< Psalms 143 >

1 Hear, O Lord, my prayer: give ear to my supplication in thy truth: hear me in thy justice.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
2 And enter not into judgment with thy servant: for in thy sight no man living shall be justified.
Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
3 For the enemy hath persecuted my soul: he hath brought down my life to the earth. He hath made me to dwell in darkness as those that have been dead of old:
Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
4 And my spirit is in anguish within me: my heart within me is troubled.
Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
5 I remembered the days of old, I meditated on all thy works: I meditated upon the works of thy hands.
Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
6 I stretched forth my hands to thee: my soul is as earth without water unto thee.
Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
7 Hear me speedily, O Lord: my spirit hath fainted away. Turn not away thy face from me, lest I be like unto them that go down into the pit.
Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
8 Cause me to hear thy mercy in the morning; for in thee have I hoped. Make the way known to me, wherein I should walk: for I have lifted up my soul to thee.
Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
9 Deliver me from my enemies, O Lord, to thee have I fled:
Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
10 Teach me to do thy will, for thou art my God. Thy good spirit shall lead me into the right land:
Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
11 For thy name’s sake, O Lord, thou wilt quicken me in thy justice. Thou wilt bring my soul out of trouble:
Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
12 And in thy mercy thou wilt destroy my enemies. And thou wilt cut off all them that afflict my soul: for I am thy servant.
Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.

< Psalms 143 >