< 1 Samuel 17 >

1 Nowe the Philistims gathered their armies to battell, and came together to Shochoh, which is in Iudah, and pitched betweene Shochoh and Azekah, in the coast of Dammim.
Basi Wafilisti walikusanya majeshi yao kwa ajili ya vita. Walikusanyika huko Soko, iliyoko Yuda. Nao wakapiga kambi kati ya Soko na Aseka katika Efesdamimu.
2 And Saul, and the men of Israel assembled, and pitched in the valley of Elah, and put themselues in battell araie to meete the Philistims.
Sauli na watu wa Israeli alijikusanya na kuweka kambi katika bonde la Ela, na wakapanga vita kukutana na Wafilisti.
3 And the Philistims stoode on a mountaine on the one side, and Israel stoode on a mountaine on the other side: so a valley was betweene them.
Wafilisti walisimama juu ya mlima upande mmoja, na Iraeli nao walisimama juu ya mlima upande mwingine wakitenganishwa na bonde kati yao.
4 Then came a man betweene them both out of the tents of the Philistims, named Goliath of Gath: his height was sixe cubites and an hande breadth,
Mtu mmoja mwenye nguvu akatoka katika kambi ya Wafilisti, mtu huyo aliitwa Goliathi wa Gathi, kimo chake mikono sita na shubiri moja.
5 Aud had an helmet of brasse vpon his head, and a brigandine vpon him: and the weight of his brigandine was fiue thousand shekels of brasse.
Alikuwa na chepeo ya shaba kichwani mwake, na alivaa dirii ya chuma. Hiyo dirii ilikuwa na uzito wa shekeli elfu hamsini za shaba.
6 And he had bootes of brasse vpon his legs, and a shield of brasse vpon his shoulders.
Alikuwa na mabampa ya shaba kwenye miguu yake na mkuki wa shaba katikati ya mabega yake.
7 And the shaft of his speare was like a weauers beame: and his speare head weyed sixe hundreth shekels of yron: and one bearing a shielde went before him.
Ule mpini wa mkuki wake ulikuwa mkubwa, wenye kamba iliyo na kitanzi kwa ajili ya kuutupia kama kamba ya sindano ya mfumaji. Kichwa cha mkuki wake kilikuwa na uzito wa shekeli mia sita za chuma. Aliyembebea ngao alitembea mbele yake.
8 And he stoode, and cried against the hoste of Israel, and saide vnto them, Why are yee come to set your battell in aray? am not I a Philistim, and you seruaunts to Saul? chuse you a man for you, and let him come downe to me.
Alisimama akayapigia kelele majeshi ya Israeli, “Kwa nini mmekuja na mmejipanga kwa ajili ya vita? Mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli? Chagueni mtu kutoka kwenu ateremke na kuja kwangu.
9 If he be able to fight with me, and kill me, then wil we be your seruants: but if I ouercome him, and kill him, then shall yee be our seruants, and serue vs.
Kama anaweza kupigana nami na kuniua, hapo ndipo tutakuwa watumwa wenu. Lakini kama nitamshinda na kumuua, basi mtakuwa watumwa wetu na kututumikia.”
10 Also the Philistim saide, I defie the hoste of Israel this day: giue mee a man, that we may fight together.
Mfilisti huyo akasema tena, “Leo ninayapa changamoto majeshi ya Israeli. Mnipe mtu ili tuweze kupigana naye.”
11 When Saul and all Israel heard those wordes of the Philistim, they were discouraged, and greatly afraide.
Sauli na Israeli wote waliposikia alichosema Mfilisti huyo, walikata tamaa na kuogopa sana.
12 Nowe this Dauid was the sonne of an Ephrathite of Beth-lehem Iudah, named Ishai, which had eight sonnes: and this man was taken for an olde man in the daies of Saul.
Basi Daudi alikuwa mwana wa Mwefraimu wa Bethtelehemu ya Yuda, aliyeitwa Yese. Naye alikuwa na watoto wanane wa kiume. Yese alikuwa mtu mzee katika siku za Sauli, mwenye umri mkubwa kati ya watu.
