< Philemon 1 >

1 Paul, a prisoner of Christ Jesus, and Timothy, a brother: to Philemon, our beloved and fellow labourer;
Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na ndugu Timotheo kwa Filemoni, mpendwa rafiki yetu na mtenda kazi pamoja nasi,
2 And to Appia, our dearest sister, and to Archippus, our fellow soldier, and to the church which is in thy house:
na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipas askari mwenzetu, na kwa kanisa lile linalokutana nyumbani kwako.
3 Grace to you and peace from God our Father, and from the Lord Jesus Christ.
Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
4 I give thanks to my God, always making a remembrance of thee in my prayers.
Wakati wote namshukuru Mungu. Ninakutaja katika maombi yangu.
5 Hearing of thy charity and faith, which thou hast in the Lord Jesus, and towards all the saints:
Nimesikia upendo na imani uliyonayo katika Bwana Yesu na kwa ajili ya waumini wote.
6 That the communication of thy faith may be made evident in the acknowledgment of every good work, that is in you in Christ Jesus.
Ninaomba kwamba ushirika wa imani yenu iwe na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema lililoko kati yetu katika Kristo.
7 For I have had great joy and consolation in thy charity, because the bowels of the saints have been refreshed by thee, brother.
Kwa kuwa nimekuwa na furaha na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa sababu mioyo ya waumini imekuwa ikitulizwa nawe, ndugu.
8 Wherefore though I have much confidence in Christ Jesus, to command thee that which is to the purpose:
Kwa hiyo, ingawa nina ujasiri wote katika Kristo kukuamuru wewe kufanya kile unachoweza kufanya,
9 For charity sake I rather beseech, whereas thou art such a one, as Paul an old man, and now a prisoner also of Jesus Christ.
lakini kwa sababu ya upendo, badala yake nakusihi - mimi, Paulo niliye mzee, na sasa ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu.
10 I beseech thee for my son, whom I have begotten in my bands, Onesimus,
Ninakusihi kuhusu mwanangu Onesmo, niliyemzaa katika vifungo vyangu.
11 Who hath been heretofore unprofitable to thee, but now is profitable both to me and thee,
Kwa kuwa mwanzoni hakukufaa, lakini sasa anakufaa wewe na mimi.
12 Whom I have sent back to thee. And do thou receive him as my own bowels.
Nimemtuma- yeye ambaye ni wa moyo wangu hasa - kurudi kwako.
13 Whom I would have retained with me, that in thy stead he might have ministered to me in the bands of the gospel:
Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niwako kifungoni kwa ajili ya injili.
14 But without thy counsel I would do nothing: that thy good deed might not be as it were of necessity, but voluntary.
Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
15 For perhaps he therefore departed for a season from thee, that thou mightest receive him again for ever: (aiōnios g166)
Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele. (aiōnios g166)
16 Not now as a servant, but instead of a servant, a most dear brother, especially to me: but how much more to thee both in the flesh and in the Lord?
Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa, hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
17 If therefore thou count me a partner, receive him as myself.
Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
18 And if he hath wronged thee in any thing, or is in thy debt, put that to my account.
Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
19 I Paul have written it with my own hand: I will repay it: not to say to thee, that thou owest me thy own self also.
Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: mimi nitakulipa. Sisemi kwako kwamba nakudai maisha yako hasa.
20 Yea, brother. May I enjoy thee in the Lord. Refresh my bowels in the Lord.
Naam ndugu, acha nipate furaha ya Bwana toka kwako: uburudishe moyo wangu katika Kristo.
21 Trusting in thy obedience, I have written to thee: knowing that thou wilt also do more than I say.
Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
22 But withal prepare me also a lodging. For I hope that through your prayers I shall be given unto you.
Wakati huo huo andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitakutembelea hivi karibuni.
23 There salute thee Epaphras, my fellow prisoner in Christ Jesus;
Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
24 Mark, Aristarchus, Demas, and Luke my fellow labourers.
na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
25 The grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit. Amen.
Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.

< Philemon 1 >