< Luke 3 >

1 By now Tiberias had been Caesar for fifteen years. Pontius Pilate was governor of Judea. Herod was ruler of Galilee, his brother Philip was ruler of Iturea and Trachonitis, and Lysanius was ruler of Abiline.
Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 Annas and Caiphas were the current high priests. This was the time when the word of God came to John, Zechariah's son, who was living in the desert.
na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
3 He went throughout the whole Jordan region, announcing to everyone that they needed to be baptized to show they had repented and their sins had been forgiven.
Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
4 As Isaiah the prophet wrote: “A voice was heard crying out in the desert, ‘Prepare the way of the Lord: make his paths straight.
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
5 Every valley will be filled, and every mountain and hill will be leveled. Crooked ways will be straightened, and rough roads will be smoothed.
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
6 Every human being will see God's salvation.’”
Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
7 John addressed the crowds that came to him to be baptized. “You viper's brood! Who warned you to flee from the coming judgment?” he asked.
Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
8 “Demonstrate that you have truly repented. Don't try to justify yourselves by saying, ‘We're Abraham's descendants.’ Let me tell you, God can create children of Abraham from these stones.
Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
9 The ax is set to begin chopping at the base of the trees. Any tree that doesn't produce good fruit will be chopped down and thrown into the fire.”
Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
10 “So what should we do?” the crowds asked him.
Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
11 “If you have two coats, then share with someone who doesn't have one. If you have food, then share with those who don't,” he told them.
Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 Some tax collectors came to be baptized. “Teacher, what should we do?” they also asked.
Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
13 “Don't collect any more tax than you're meant to,” he replied.
Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
14 “What about us?” some soldiers asked. “What should we do?” “Don't demand money with threats of violence. Don't make accusations that are untrue. Be satisfied with your wages,” he replied.
Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
15 The people were waiting expectantly, and wondered whether John himself might be the Messiah.
Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
16 John replied and explained to everybody, “Yes, I am baptizing you in water. But the one who is coming is more important than me, and I'm not worthy to undo his sandals. He will baptize you with the Holy Spirit and with fire.
Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 His winnowing fork is in his hand and he's ready to separate the wheat from the chaff on his threshing floor. He'll gather the wheat into his barn, but he will burn up the chaff with fire that can't be extinguished.”
Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
18 John gave many warnings like this as he announced the good news to the people.
Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
19 But when John reprimanded Herod the ruler for marrying Herodias, Herod's brother's wife, and for all the evil things he'd done,
Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
20 Herod added to his crimes by having John thrown into jail.
Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
21 Now it happened that after everyone had been baptized, Jesus was baptized as well. As he was praying, heaven was opened,
Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
22 and the Holy Spirit descended upon him, taking the form of a dove. A voice came from heaven, saying, “You are my son, the one I love. I am truly pleased with you.”
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
23 Jesus was around thirty when he began his public ministry. People presumed he was the son of Joseph. Joseph was the son of Heli,
Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
24 the son of Matthat, the son of Levi, the son of Melchi, the son of Jannai, the son of Joseph,
mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
25 the son of Mattathias, the son of Amos, the son of Nahum, the son of Esli, the son of Naggai,
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
26 the son of Maath, the son of Mattathias, the son of Semein, the son of Josech, the son of Joda,
mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
27 the son of Joanan, the son of Rhesa, the son of Zerubbabel, the son of Shealtiel, the son of Neri,
mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 the son of Melchi, the son of Addi, the son of Cosam, the son of Elmadam, the son of Er,
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 the son of Joshua, the son of Eliezer, the son of Jorim, the son of Matthat, the son of Levi,
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
30 the son of Simeon, the son of Judah, the son of Joseph, the son of Jonam, the son of Eliakim,
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
31 the son of Melea, the son of Menna, the son of Mattatha, the son of Nathan, the son of David,
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 the son of Jesse, the son of Obed, the son of Boaz, the son of Salmon, the son of Nahshon,
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 the son of Amminadab, the son of Arni, the son of Hezron, the son of Perez, the son of Judah,
mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
34 the son of Jacob, the son of Isaac, the son of Abraham, the son of Terah, the son of Nahor,
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 the son of Serug, the son of Reu, the son of Peleg, the son of Eber, the son of Shelah,
mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 the son of Cainan, the son of Arphaxad, the son of Shem, the son of Noah, the son of Lamech,
mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
37 the son of Methuselah, the son of Enoch, the son of Jared, the son of Mahalaleel, the son of Cainan,
mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
38 the son of Enosh, the son of Seth, the son of Adam, the son of God.
mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.

< Luke 3 >