< Matthew 13 >

1 The same day Jesus going out of the house, sat by the sea side.
Katika siku hiyo Yesu aliondoka nyumbani na kukaa kando ya bahari.
2 And great multitudes were gathered unto him, so that he went up into a boat and sat: and all the multitude stood on the shore.
Umati mkubwa ulikusanyika kwa kumzunguka, aliingia ndani ya mtumbwi na kukaa ndani yake. Umati wote walisimama kando ya bahari.
3 And he spoke to them many things in parables, saying: Behold the sower went forth to sow.
Kisha Yesu alisema maneno mengi kwa mifano, Alisema, “Tazama, mpanzi alienda kupanda.
4 And whilst he soweth some fell by the way side, and the birds of the air came and ate them up.
Alipokuwa akipanda baadhi ya mbegu zilianguka kando ya njia na ndege walikuja wakazidonoa.
5 And other some fell upon stony ground, where they had not much earth: and they sprung up immediately, because they had no deepness of earth.
Mbegu zingine zilianguka juu ya mwamba, ambapo hazikupata udongo wa kutosha. Ghafla zilichipuka kwa sababu udongo haukuwa na kina.
6 And when the sun was up they were scorched: and because they had not root, they withered away.
Lakini jua lilipo chomoza zilichomwa kwa sababu hazikuwa na mizizi, na zilikauka.
7 And others fell among thorns: and the thorns grew up and choked them.
Mbengu zingine zilianguka kati ya miti yenye miiba. Miti yenye miiba ilirefuka juu ikaisonga.
8 And others fell upon good ground: and they brought forth fruit, some an hundredfold, some sixtyfold, and some thirtyfold.
Mbegu zingine zilianguka kwenye udongo mzuri na kuzaa mbegu, zingine mara mia moja zaidi, zingine sitini na zingine thelathini
9 He that hath ears to hear, let him hear.
Aliye na masikio na asikie.
10 And his disciples came and said to him: Why speakest thou to them in parables?
Wanafunzi walikuja na kumwambia Yesu, “Kwa nini unazungumza na makutano kwa mifano?”
11 Who answered and said to them: Because to you it is given to know the mysteries of the kingdom of heaven: but to them it is not given.
Yesu alijibu kuwaambia, “Mmepewa upendeleo wa kufahamu siri za ufalme wa mbinguni, bali kwao hawajapewa.
12 For he that hath, to him shall be given, and he shall abound: but he that hath not, from him shall be taken away that also which he hath.
Lakini yeyote aliyenacho, kwake yeye ataongezewa zaidi, na atapata faida kubwa. Ilasiye nacho hata kile alichonacho atanyang'anywa.
13 Therefore do I speak to them in parables: because seeing they see not, and hearing they hear not, neither do they understand.
Hivyo naongea nao kwa mifano kwa sababu ingawa wanaona, wasione kweli. Na ingawa wanasikia wasisikie wala kufahamu.
14 And the prophecy of Isaias is fulfilled in them, who saith: By hearing you shall hear, and shall not understand: and seeing you shall see, and shall not perceive.
Unabii wa Isaya umetimia kwao, ule usemao, “Msikiapo msikie, lakini kwa namna yoyote hamtaelewa; wakati mwonapo muweze kuona, lakini kwa namna yeyote ile msijue.
15 For the heart of this people is grown gross, and with their ears they have been dull of hearing, and their eyes they have shut: lest at any time they should see with their eyes, and hear with their ears, and understand with their heart, and be converted, and I should heal them.
Na mioyo ya watu hawa imekuwa giza, ni vigumu kusikia, na wamefumba macho yao, ili wasiweze kuona kwa macho yao, au kusikia kwa masikio yao, au kufahamu kwa mioyo yao, hivyo wangenigeukia tena, na ningewaponya.'
16 But blessed are your eyes, because they see, and your ears, because they hear.
Bali macho yenu yamebarikiwa, kwa kuwa yanaona, na masikio yenu kwa kuwa yanasikia.
17 For, amen, I say to you, many prophets and just men have desired to see the things that you see, and have not seen them, and to hear the things that you hear and have not heard them.
Hakika nawaambia manabii wengi na watu wenye haki walikuwa na hamu ya kuyaona mambo yale myaonayo, na hawakuweza kuyaona. Walitamani kusikia mambo yale mnayosikia, hawakuyasikia.
18 Hear you therefore the parable of the sower.
. Sasa sikilizeni mfano wa mpanzi.
19 When any one heareth the word of the kingdom, and understandeth it not, there cometh the wicked one, and catcheth away that which was sown in his heart: this is he that received the seed by the way side.
Wakati yeyote asikiapo neno la ufalme na asilifahamu, ndipo mwovu huja na kukinyakua kilichokwisha kupandwa ndani ya moyo wake. Hii ni mbegu ile iliyopandwa kando ya njia.
