< Numbers 33 >

1 These are the mansions of the children of Israel, who went out of Egypt by their troops under the conduct of Moses and Aaron,
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Which Moses wrote down according to the places of their encamping, which they changed by the commandment of the Lord.
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 Now the children of Israel departed from Ramesses the first month, on the fifteenth day of the first month, the day after the phase, with a mighty hand, in the eight of all the Egyptians,
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 Who were burying their firstborn, whom the Lord had slain (upon their gods also he had executed vengeance, )
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 And they camped in Soccoth.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 And from Soccoth they came into Etham, which is in the uttermost borders of the wilderness.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Departing from thence they came over against Phihahiroth, which looketh towards Beelsephon, and they camped before Magdalum.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 And departing from Phihahiroth, they passed through the midst of the sea into the wilderness: and having marched three days through the desert of Etham, they camped in Mara.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 And departing from Mara, they came into Elim, where there were twelve fountains of waters, and seventy palm trees: and there they camped.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 But departing from thence also, they pitched their tents by the Red Sea. And departing from the Red Sea,
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 They camped in the desert of Sin.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 And they removed from thence, and came to Daphca.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 And departing from Daphca, they camped in Alus.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 And departing from Alus, they pitched their tents in Raphidim, where the people wanted water to drink.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 And departing from Raphidim, they camped in the desert of Sinai.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 But departing also from the desert of Sinai, they came to the graves of lust.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 And departing from the graves of lust, they camped in Haseroth.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 And from Haseroth they came to Rethma.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 And departing from Rethma, they camped in Remmomphares.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 And they departed from thence and came to Lebna.
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Removing from Lebna they camped in Ressa.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 And departing from Ressa, they came to Ceelatha.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 And they removed from thence and camped in the mountain Sepher.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Departing from the mountain Sepher, they came to Arada.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 From thence they went and camped in Maceloth.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 And departing from Maceloth, they came to Thahath.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Removing from Thahath they camped in Thare.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 And they departed from thence, and pitched their tents in Methca.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 And removing from Methca, they camped in Hesmona.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 And departing from Hesmona, they came to Moseroth.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 And removing from Moseroth, they camped in Benejaacan.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 And departing from Benejaacan, they came to mount Gadgad.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 From thence they went and camped in Jetebatha.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 And from Jetebatha they came to Hebrona.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 And departing from Hebrona, they camped in Asiongaber.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 They removed from thence and came into the desert of Sin, which is Cades.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 And departing from Cades, they camped in mount Her, in the uttermost borders of the land of Edom.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 And Aaron the priest went up into mount Hor at the commandment of the Lord: and there he died in the fortieth year of the coming forth of the children of Israel out of Egypt, the fifth month, the first day of the month,
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 When he was a hundred and twenty-three years old.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 And king Arad the Chanaanite, who dwelt towards the south, heard that the children of Israel were come to the land of Chanaan.
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 And they departed from mount Her, and camped in Salmona.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 From whence they removed and came to Phunon.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 And departing from Phunon, they camped in Oboth.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 And from Oboth they came to Ijeabarim, which is in the borders of the Moabites.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 And departing from Ijeabarim they pitched their tents in Dibongab.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 From thence they went and camped in Helmondeblathaim.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 And departing from Helmondeblathaim, they came to the mountains of Abarim over against Nabo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 And departing from the mountains of Abarim, they passed to the plains of Moab, by the Jordan, over against Jericho.
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 And there they camped from Bethsi moth even to Ablesatim in the plains of the Moabites,
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 Where the Lord said to Moses:
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 Command the children of Israel, and say to them: When you shall have passed over the Jordan, entering into the land of Chanaan,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 Destroy all the inhabitants of that land: beat down their pillars, and break in pieces their statues, and waste all their high places,
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 Cleansing the land, and dwelling in it. For I have given it you for a possession.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 And you shall divide it among you by lot. To the more you shall give a larger part, and to the fewer a lesser. To every one as the lot shall fall, so shall the inheritance be given. The possession shall be divided by the tribes and the families.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 But if you will not kill the inhabitants of the land: they that remain, shall be unto you as nails in your eyes, and spears in your sides, and they shall be your adversaries in the land of your habitation.
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 And whatsoever I had thought to do to them, I will do to you.
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< Numbers 33 >