< Numbers 10 >

1 And the Lord spoke to Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose:
2 Make thee two trumpets of beaten silver, wherewith thou mayest call together the multitude when the camp is to be removed.
“Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
3 And when thou shalt sound the trumpets, all the multitude shall gather unto thee to the door of the tabernacle of the covenant.
Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
4 If thou sound but once, the princes and the heads of the multitude of Israel shall come to thee.
Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
5 But if the sound of the trumpets be longer, and with interruptions, they that are on the east side, shall first go forward.
Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
6 And at the second sounding and like noise of the trumpet, they who lie on the south side shall take up their tents. And after this manner shall the rest do, when the trumpets shall sound for a march.
Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
7 But when the people is to be gathered together, the sound of the trumpets shall be plain, and they shall not make a broken sound.
Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
8 And the sons of Aaron the priest shall sound the trumpets: and this shall be an ordinance for ever in your generations.
“Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
9 If you go forth to war out of your land against the enemies that fight against you, you shall sound aloud with the trumpets, and there shall be a remembrance of you before the Lord your God, that you may be delivered out of the hands of your enemies.
Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
10 If at any time you shall have a banquet, and on your festival days, and on the first days of your months, you shall sound the trumpets over the holocausts, and the sacrifices of peace offerings, that they may be to you for a remembrance of your God. I am the Lord your God.
Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
11 The second year, in the second month, the twentieth day of the month, the cloud was taken up from the tabernacle of the covenant.
Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
12 And the children of Israel marched by their troops from the desert of Sinai, and the cloud rested in the wilderness of Pharan.
Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
13 And the first went forward according to the commandment of the Lord by the hand of Moses.
Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
14 The sons of Juda by their troops: whose prince was Nahasson the son of Aminadab.
Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
15 In the tribe of the sons of Issachar, the prince was Nathanael the son of Suar.
Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
16 In the tribe of Zabulon, the prince was Eliab the son of Helon.
naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
17 And the tabernacle was taken down, and the sons of Gerson and Merari set forward, bearing it.
Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
18 And the sons of Ruben also marched, by their troops and ranks, whose prince was Helisur the son of Sedeur.
Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
19 And in the tribe of Simeon, the prince was Salamiel the son of Surisaddai.
Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
20 And in the tribe of Cad, the prince was Eliasaph the son of Duel.
naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
21 Then the Caathites also marched carrying the sanctuary. So long was the tabernacle carried, till they same to the place of setting it up.
Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
22 The sons of Ephraim also moved their camp by their troops, in whose army the prince was Elisama the son of Ammiud.
Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
23 And in the tribe of the sons of Manasses, the prince was Gamaliel the son of Phadassur.
Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
24 And in the tribe of Benjamin, the prince was Abidan the son of Gedeon.
naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
25 The last of all the camp marched the sons of Dan by their troops, in whose army the prince was Ahiezer the son of Ammisaddai.
Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
26 And in the tribe of the sons of Aser, the prince was Phegiel the son of Ochran.
Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
27 And in the tribe of the sons of Nephtali, the prince was Ahira the son of Enan.
naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
28 This was the order of the camps, and marches of the children of Israel by their troops, when they set forward.
Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
29 And Moses said to Hobab the son of Raguel the Madianite, his kinsman: We are going towards the place which the Lord will give us: come with us, that we may do thee good: for the Lord hath promised good things to Israel.
Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
30 But he answered him: I will not go with thee, but I will return to my country, wherein I was born.
Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
31 And he said: Do not leave us: for thou knowest in what places we should encamp in the wilderness, and thou shalt be our guide.
Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
32 And if thou comest with us, we will give thee what is the best of the riches which the Lord shall deliver to us.
Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
33 So they marched from the mount of the Lord three days’ journey, and the ark of the covenant of the Lord went before them, for three days providing a place for the camp.
Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
34 The cloud also of the Lord was over them by day when they marched.
Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
35 And when the ark was lifted up, Moses said: Arise, O Lord, and let thy enemies be scattered, and let them that hate thee, flee from before thy face.
Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
36 And when it was set down, he said: Return, O Lord, to the multitude of the host of Israel.
Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”

< Numbers 10 >