< Psalms 4 >

1 Unto the end, in verses. A psalm for David. When I called upon him, the God of my justice heard me: when I was in distress, thou hast enlarged me. Have mercy on me: and hear my prayer.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi. Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.
2 O ye sons of men, how long will you be dull of heart? why do you love vanity, and seek after lying?
Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu kuwa aibu mpaka lini? Mtapenda udanganyifu na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
3 Know ye also that the Lord hath made his holy one wonderful: the Lord will hear me when I shall cry unto him.
Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga wale wamchao kwa ajili yake; Bwana atanisikia nimwitapo.
4 Be angry, and sin not: the things you say in your hearts, be sorry for them upon your beds.
Katika hasira yako, usitende dhambi. Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya mkiichunguza mioyo yenu.
5 Offer up the sacrifice of justice, and trust in the Lord: many say, Who sheweth us good things?
Toeni dhabihu zilizo haki; mtegemeeni Bwana.
6 The light of thy countenance O Lord, is signed upon us: thou hast given gladness in my heart.
Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye kutuonyesha jema lolote?” Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.
7 By the fruit of their corn, their wine and oil, they are multiplied.
Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
8 In peace in the selfsame I will sleep, and I will rest: For thou, O Lord, singularly hast settled me in hope.
Nitajilaza chini na kulala kwa amani, kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana, waniwezesha kukaa kwa salama.

< Psalms 4 >