13 And the three eldest sonnes of Ishai went and followed Saul to the battel: and the names of his three sonnes that went to battell, were Eliab the Eldest, and the next Abinadab, and the thirde Shammah.
Watoto watatu wakubwa wa Yese walimfuata Sauli vitani. Majina ya watoto wake watatu waliokwenda vitani yalikwa ni Eliabu mzaliwa wa kwanza, aliyemfuata Abinadabu, na watatu aliitwa Shama.
14 So Dauid was the least: and the three eldest went after Saul.
Daudi ndiye aliyekuwa mdogo kabisa. Hao wakubwa watatu walimfuata Sauli.
15 Dauid also went, but hee returned from Saul to feede his fathers sheepe in Beth-lehem.
Basi Daudi alikwenda na kurudi akipita kati ya majeshi ya Sauli akiwa na kondoo za baba yake huko Bethtelehemu, ili kuwachunga.
16 And the Philistim drew neere in the morning, and euening, and continued fourtie daies.
Kwa muda wa siku arobaini yule Mfilisti mwenye nguvu alikuwa akijitokeza asubuhi na jioni kwa ajili ya vita.
17 And Ishai said vnto Dauid his sone, Take nowe for thy brethren an Ephah of this parched corne, and these ten cakes, and runne to the hoste to thy brethren.
Kisha Yese akamwambia mwanawe Daudi, “Wapelekee kaka zako efa ya bisi na hii mikate kumi, na uzipeleke upesi kule kambini kwa ajili ya kaka zako.
18 Also carie these ten fresh cheeses vnto the captaine, and looke howe thy brethren fare, and receiue their pledge.
Pia peleka hizi jibini kumi kwa jemedari wa kikosi chao cha elfu. Ukawaangalie wako na hali gani kisha uniletee habari kuhusu wanavyoendelea vizuri.
19 (Then Saul and they, and all the men of Israel were in the valley of Elah, fighting with the Philistims)
Kaka zako wako pamoja na Sauli na watu wote wa Israeli katika bonde la Ela, wanapigana na Wafilisti.”
20 So Dauid rose vp earely in the morning, and left the sheepe with a keeper, and tooke and went as Ishai had commanded him, and came within the compasse of the hoste: and the hoste went out in araie, and shouted in the battell.
Daudi aliamka asubuhi na mapema na kuliacha kundi chini ya uangalizi wa mchungaji. Akachukua vile vitu na kuondoka, kama Yese alivyomwamuru. Akafika kambini wakati jeshi linaondoka kwenda uwanja wa vita wakipiga kelele za vita.
21 For Israel and the Philistims had put themselues in araie, armie against armie.
Nao Israeli na Wafilisti walijipanga kivita, jeshi dhidi ya jeshi.
22 And Dauid left the things, which hee bare, vnder the handes of the keeper of the cariage, and ranne into the hoste, and came, and asked his brethren howe they did.
Daudi aliviacha vitu vyake kwa mtunza mahitaji, akalikimbilia jeshi, na kuwasalimia kaka zake.
23 And as hee talked with them, beholde, the man that was betweene the two armies, came vp, (whose name was Goliath ye Philistim of Gath) out of the armie of the Philistims, and spake such woordes, and Dauid heard them.
Alipoongea nao, yule mtu mwenye nguvu, Mfilisti wa Gathi, jina lake Goliathi, akajitokeza kutoka majeshi ya Wafilisti, naye akasema maneno yaleyale kama hapo mwanzo. Naye Daudi akayasikia.
24 And all the men of Israel, when they sawe the man, ranne away from him, and were sore afraied.
Watu wote wa Israeli walipomwona Goliathi, walimkimbia na waliogopa sana.
25 For euery man of Israel saide, Sawe yee not this man that commeth vp? euen to reuile Israel is he come vp: and to him that killeth him, wil the king giue great riches, and will giue him his daughter, yea, and make his fathers house free in Israel.
