< Luke 19 >

1 He entered and started passing through Jericho.
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 A man named Zacchaeus was there—he was a chief tax collector, and he was wealthy!
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 He was trying to see who Jesus was, but could not because of the crowd, because he was short.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 And running on ahead he climbed up into a sycamore tree, in order to see Him, since He was about to pass by there.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 And when Jesus came to the place, He looked up and saw him, and said to him, “Zacchaeus, come down quickly, because today I must stay at your house.”
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 So he came down quickly, and received Him joyfully.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 But when they saw it, they all started complaining, saying, “He has entered to lodge with a sinful man!”
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 Then Zacchaeus stood and said to the Lord, “Indeed, Lord, I herewith give half of my goods to the poor, and if I have extorted anything from anyone, I restore fourfold.”
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 So Jesus said about him, “Today salvation has happened in this house, in that he also is a son of Abraham;
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 because the Son of the Man has come to seek and to save that which was lost.”
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 Now as they heard these things, He continued with a parable, because He was near Jerusalem and they were supposing that the Kingdom of God was on the verge of being revealed.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 So He said: “A certain nobleman went to a distant country to receive for himself a kingdom and return.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 He called ten of his slaves, gave them ten ‘minas’, and said to them, ‘Conduct business until I come.’
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 But his citizens hated him and sent a delegation after him, saying, ‘We do not want this man to reign over us.’
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 It happened that he did receive the kingdom, and upon returning he ordered that those slaves to whom he had given the money be called to him, to know who had gained what by trading.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 So the first one came and said, ‘Master, your mina earned ten minas!’
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 He said to him: ‘Super, you good slave! Because you were faithful in a very little, have authority over ten cities!’
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 And the second one came and said, ‘Master, your mina made five minas.’
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 Likewise he said to him, ‘You also be over five cities.’
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 Then a different one came, saying: ‘Master, here is your mina, that I kept laid away in a piece of cloth
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 —I feared you because you are a hard man, removing what you did not place, and reaping what you did not sow.’
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 So he said to him: ‘I will judge you out of your own mouth, you wicked slave! You knew that I am a hard man, removing what I did not place, and reaping what I did not sow.
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 Why then didn't you put my money on deposit, and upon coming I would have collected it with interest?’
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 And to those standing by he said, ‘Take the mina from him and give it to him who has the ten minas.’
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 (They even said to him, ‘Master, he already has ten minas!’)
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 ‘Indeed I tell you, to everyone who has, more will be given; but from him who does not have, even what he has will be taken from him.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 But as for those enemies of mine who did not want me to reign over them, bring them here and slaughter them in front of me!’”
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 Having said these things, He went on ahead, going up to Jerusalem.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 When He drew near to Bethphage and Bethany, at the mountain called ‘of Olives’, it happened like this: He sent two of His disciples,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 saying: “Go to the village opposite you, where as you enter you will find a colt tied, on which no man ever yet sat. Untie and bring it.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 And if anyone asks you, ‘Why are you untying it?’ just say this to him: ‘The Lord needs it.’”
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 So those who were sent went and found it just like He told them.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 As they were untying the colt, its owners said to them, “Why are you untying the colt?”
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 So they said, “The Lord needs it.”
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 Then they brought it to Jesus; and throwing their own clothes on the colt, they placed Jesus on it.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 And as He went along people were spreading their clothes on the road.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 Then, as He was approaching the descent of the Mount of Olives, the whole multitude of the disciples began to rejoice and praise God with a loud voice for all the mighty works they had seen,
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 saying: “Blessed is the King who comes in the name of the Lord! Peace in heaven and glory in the highest!”
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 Some of the Pharisees said to Him from the crowd, “Teacher, rebuke your disciples!”
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 In answer He said to them, “I tell you that if these should keep silent, the very stones would cry out!”
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 Now as He approached, observing the city He wept over it,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 saying: “If you, yes you, especially in this your day, had known the things pertaining to your peace! But now they are hidden from your eyes.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 Yes, the days will come upon you when your enemies will build an embankment around you; indeed they will surround you and hem you in on every side.
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 And they will raze you, and your children within you, to the ground—they will not leave in you one stone upon another—all because you did not recognize the time of your visitation.”
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 And upon entering the temple He began to drive out those who were selling and buying in it,
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 saying to them, “It is written: ‘My house is a house of prayer,’ but you have made it a ‘den of robbers’!”
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 And He was teaching daily in the temple; but the chief priests and the scribes, as also the leaders of the people, were trying to destroy Him,
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 but could not figure out how to do it, because all the people were hanging on His words.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luke 19 >