20 And he that received the seed upon stony ground, is he that heareth the word, and immediately receiveth it with joy.
Yeye aliyepandwa katika miamba ni yule asikiaye neno na kulipokea haraka kwa furaha.
21 Yet hath he not root in himself, but is only for a time: and when there ariseth tribulation and persecution because of the word, he is presently scandalized.
Bado hana mizizi ndani yake, ila huvumilia kwa kitambo kifupi. Wakati matatizo au mateso yanapotokea kwa sababu ya neno hujikwaa ghafla.
22 And he that received the seed among thorns, is he that heareth the word, and the care of this world and the deceitfulness of riches choketh up the word, and he becometh fruitless. (aiōn g165)
Aliyepandwa kati ya miti ya miiba, huyu ni yule alisikiaye neno lakini masumbuko ya ulimwengu na udaganyifu wa utajiri hulisonga lile neno lisije likazaa matunda. (aiōn g165)
23 But he that received the seed upon good ground, is he that heareth the word, and understandeth, and beareth fruit, and yieldeth the one an hundredfold, and another sixty, and another thirty.
Aliyepandwa kwenye udongo mzuri, huyu ni yule asikiaye neno na kulifahamu. Huyu ni yule azaaye matunda na kuendelea kuzaa moja zaidi ya mara mia, nyingine sitini, nyingine thelathini.''
24 Another parable he proposed to them, saying: The kingdom of heaven is likened to a man that sowed good seeds in his field.
Yesu aliwapa mfano mwingine. Akisema, “Ufalme wa mbinguni unafananishwa na mtu aliye panda mbengu nzuri katika shamba lake
25 But while men were asleep, his enemy came and oversowed cockle among the wheat and went his way.
Lakini watu waliposinzia, adui wake akaja pia akapanda magugu katikati ya ngano kisha akaenda zake.
26 And when the blade was sprung up, and had brought forth fruit, then appeared also the cockle.
Baadaye ngano ilipoota na kutoa mazao yake, ndipo magugu yalitokea pia.
27 And the servants of the goodman of the house coming said to him: Sir, didst thou not sow good seed in thy field? whence then hath it cockle?
Na watumishi wa mwenye shamba walikuja wakamwambia, 'Bwana, hukupanda mbengu nzuri katika shamba lako? Imekuwaje sasa lina magugu?
28 And he said to them: An enemy hath done this. And the servants said to him: Wilt thou that we go and gather it up?
Akawaambia, Adui ametenda hili.' Watumishi walimwambia, “Kwa hiyo unataka twende tukayang'oe?”
29 And he said: No, lest perhaps gathering up the cockle, you root up the wheat also together with it.
Mwenye shamba akisema, 'Hapana, wakati mnayang'oa magugu mtang'oa pamoja na ngano.
30 Suffer both to grow until the harvest, and in the time of the harvest I will say to the reapers: Gather up first the cockle, and bind it into bundles to burn, but the wheat gather ye into my barn.
Yaacheni yakue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati wa mavuno nitasema kwa wavunaji, 'Kwanza yang'oeri magugu na yafungeni matita matita na kuyachoma, lakini kusanyeni ngano katika ghala langu.''''
31 Another parable he proposed unto them, saying: The kingdom of heaven is like to a grain of mustard seed, which a man took and sowed in his field.
Kisha Yesu aliwatolea mfano mwingine. Akasema, “Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake.
32 Which is the least indeed of all seeds; but when it is grown up, it is greater than all herbs, and becometh a tree, so that the birds of the air come, and dwell in the branches thereof.
Mbegu hii kwa hakika ni ndogo kuliko mbegu zingine zote. Lakini imeapo huwa kubwa kuliko mimea yote ya bustani, huwa mti, kiasi kwamba ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake.”
33 Another parable he spoke to them: The kingdom of heaven is like to leaven, which a woman took and hid in three measures of meal, until the whole was leavened.
Akawaambia mfano mwingine tena.”Ufalme wa mbinguni ni kama chachu ile iliyo twaliwa na mwanamke na kuichanganya kwa vipimo vitatu kwa unga mpaka viumuke.
34 All these things Jesus spoke in parables to the multitudes: and without parables he did not speak to them.
Hayo yote Yesu aliyasema kwenye umati kwa mifano. Na pasipo mifano hakusema chochote kwao.
35 That it might be fulfilled which was spoken by the prophet, saying: I will open my mouth in parables, I will utter things hidden from the foundation of the world.
Hii ilikuwa kwamba kile kilichokwisha semwa kupitia kwa nabii kiweze kutimia, pale aliposema, “Nitafumbua kinywa changu katika mifano. Nitasema mambo yale yaliyokuwa yamefichwa tangu misingi ya ulimwengu”.
36 Then having sent away the multitudes, he came into the house, and his disciples came to him, saying: Expound to us the parable of the cockle of the field.
