< Psalms 44 >

1 Unto the end, for the sons of Core, to give understanding. We have heard, O God, with our ears: our fathers have declared to us, The work, thou hast wrought in their days, and in the days of old.
Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
2 Thy hand destroyed the Gentiles, and thou plantedst them: thou didst afflict the people and cast them out.
Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
3 For they got not the possession of the land by their own sword: neither did their own arm save them. But thy right hand and thy arm, and the light of thy countenance: because thou wast pleased with them.
Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
4 Thou art thyself my king and my God, who commandest the saving of Jacob.
Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
5 Through thee we will push down our enemies with the horn: and through thy name we will despise them that rise up against us.
Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
6 For I will not trust in my bow: neither shall my sword save me.
Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
7 But thou hast saved us from them that afflict us: and hast put them to shame that hate us.
Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
8 In God shall we glory all the day long: and in thy name we will give praise for ever.
Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
9 But now thou hast cast us off, and put us to shame: and thou, O God, wilt not go out with our armies.
Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10 Thou hast made us turn our back to our enemies: and they that hated us plundered for themselves.
Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11 Thou hast given us up like sheep to be eaten: thou hast scattered us among the nations.
Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12 Thou hast sold thy people for no price: and there was no reckoning in the exchange of them.
Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13 Thou hast made us a reproach to our neighbours, a scoff and derision to them that are round about us.
Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14 Thou hast made us a byword among the Gentiles: a shaking of the head among the people.
Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
15 All the day long my shame is before me: and the confusion of my face hath covered me,
Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16 At the voice of him that reproacheth and detracteth me: at the face of the enemy and persecutor.
kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17 All these things have come upon us, yet we have not forgotten thee: and we have not done wickedly in they covenant.
Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18 And our heart hath not turned back: neither hast thou turned aside our steps from thy way.
Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 For thou hast humbled us in the place of affliction: and the shadow of death hath covered us.
Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20 If we have forgotten the name of our God, and if we have spread forth our hands to a strange god:
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21 Shall not God search out these things: for he knoweth the secrets of the heart.
Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
22 Because for thy sake we are killed all the day long: we are counted as sheep for the slaughter.
Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
23 Arise, why sleepest thou, O Lord? arise, and cast us not off to the end.
Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
24 Why turnest thou face away? and forgettest our want and our trouble?
Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25 For our soul is humbled down to the dust: our belly cleaveth to the earth.
Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
26 Arise, O Lord, help us and redeem us for thy name’s sake.
Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.

< Psalms 44 >