< Luke 21 >

1 Looking around, Jesus watched rich people putting their gifts into the collection box.
Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
2 He also saw a very poor widow put in two small coins.
Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
3 “I tell you the truth,” he said, “this poor widow has put in more than all the rest together.
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
4 All of them gave from their wealth what they had, but she gave from her poverty all she had to live on.”
Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
5 Some of those there were talking about the Temple, its fine stonework and the beautiful gifts that had been donated. But Jesus said,
Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
6 “Regarding these things you're looking at… The time is coming when not one stone will be left on another; everything will be destroyed!”
“Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
7 “Teacher, when will this happen?” they asked him. “What will be the sign that these things are about to happen?”
Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
8 “Make sure you're not deceived,” Jesus warned them. “Many people will come claiming to be me, saying, ‘Here I am!’ and, ‘The time has come!’ but don't follow them.
Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
9 When you hear of wars and revolutions, don't be frightened, because these things have to happen first, but the end won't come immediately.
Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
10 Nation will fight nation, and kingdom will fight kingdom,” he told them.
Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
11 “There will be severe earthquakes, famines, and epidemic diseases in many lands, and extraordinary signs in the sky that are terrifying.
Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
12 But before all this, they will seize you and persecute you. They will drag you before synagogues and throw you into prison, and put you on trial before kings and governors on account of me.
“Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
13 But this will provide you an opportunity to speak on my behalf before them.
Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
14 So make up your mind beforehand not to worry about how to defend yourselves,
Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
15 for I will give you words of wisdom that your enemies won't be able to dispute or contradict.
Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
16 You will be betrayed even by your parents, brothers, relatives, and friends, and they will kill some of you.
Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
17 Everyone will hate you because of me.
Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
18 But not a single hair of your head will be lost.
Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
19 By standing firm you will gain your lives.
Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
20 However, when you see Jerusalem surrounded by armies, then you know that its destruction is near.
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
21 Those who are in Judea should run away to the mountains, and those who are in Jerusalem should leave, and those who are the countryside shouldn't enter the city.
Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
22 For these are days of punishment, fulfilling all that's written.
Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
23 How hard it will be for those who are pregnant or nursing babies at that time! For terrible trouble is coming on the land and punishment against this people.
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
24 They will be killed by the sword and taken away as prisoners to all the nations. Jerusalem will be trodden down by the foreign nations until their time is fulfilled.
Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
25 There will be signs in the sun, moon, and stars, and on the earth the nations will be in distress, confused by the sea's rolling and crashing.
“Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
26 People will be faint from fear, terrified about what is happening to the world, for the powers of heaven will be shaken.
Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
27 Then they'll see the Son of man coming in a cloud with power and great glory.
Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
28 But when these things happen, stand up and look up, because you will soon be saved.”
Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
29 Then he told them this story as an illustration. “Look at the fig tree, or any other kind of tree.
Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
30 When you see new leaves appear, you don't need to be told that summer is near.
Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
31 In the same way, when you see these things happening, you don't need to be told that God's kingdom is near.
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 I tell you the truth, this generation won't come to an end before all this happens.
“Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
33 Heaven and earth will come to an end, but my word will not.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
34 Watch out that you don't become distracted by partying or getting drunk or by the worries of this life, so that this day catches you by surprise.
“Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
35 For this day will come upon everyone who lives on the face of the earth.
Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
36 Always keep watch and pray, so that you may be able to escape all that will happen and stand before the Son of man.”
Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
37 Every day Jesus taught in the Temple, and every evening he went and stayed on the Mount of Olives.
Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
38 All the people came early in the morning to listen to him in the Temple.
Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.

< Luke 21 >