Watu wa Israeli walisema, “Umemuona mtu huyu aliyejitokeza? Amekuja kuipa changamoto Israeli. Basi mfalme atampa mali nyingi mtu atakayemua, atamuozesha binti yake, na familia ya baba yake haitalipa kodi katika Israeli.”
26 Then Dauid spake to the men that stoode with him, and sayde, What shall be done to the man that killeth this Philistim, and taketh away the shame from Israel? for who is this vncircumcised Philistim, that he shoulde reuile the hoste of the liuing God?
Daudi akawauliza watu waliosimama karibu naye, “Atafanyiwa nini mtu ambaye atamuua Mfilisti huyu na kuiondolea Israeli fedheha? Ni nani Mfilisti huyu asiyetahiriwa ayatukanaye majeshi ya Mungu aliye hai?”
27 And the people answered him after this maner, saying, Thus shall it be done to the man that killeth him.
Ndipo watu wakarudia kile walichokuwa wamesema na kumwambia, “Ndivyo iitakavyofanyika kwa mtu atakayemuua.”
28 And Eliab his eldest brother heard when he spake vnto the men, and Eliab was verie angrie with Dauid, and sayde, Why camest thou downe hither? and with whome hast thou left those fewe sheepe in the wildernesse? I knowe thy pride and the malice of thine heart, that thou art come downe to see the battell.
Kaka yake mkubwa Eliabu, alisikia wakati akisema na watu. Hasira ya Eliabu ikawaka moto dhidi ya Daudi, naye akamuuliza, “Kwa nini umekuja hapa? Wale kondoo wachache umewaacha na nani huko nyikani? Nakijua kiburi chako, na utundu wa moyo wako; maana umekuja hapa ili uweze kuona mapigano.”
29 Then Dauid sayde, What haue I nowe done? Is there not a cause?
Naye Daudi akamjibu, “Nimefanya nini sasa? Mimi si nuliuliza swali tu?
30 And hee departed from him into the presence of another, and spake of the same maner, and the people answered him according to the former woordes.
Akamgeukia mtu mwingine na kumwacha huyo, na kusema vivyo hivyo. Nao watu wakajibu vilevile kama mwanzo.
31 And they that heard the wordes which Dauid spake, rehearsed them before Saul, which caused him to be brought.
Maneno aliyosema Daudi yaliposikika, askari waliyasema tena kwa Sauli, naye akawatuma kwa Daudi.
32 So Dauid saide to Saul, Let no mans heart faile him, because of him: thy seruant wil goe, and fight with this Philistim.
Kisha Daudi akamwambia Sauli, “Pasiwepo moyo wa mtu atakayezimia kwa sababu ya Mfilisti huyo; Mtumishi wako atakwenda kupigana na Mfilisti huyu.”
33 And Saul sayde to Dauid, Thou art not able to goe against this Philistim to fight with him: for thou art a boye, and he is a man of warre from his youth.
Sauli akamwambia Daudi, “Huwezi kumpinga Mfilisti ama kupigana naye; wewe ni kijana tu, na yeye amekuwa mtu wa vita tangu ujana wake.”
34 And Dauid answered vnto Saul, Thy seruant kept his fathers sheepe, and there came a lyon, and likewise a beare, and tooke a sheepe out of the flocke,
Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake. Mara simba au dubu alikuja akamchukua mwana kondoo kutoka kundini,
35 And I went out after him and smote him, and tooke it out of his mouth: and when he arose against me, I caught him by the beard, and smote him, and slue him.
Nilimfukuza na kumshambulia na kumpokonya kutoka kinywani mwake. Na aliponirukia, nilimshika ndevu zake, nilimpiga, na kumuua.
36 So thy seruaunt slue both the lyon, and the beare: therefore this vncircumcised Philistim shall be as one of them, seeing hee hath railed on the hoste of the liuing God.
Mtumishi wako amekwisha kmuua simba na dubu. N huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa wanyama hao, kwa kuwa ameyadharau majeshi ya Mungu aliye hai.”
