< Zechariah 10 >

1 Ask ye of the Lord rain in the latter season, and the Lord will make snows, and will give them showers of rain, to every one grass in the field.
Mwombeni Bwana mvua wakati wa vuli; ndiye Bwana atengenezaye mawingu ya tufani. Huwapa watu manyunyu ya mvua, pia mimea ya shambani kwa ajili ya kila mtu.
2 For the idols have spoken what was unprofitable, and the diviners have seen a lie, and the dreamers have spoken vanity: they comforted in vain: therefore they were led away as a dock: they shall be afflicted, because they have no shepherd.
Sanamu huzungumza udanganyifu, waaguzi huona maono ya uongo; husimulia ndoto ambazo si za kweli, wanatoa faraja batili. Kwa hiyo watu wanatangatanga kama kondoo walioonewa kwa kukosa mchungaji.
3 My wrath is kindled against the shepherds, and I will visit upon the buck goats: for the Lord of hosts hath visited his flock, the house of Juda, and hath made them as the horse of his glory in the battle.
“Hasira yangu inawaka dhidi ya wachungaji, nami nitawaadhibu viongozi; kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote atalichunga kundi lake, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi mwenye kiburi akiwa vitani.
4 Out of him shall come forth the corner, out of him the pin, out of him the bow of battle, out of him every exacter together.
Kutoka Yuda litatokea Jiwe la pembeni, kutoka kwake vitatoka vigingi vya hema, kutoka kwake utatoka upinde wa vita, kutoka kwake atatoka kila mtawala.
5 And they shall be as mighty men, treading under foot the mire of the ways in battle: and they shall fight, because the Lord is with them, and the riders of horses shall be confounded.
Kwa pamoja watakuwa kama mashujaa wanaokanyaga barabara za matope wakati wa vita. Kwa sababu Bwana yu pamoja nao, watapigana na kuwashinda wapanda farasi.
6 And I will strengthen the house of Juda, and save the house of Joseph: and I will bring them back again, because I will have mercy on them: and they shall be as they were when I had cast them off, for I am the Lord their God, and will hear them.
“Nitaiimarisha nyumba ya Yuda na kuiokoa nyumba ya Yosefu. Nitawarejesha kwa sababu nina huruma juu yao. Watakuwa kama watu ambao sijawahi kuwakataa kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wao, nami nitawajibu.
7 And they shall be as the valiant men of Ephraim, and their heart shall rejoice as through wine: and their children shall see, and shall rejoice, and their heart shall be joyful in the Lord.
Waefraimu watakuwa kama mashujaa, mioyo yao itafurahi kana kwamba ni kwa divai. Watoto wao wataona na kufurahi, mioyo yao itashangilia katika Bwana.
8 I will whistle for them, and I will gather them together, because I have redeemed them: and I will multiply them as they were multiplied before.
Nitawaashiria na kuwakusanya ndani. Hakika nitawakomboa, nao watakuwa wengi kama walivyokuwa mwanzoni.
9 And I will sow them among peoples: and from afar they shall remember me: and they shall live with their children, and shall return.
Ijapokuwa niliwatawanya miongoni mwa mataifa, hata hivyo wakiwa katika nchi za mbali watanikumbuka mimi. Wao na watoto wao watanusurika katika hatari nao watarudi.
10 And I will bring them back out of the land of Egypt, and will gather them from among the Assyrians: and will bring them to the land of Galaad, and Libanus, and place shall not be found for them.
Nitawarudisha kutoka Misri na kuwakusanya toka Ashuru. Nitawaleta katika nchi ya Gileadi na Lebanoni, na hapo hapatakuwa na nafasi ya kuwatosha.
11 And he shall pass over the strait of the sea, and shall strike the waves in the sea, and all the depths of the river shall be confounded, and the pride of Assyria shall be humbled, and the sceptre of Egypt shall depart.
Watapita katika bahari ya mateso; bahari iliyochafuka itatulizwa na vilindi vyote vya Mto Naili vitakauka. Kiburi cha Ashuru kitashushwa, nayo fimbo ya utawala ya Misri itatoweka.
12 I will strengthen them in the Lord, and they shall walk in his name, saith the Lord.
Nitawaimarisha katika Bwana, na katika jina lake watatembea,” asema Bwana.

< Zechariah 10 >