< Psalms 120 >

1 In my trouble I cried to the Lord: and he heard me.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 O Lord, deliver my soul from wicked lips, and a deceitful tongue.
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 What shall be given to thee, or what shall be added to thee, to a deceitful tongue.
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 The sharp arrows of the mighty, with coals that lay waste.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Woe is me, that my sojourning is prolonged! I have dwelt with the inhabitants of cedar:
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 My soul hath been long a sojourner.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 With them that hate peace I was peaceable: when I spoke to them they fought against me without cause.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.

< Psalms 120 >