37 Moreouer Dauid sayd, The Lord that deliuered me out of the pawe of the lyon, and out of the paw of the beare, he wil deliuer me out of the hand of this Philistim. Then Saul sayd vnto Dauid, Go, and the Lord be with thee.
Daudi akasema, “BWANA aliyeniokoa kutoka makucha ya simba na makucha ya dubu. Ataniokoa kutoka mkono wa Mfilisti huyu.” Kisha Sauli akamwambia Daudi, “Nenda, BWANA awe pamoja nawe.”
38 And Saul put his rayment vpon Dauid, and put an helmet of brasse vpon his head, and put a brigandine vpon him.
Sauli akamvika Daudi vazi lake la vita. Akamvika chepeo ya shaba kichwani pake, na akamvika koti la chuma.
39 Then girded Dauid his sword vpon his rayment, and began to go: for he neuer proued it: and Dauid sayde vnto Saul, I can not goe with these: for I am not accustomed. wherefore Dauid put them off him.
Daudi akaufunga upanga wake juu ya vazi la Sauli. Lakini hakuweza kutembea, kwa sababu hakupata mafunzo kwa mavazi hayo. Ndipo Daudi akamwambia Sauli, “Siwezi kwenda kupigana nikiwa na haya, maana sikupata mafunzo kwa haya.” Kwa hiyo Daudi akayavua.
40 Then tooke he his staffe in his hand, and chose him fiue smoothe stones out of a brooke, and put them in his shepheards bagge or skrippe, and his sling was in his hand, and he drewe neere to the Philistim.
Akachukua fimbo mkononi mwake na akachagua mawe matano laini kutoka katika kijito; akayaweka kwenye mfuko wake wa kichungaji. Kombeo lake lilikuwa mkononi akawa anamsogelea yule Mfilisti.
41 And the Philistim came and drew neere vnto Dauid, and the man that bare the shielde went before him.
Yule Mfilisti akaja na kumsogelea Daudi, mbeba ngao yake akiwa mbele yake.
42 Now when the Philistim looked about and saw Dauid, he disdeined him: for he was but yong, ruddie, and of a comely face.
Mfilisti alipotazama kila upande na kumuona Daudi, akamdharau, maana alikuwa kijana tu, mwekundu, na umbo la kupendeza.
43 And the Philistim sayde vnto Dauid, Am I a dog, that thou commest to me with staues? And the Philistim cursed Dauid by his gods.
Ndipo Mfilisti akamuuliza Daudi, “Je, mimi ni mbwa, hata ukanijia na fimbo? Naye Mfilisti kwa miungu yake akamlaani Daudi.
44 And the Philistim sayd to Dauid, Come to me, and I will giue thy flesh vnto the foules of the heauen, and to the beastes of the field.
Huyo Mfilisti akamwambia Daudi, “Njoo kwangu, na nyama yako nitawatupia ndege wa angani na wanyama wa mwituni.”
45 Then sayd Dauid to the Philistim, Thou commest to me with a sword, and with a speare, and with a shield, but I come to thee in the Name of the Lord of hostes, the God of the hoste of Israel, whom thou hast rayled vpon.
Daudi akamjibu Mfilisti, “Unaniijia kwa upanga, kwa mkuki na mkuki mdogo. Bali mimi nakuijia kwa jina la BWANA wa majeshi, Mungu wa Majeshi ya Israeli, uliyemdharau.
46 This day shall the Lord close thee in mine hand, and I shall smite thee, and take thine head from thee, and I wil giue the carkeises of the hoste of the Philistims this daye vnto the foules of the heauen, and to the beasts of the earth, that all the world may know that Israel hath a God,
Leo BWANA atanipa ushindi dhidi yako, na nitakuua na kukiondoa kichwa chako kwenye kiwiliwili. Leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni walioko duniani mizoga ya jeshi la Wafilisti, ili dunia yote ijue kwamba yupo Mungu katika Israeli,
47 And that all this assembly may know, that the Lord saueth not with sworde nor with speare (for the battel is the Lords) and he will giue you into our handes.
na kusanyiko hili lote lijue kwamba BWANA hatoi ushindi kwa upanga wala kwa mkuki. Kwa kuwa vita ni ya BWANA, na atawaweka katika mkono wetu.”
