< 1 Samuel 22 >

1 Dauid therefore departed thence, and saued him selfe in the caue of Adullam: and when his brethren and all his fathers house heard it, they went downe thither to him.
Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
2 And there gathered vnto him all men that were in trouble and all men that were in dette, and all those that were vexed in minde, and he was their prince, and there were with him about foure hundreth men.
Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
3 And Dauid went thence to Mizpeh in Moab, and said vnto the King of Moab, I pray thee, let my father and my mother come and abide with you, till I knowe what God wil doe for me.
Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
4 And he brought them before the King of Moab, and they dwelt with him all the while that Dauid was in the holde.
Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
5 And the Prophet Gad sayde vnto Dauid, Abide not in the holde, but depart and goe into the land of Iudah. Then Dauid departed and came into the forest of Hareth.
Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
6 And Saul heard that Dauid was discouered, and the men that were with him, and Saul remayned in Gibeah vnder a tree in Ramah, hauing his speare in his hande, and all his seruants stoode about him.
Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
7 And Saul said vnto his seruants that stood about him, Heare now, ye sonnes of Iemini, wil the sonne of Ishai giue euery one of you fields and vineyardes: will he make you all captaines ouer thousands, and captaines ouer hundreths:
Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
8 That all ye haue conspired against me, and there is none that tellerh mee that my sonne hath made a couenant with the sonne of Ishai? and there is none of you that is sory for me, or sheweth mee, that my sonne hath stirred vp my seruant to lie in wayte against me, as appeareth this day?
Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
9 Then answered Doeg the Edomite (who was appoynted ouer the seruants of Saul) and sayd, I saw the sonne of Ishai when he came to Nob, to Ahimelech the sonne of Ahitub,
Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
10 Who asked counsell of the Lord for him and gaue him vitailes, and he gaue him also the sword of Goliath the Philistim.
Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
11 Then the King sent to call Ahimelech the Priest the sonne of Ahitub, and all his fathers house, to wit, the Priests that were in Nob: and they came all to the King.
Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
12 And Saul said, Heare now thou sonne of Ahitub. And he answered, Here I am, my lord.
Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
13 Then Saul sayde vnto him, Why haue yee conspired against me, thou and the sonne of Ishai, in that thou hast giuen him vitaile, and a sworde, and hast asked counsell of God for him, that he should rise against me, and lye in wayte as appeareth this day?
Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
14 And Ahimelech answered the King, and sayde, Who is so faithfull among all thy seruants as Dauid, being also the Kings sonne in lawe, and goeth at thy commandement, and is honourable in thine house?
Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
15 Haue I this day first begun to aske counsell of God for him? be it farre from mee, let not the King impute any thing vnto his seruant, nor to all the house of my father: for thy seruant knew nothing of all this, lesse nor more.
Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
16 Then the King sayd, Thou shalt surely die, Ahimelech, thou, and all thy fathers house.
Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
17 And the King sayde vnto the sergeantes that stoode about him, Turne, and slay the Priestes of the Lord, because their hand also is with Dauid, and because they knewe when he fled, and shewed it not vnto mee. But the seruantes of the King would not moue their hands to fall vpon the Priests of the Lord.
Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
18 Then the King sayde to Doeg, Turne thou and fall vpon the Priests. And Doeg the Edomite turned, and ran vpon the Priestes, and slewe that same daye foure score and fiue persons that did weare a linen Ephod.
Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
19 Also Nob the citie of the Priestes smote he with the edge of the sword, both man and woman, both childe and suckling, both oxe and asse, and sheepe with the edge of the sword.
Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
20 But one of the sonnes of Ahimelech the sonne of Ahitub (whose name was Abiathar) escaped and fled after Dauid.
Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
21 And Abiathar shewed Dauid, that Saul had slayne the Lords Priestes.
Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
22 And Dauid sayd vnto Abiathar, I knewe it the same day, when Doeg the Edomite was there, that he would tell Saul. I am the cause of the death of all the persons of thy fathers house.
Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
23 Abide thou with me, and feare not: for he that seeketh my life, shall seeke thy life also: for with me thou shalt be in safegard.
Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”

< 1 Samuel 22 >