< Song of Solomon 3 >

1 In my bed by night I sought him whom my soul loveth: I sought him, and found him not.
Usiku kucha kwenye kitanda changu nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye; nilimtafuta, lakini sikumpata.
2 I will rise, and will go about the city: in the streets and the broad ways I will seek him whom my soul loveth: I sought him, and I found him not.
Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini, katika barabara zake na viwanja; nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye. Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.
3 The watchmen who keep the city, found me: Have you seen him, whom my soul loveth?
Walinzi walinikuta walipokuwa wakizunguka mji. Nikawauliza, “Je, mmemwona yule moyo wangu umpendaye?”
4 When I had a little passed by them, I found him whom my soul loveth: I held him: and I will not let him go, till I bring him into my mother’s house, and into the chamber of her that bore me.
Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita nilimpata yule moyo wangu umpendaye. Nilimshika na sikumwachia aende mpaka nilipomleta katika nyumba ya mama yangu, katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.
5 I adjure you, O daughters of Jerusalem, by the roes and the harts of the fields, that you stir not up, nor awake my beloved, till she please.
Binti za Yerusalemu, ninawaagiza kwa paa na kwa ayala wa shambani: Msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe.
6 Who is she that goeth up by the desert, as a pillar of smoke of aromatical spices, of myrrh, and frankincense, and of all the powders of the perfumer?
Ni nani huyu anayekuja kutoka jangwani kama nguzo ya moshi, anayenukia manemane na uvumba iliyotengenezwa kwa vikolezo vyote vya mfanyabiashara?
7 Behold threescore valiant ones of the most valiant of Israel, surrounded the bed of Solomon?
Tazama! Ni gari la Solomoni lisindikizwalo na mashujaa sitini, walio wakuu sana wa Israeli,
8 All holding swords, and most expert in war: every man’s sword upon his thigh, because of fears in the night.
wote wamevaa panga, wote wazoefu katika vita, kila mmoja na upanga wake pajani, wamejiandaa kwa ajili ya hofu za usiku.
9 King Solomon hath made him a litter of the wood of Libanus:
Mfalme Solomoni alijitengenezea gari; alilitengeneza kwa mbao kutoka Lebanoni.
10 The pillars thereof he made of silver, the seat of gold, the going up of purple: the midst he covered with charity for the daughters of Jerusalem.
Nguzo zake alizitengeneza kwa fedha, kitako chake kwa dhahabu. Kiti chake kilipambwa kwa zambarau, gari lake likanakshiwa njumu kwa upendo na binti za Yerusalemu.
11 Go forth, ye daughters of Sion, and see king Solomon in the diadem, wherewith his mother crowned him in the day of his espousals, and in the day of the joy of his heart.
Tokeni nje, ninyi binti za Sayuni, mkamtazame Mfalme Solomoni akiwa amevaa taji, taji ambalo mama yake alimvika siku ya arusi yake, siku ambayo moyo wake ulishangilia.

< Song of Solomon 3 >