I will correct you with scourges.
Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi; mimi nitawachapa kwa nge.’”
12 Then Ieroboam and all the people came to Rehoboam the third day, as the King had appointed saying, Come againe to me the third day.
Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
13 And the King answered them sharply: and King Rehoboam left the counsel of the ancient men,
Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
14 And spake to them after ye counsell of the yong men, saying, My father made your yoke grieuous, but I wil incease it: my father chastised you with rods, but I will correct you with scourges.
akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
15 So the king hearkened not vnto the people: for it was the ordinance of God that the Lord might performe his saying, which hee had spoken by Ahiiah the Shilonite to Ieroboam the sonne of Nebat.
Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Mungu ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
16 So when all Isarael sawe that the King would not heare them, the people answered the King, saying, What portion haue we in Dauid? for we haue none inheritance in the sonue of Ishai. O Israel, euery man to your tents: now see to thine owne house, Dauid. So all Israel departed to their tents.
Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli, angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
17 Howbeit Rehoboam reigned ouer the children of Israel, that dwelt in the cities of Iudah.
Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
18 Then King Rehoboam sent Hadoram that was ouer the tribute, and the children of Israel stoned him with stones, that he died: then King Rehoboam made speede to get him vp to his charet, to flee to Ierusalem.
Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoniramu aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
19 And Israel rebelled against the house of Dauid vnto this day.
Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.

< 2 Chronicles 10 >