48 And when the Philistim arose to come and drawe neere vnto Dauid, Dauid hasted and ran to fight against the Philistim.
Mfilisti aliponyanyuka na kukaribia akutane na Daudi, ndipo Daudi akakimbia kwa haraka kuelekea jeshi la adui ili akutane naye.
49 And Dauid put his hande in his bagge, and tooke out a stone, and slang it, and smote the Philistim in his forehead, that the stone sticked in his forehead, and he fell groueling to the earth.
Daudi aliweka mkono wake mfukoni, akachukua jiwe kutoka humo, akalitupa kwa kombeo, na likampiga Mfilisti kwenye paji la uso, akaanguka chini kifudifudi.
50 So Dauid ouercame the Philistim with a sling and with a stone, and smote the Philistim, and slew him, when Dauid had no sword in his hand.
Daudi alimshinda Mfilisti kwa kombeo na kwa jiwe moja. Alimpiga huyo Mfilisti na kumuua. Mkononi mwa Daudi hakukuwa na upanga.
51 Then Dauid ranne, and stood vpon the Philistim, and tooke his sword and drew it out of his sheath, and slewe him, and cut off his head therewith. So whe the Philistims saw, that their champion was dead, they fled.
Ndipo Daudi akakimbia akasimama juu ya Mfilisti na kutwaa upanga wake, akauchomoa kutoka alani, akamuua, na kukata kichwa chake kwa upanga huo.
52 And the men of Israel and Iudah arose, and shouted, and followed after the Philistims, vntill they came to the valley, and vnto the gates of Ekron: and the Philistims fell downe wounded by the way of Shaaraim, euen to Gath and to Ekron.
Ndipo watu wa Israeli na wale wa Yuda wakaamka kwa kelele, na kuwafukuza Wafilisti kuvuka bonde na malango ya Ekroni. Na maiti za Wafilisti walilala katika njia iendayo Shaaraimu, na njia yote kuelekea Gathi na Ekroni.
53 And the children of Israel returned from pursuing the Philistims, and spoyled their tents.
Watu wa Israeli wakarejea kutoka kuwafukuza Wafilisti, na wakateka nyara kambi yao.
54 And Dauid tooke the head of ye Philistim, and brought it to Ierusalem, and put his armour in his tent.
Daudi akachukua kichwa cha Mfilisti na kukipeleka Yerusalemu, lakini akaliweka vazi la vita katika hema lake.
55 When Saul sawe Dauid go forth against the Philistim, he sayd vnto Abner the captaine of his hoste, Abner, whose sonne is this yong man? and Abner answered, As thy soule liueth, O King, I can not tell.
Sauli alipomuona Daudi akienda kukabiliana na yule Mfilisti, akamwambia Abneri, jemedari wa jeshi, “Abneri, kijana huyu ni mtoto wa nani? Abneri akasema, “Kama uishivyo, mfalme, mimi sijui.”
56 Then the King sayde, Enquire thou whose sonne this yong man is.
Naye mfalme akasema, “Waulize wanaoweza kufahamu, mvulana huyu ni kijana wa nani.”
57 And when Dauid was returned from the slaughter of the Philistim, then Abner tooke him, and brought him before Saul with the head of the Philistim in his hand.
Daudi aliporudi kutoka kumuua yule Mfilisti, Abneri alimchukuwa, na kumleta mbele ya Sauli akiwa na kichwa cha Mfilisti mkononi mwake.
58 And Saul sayde to him, Whose sonne art thou, thou yong man? And Dauid answered, I am the sonne of thy seruant Ishai the Bethlehemite.
Sauli akamuuliza, “Kijana, wewe ni mtoto wa nani? Na Daudi akamjibu, “Mimi ni mtoto wa mtumishi wako Yese Mbethlehemu.”

< 1 Samuel 17 >