< 1 Samuel 3 >

1 Nowe the childe Samuel ministred vnto the Lord before Eli: and the word of the Lord was precious in those dayes: for there was no manifest vision.
Yule mtoto Samweli alimtumikia BWANA chini ya uangalizi wa Eli. Neno la BWANA halikupatikana kwa wingi siku hizo; hapakuwa na maono ya mara kwa mara ya kinabii.
2 And at that time, as Eli lay in his place, his eyes began to waxe dimme that he could not see.
Wakati huo, nguvu ya macho ya Eli ilikuwa imefifia kiasi cha kutoweza kuona vizuri, na alikuwa amelala kitandani mwake.
3 And yet the light of God went out, Samuel slept in the temple of the Lord, where the Arke of God was.
Ile taa ya BWANA bado ilikuwa bado inawaka, na Samweli alikuwa amelala katika nyumba ya BWANA, palipokuwa na sanduku la Mungu.
4 Then the Lord called Samuel: and hee said, Here I am.
BWANA akamwita Samweli, naye akaitika, “Niko hapa”
5 And he ranne vnto Eli, and said, Here am I, for thou calledst me. But he said, I called thee not: goe againe and sleepe. And he went and slept.
Samweli alimwedea Eli na kusema, “Niko hapa, sababu uliniita.” Eli akasema, “Sikukuita; kalale tena.” Hivyo Samweli akarudi na kulala.
6 And the Lord called once againe, Samuel. And Samuel arose, and went to Eli, and said, I am here: for thou diddest call me. And he answered, I called thee not, my sonne: go againe and sleepe.
BWANA akamwita tena, “Samweli.” Saamweli aliamka tena na kwenda kwa Eli na kusema, Niko hapa, sababu umeniita.” Eli akajibu, “Sijakuita, mwanangu; kalale tu tena.” 8
7 Thus did Samuel, before hee knewe the Lord, and before the word of the Lord was reueiled vnto him.
Basi Samweli bado hakuwa na uzoefu kuhusu Bwana, wala hakuwahi kupata ujumbe wowote kutoka kwa BWANA ukifunuliwa kwake.
8 And the Lord called Samuel againe the thirde time: and he arose, and went to Eli, and said, I am here: for thou hast called me. Then Eli perceiued that the Lord had called the childe.
BWANA akamwita tena Samweli kwa mara ya tatu. Samweli alinyanyuka tena na kwenda kwa Eli na kusema, “Niko hapa, sababu uliniita,” Ndipo Eli alitambua kwamba BWANA alimwita kijana.
9 Therefore Eli saide vnto Samuel, Goe and sleepe: and if he call thee, then say, Speake Lord, for thy seruant heareth. So Samuel went, and slept in his place.
Kisha Eli aka, mwambia Samweli, “Nenda ukalale tena; ikiwa atakuita tena, sharti useme, 'Sema, BWANA, maana mtumwa wako anasikiliza.”' Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake tena.
10 And the Lord came, and stoode, and called as at other times, Samuel, Samuel. Then Samuel answered, Speake, for thy seruant heareth.
BWANA alikuja na kusimama; akaita vilevile kama vile mwanzoni, “Samweli, Samweli.” Ndipo Samweli akasema, “Nena, kwa sababu mtumwa wako anasikiliza.”
11 Then the Lord said to Samuel, Beholde, I wil doe a thing in Israel, whereof whosoeuer shall heare, his two eares shall tingle.
BWANA akasema na Samweli, “Tazama, Niko tayari kufanya jambo katika Israeli ambalo masikio ya kila mmoja akisikia atashtuka. -14
12 In that day I will raise vp against Eli all things which I haue spoken concerning his house: when I begin, I will also make an ende.
Siku hiyo nitatimiza kila kitu nilichokisema dhidi ya Eli kuhusu nyumba yake, kutoka mwanzo hadi mwisho.
13 And I haue tolde him that I will iudge his house for euer, for the iniquitie which hee knoweth, because his sonnes ranne into a slaunder, and he stayed them not.
Nimemwambia kwamba niko tayari kuhukumu nyumba yake mara moja kwa ile dhambi aliyoifahamu, kwa sababu watoto wake walijiletea laana juu yao wenyewe na hakuwazuia.
14 Nowe therefore I haue sworne vnto the house of Eli, that the wickednes of Elis house, shall not be purged with sacrifice nor offring for euer.
Hii ndiyo sababu nimeapa kwa nyumba ya Eli, kwamba dhambi za nyumba yake hazitasahehewa kwa dhabihu au kwa sadaka kamwe.” 16
15 Afterward Samuel slept vntil the morning, and opened the doores of the house of the Lord, and Samuel feared to shewe Eli the vision.
Samweli akalala hadi asubuhi; baadaye alifungua milango ya nyumba ya BWANA. Lakini Samweli aliogopa kumwambia Eli kuhusu maono hayo.
16 Then Eli called Samuel, and said, Samuel my sonne. And he answered, Here I am.
Kisha Eli akamwita Samweli na kusema, “Samweli, mwanangu.” Samweli akasema, “Niko hapa.” 18
17 Then he said, What is it, that the Lord said vnto thee? I pray thee, hide it not from mee. God doe so to thee, and more also, if thou hide any thing from me, of all that he said vnto thee.
Akamuuliza, “Ni neno gani alilokusemesha? Tafadhali usinifiche jambo hilo. Mungu akutendee hivyo na kukuzidishia, endapo utanificha kitu chochote kati ya yote ambayo amesema nawe.”
18 So Samuel tolde him euery whit, and hid nothing from him. Then hee said, It is the Lord: let him do what seemeth him good.
Samweli akamweleza kila kitu; hakumficha jambo lolote. Eli akasema, “Ni BWANA. Na afanye linaloonekana jema kwake.”
19 And Samuel grew, and the Lord was with him, and let none of his words fall to the ground.
Samweli akakua, na BWANA alikuwa pamoja naye na hakuacha kutimiza maneno yake ya unabii.
20 And all Israel from Dan to Beer-sheba knew that faithfull Samuel was the Lordes Prophet.
Israeli yote tokea Dani hadi Beersheba walijua kwamba Samweli aliteuliwa kuwa nabii wa BWANA.
21 And the Lord appeared againe in Shiloh: for the Lord reueiled himselfe to Samuel in Shiloh by his word.
Naye BWANA alionekana tena huko Shilo, maana alijifunua mwenyewe kwa Samweli huko Shilo kwa neno lake.

< 1 Samuel 3 >