< 1 Chronicles 19 >

1 After this also Nahash the King of the children of Ammon dyed, and his sonne reigned in his stead.
Ikajakuwa baadae kwamba Nahashi, mfalme wa watu wa Amoni, akafa, na mwanae akawa mfalme baada yake.
2 And Dauid said, I will shew kindnesse vnto Hanun the sonne of Nahash, because his father shewed kindnesse vnto me. And Dauid sent messengers to comfort him for his father. So the seruants of Dauid came into the lande of the children of Ammon to Hanun to comfort him.
Daudi akasema, “Nitaonyesha ukarimu kwa mwana wa Hanuni wa Nahashi, kwasababu baba yake alionyesha ukarimu kwangu.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kumfariji kuhusu baba yake. Watumishi wa Daudi wakaingia nchi ya Waamoni na kumfuata Hanuni, ilikumfariji.
3 And the princes of the children of Ammon said to Hanun, Thinkest thou that Dauid doeth honour thy father, that he hath sent comforters vnto thee? Are not his seruants come to thee to search, to seeke and to spie out the land?
Lakini viongozi wakamwambia Hanuni, “Unadhani Daudi anamheshimu baba yako sababu ametuma watu kukufaraji? Je watumishi wake hawajaja kutadhimini nchi iliwaipindue?
4 Wherefore Hanun tooke Dauids seruants, and shaued them, and cut off their garments by the halfe vnto the buttocks, and sent them away.
Hanuni akawakamata watumishi wa Daudi, akawanyoa, akakata mavazi ya nusu kwenye kiuno kushuka, na kuwarudisha.
5 And there went certaine and tolde Dauid concerning the men: and he sent to meete them (for the men were exceedingly ashamed) and the King saide, Tarie at Iericho, vntill your beardes be growen: then returne.
Walipo eleza haya kwa Daudi, alienda kukutana nao, kwa kuwa walifedheeka sana. Mfalme akasema, “Bakini Yeriko hadi ndevu zenu ziote tena, kisha mrudi.”
6 When the children of Ammon saw that they stanke in the sight of Dauid, then sent Hanun and the children of Ammon a thousande talents of siluer to hire them charets and horsemen out of Aram Naharaim and out of Aram Maachah, and out of Zobah.
Waamoni walipoona wamekuwa kikwazo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni walituma talanta elfu moja za fedha kukodisha magari ya farasi kwa Waaremei na wanaume wa farasi kutoka Naharaimu, Maka, na Zoba.
7 And they hired them two and thirty thousande charets, and the King of Maachah and his people, which came and pitched before Medeba: and the children of Ammon gathered themselues together from their cities, and came to the battell.
Waliwakodishia magari ya farasi elfu thelathini na mbili pamoja na mfalme wa Maka na watu wake, walio kuja na kueka kambi mbele ya Medeba. Waamoni walijikusanya pamoja kutoka miji yao, na wakaja kwa vita.
8 And when Dauid heard, he sent Ioab and all the hoste of the valiant men.
Daudi alipo sikia, alimtuma Yoabu na wanajeshi wake wote.
9 And the children of Ammon came out, and set their battell in aray at the gate of the citie. And the Kings that were come, were by them selues in the fielde.
Watu wa Amoni walikuja na kupanga mstari kwa ajili ya pambano katika lango la mji, wafalme waliokuja walikuwa peke yao katika shamba.
10 When Ioab saw that the front of the battel was against him before and behinde, then he chose out of all the choyse of Israel, and set him selfe in aray to meete the Aramites.
Yoabu alipoona mistari ya pambano imemzunguka mbele na nyuma, alichagua wapambanaji shupavu wa Israeli na kuwa panga dhidi ya Waaremi.
11 And the rest of the people he deliuered vnto the hande of Abishai his brother, and they put them selues in aray against the children of Ammon.
Wanajeshi wengine wote, aliwaeka chini ya Abishai kaka yake, akawapanga kwa mstari dhidi ya Amoni.
12 And he saide, If Aram be too strong for me, then thou shalt succour me: and if the children of Ammon preuaile against thee, then I wil succour thee.
Yoabu akasema, “Kama Waaremi wananguvu kunizidi, kisha wewe, Abishai, lazima uniokoe. Lakini kama jeshi la Waamoni lina nguvu kukuzidi, nitakuja kukuokoa.
13 Be strong, and let vs shewe our selues valiant for our people, and for the cities of our God, and let the Lord doe that which is good in his owne sight.
Kuwa thabiti, natujionyeshe kwa watu wetu kuwa ni wenye nguvu na kwa miji ya Mungu wetu, kwa kuwa Yahweh ata fanya lililo jema kwa kusudi lake.”
14 So Ioab and the people that was with him, came neere before the Aramites vnto the battel, and they fled before him.
Hivyo Yoabu na wanajeshi wasogea kwenye pambano dhidi ya Waaremi, walio lazimika kukimbia mbele ya jeshi la Waisraeli.
15 And when the children of Ammon sawe that the Aramites fled, they fled also before Abishai his brother, and entred into the citie: so Ioab came to Ierusalem.
Jeshi la Waamoni walipoona kuwa Waaremi wamekimbia, wao pia wakamkimbia kaka yake Yoabu Abishai na kurudi mjini. Kisha Yoabu akarudi kutoka kwa watu wa Amoni na kurudi Yerusalemu.
16 And when the Aramites sawe that they were discomfited before Israel, they sent messengers and caused the Aramites to come forth that were beyond the riuer: and Shophach the captaine of the hoste of Hadarezer went before them.
Waaremi walipoona kuwa wanashindwa na Waisraeli, wakatuma msaada nyuma ya Mto Frati, na Shofaki mkuu wajeshi la Hadadezeri.
17 And when it was shewed Dauid, he gathered all Israel, and went ouer Iorden, and came vnto them, and put him selfe in aray against them: And when Dauid had put him selfe in battel aray to meete the Aramites, they fought with him.
Daudi alipo ambiwa haya, akakusanya Israeli yote, akuvuka Yordani, na kuja juu yao. Alipanga jeshi kwa ajili ya pambano dhidi ya Waaremi, na wakapigana nao.
18 But the Aramites fled before Israel, and Dauid destroyed of the Aramites seuen thousand charets, and fourtie thousand footemen, and killed Shophach the captaine of the hoste.
Waaremi waliwakimbia Waisraeli, na Daudi akaua waendesha magari ya farasi ya Waaremi elfu saba na wanajeshi wa miguu elfu arobaini. Pia alimuua Shopaki, mkuu wa jeshi.
19 And when the seruants of Hadarezer sawe that they fell before Israel, they made peace with Dauid, and serued him. And the Aramites would no more succour the children of Ammon.
Wafalme wote walio kuwa watumishi wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, walifanya amani na Daudi na kumtumikia. Hivyo watu wa Aramu hawakuwa tayari kuwasaidia Waamoni.

< 1 Chronicles 19 >