Kisha Yesu aliwaacha makutano na kwenda nyumbani. Wanafunzi wake walimwendea na kusema, “Tufafanulie mfano wa magugu ya shambani.''
37 Who made answer and said to them: He that soweth the good seed, is the Son of man.
Yesu alijibu na kusema, “Apandae mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
38 And the field, is the world. And the good seed are the children of the kingdom. And the cockle, are the children of the wicked one.
Shamba ni ulimwengu; na mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu, na adui aliye zipanda ni ibilisi.
39 And the enemy that sowed them, is the devil. But the harvest is the end of the world. And the reapers are the angels. (aiōn g165)
Na mavuno ni mwisho wa ulimwengu, na wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
40 Even as cockle therefore is gathered up, and burnt with fire: so shall it be at the end of the world. (aiōn g165)
Kama vile magugu yanavyo kusanywa na kuchomwa moto, hivyo ndivyo itakavyo kuwa mwisho wa ulimwengu. (aiōn g165)
41 The Son of man shall send his angels, and they shall gather out of his kingdom all scandals, and them that work iniquity.
Mwana wa Adamu atatuma malaika wake, na kukusanya kutoka katika ufalme wake mambo yote yaliyosababisha dhambi na wale watendao maasi.
42 And shall cast them into the furnace of fire: there shall be weeping and gnashing of teeth.
Watawatupa wote katika tanuru la moto, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
43 Then shall the just shine as the sun, in the kingdom of their Father. He that hath ears to hear, let him hear.
Ndipo watu wenye haki watakapong'aa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio na sikie.
44 The kingdom of heaven is like unto a treasure hidden in a field. Which a man having found, hid it, and for joy thereof goeth, and selleth all that he hath, and buyeth that field.
Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa shambani. Mtu akaiona na kuificha. Katika furaha yake akaenda kuuza vyote alivyokuwa navyo, na kulinunua shamba.
45 Again the kingdom of heaven is like to a merchant seeking good pearls.
Tena, ufalme wa mbinguni ni kama mtu anayefanya biashara atafutaye lulu yenye thamani.
46 Who when he had found one pearl of great price, went his way, and sold all that he had, and bought it.
Wakati alipoiona ile yenye thamani, alienda akauza kila kitu alichokuwa nacho na akainunua.
47 Again the kingdom of heaven is like to a net cast into the sea, and gathering together of all kind of fishes.
Ufalme wa mbinguni ni kama nyavu iliyo ndani ya bahari, na kwamba hukusanya viumbe vya kila aina.
48 Which, when it was filled, they drew out, and sitting by the shore, they chose out the good into vessels, but the bad they cast forth.
Ulipojaa wavuvi waliuvuta ufukweni. Kisha wakakaa chini wakakusanya vitu vyema ndani ya vyombo, lakini visivyo na thamani vilitupwa mbali.
49 So shall it be at the end of the world. The angels shall go out, and shall separate the wicked from among the just. (aiōn g165)
Itakuwa namna hii katika mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenga watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki. (aiōn g165)
50 And shall cast them into the furnace of fire: there shall be weeping and gnashing of teeth.
Na kuwatupa ndani ya tanuru ya moto, ambako kutakuwa na maombolezo na kusaga meno.
51 Have ye understood all these things? They say to him: Yes.
Mmefahamu mambo yote haya? Wanafunzi walimjibu, ''Ndiyo.''
52 He said unto them: Therefore every scribe instructed in the kingdom of heaven, is like to a man that is a householder, who bringeth forth out of his treasure new things and old.
Kisha Yesu akawambia, ''Kila mwandishi ambaye amekuwa mwanafunzi wa ufalme anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.''
53 And it came to pass: when Jesus had finished these parables, he passed from thence.
IkawaYesu alipomaliza mifano yote hiyo, akaondoka katika sehemu hiyo.
54 And coming into his own country, he taught them in their synagogues, so that they wondered and said: How came this man by this wisdom and miracles?
Kisha Yesu akafika katika mkoa wake na akawafundisha watu katika sinagogi. Matokeo yake ni kuwa walishangaa na kusema, “Ni wapi mtu huyu alipopata hekima hii na miujiza hii?
55 Is not this the carpenter’s son? Is not his mother called Mary, and his brethren James, and Joseph, and Simon, and Jude:
Mtu huyu siyo mwana wa seremala? Mariamu siyo mamaye? Na ndugu zake siyo Yakobo, Yusuph, Simoni na Yuda?
56 And his sisters, are they not all with us? Whence therefore hath he all these things?
Na dada zake tunao hapa petu? Basi mtu huyu ameyapata wapi haya yote?”.
57 And they were scandalized in his regard. But Jesus said to them: A prophet is not without honour, save in his own country, and in his own house.
Aliwachukiza. Lakini Yesu aliwambia, “Nabii hakosi kuwa na heshima isipokuwa kwao na katika nchi yao.
58 And he wrought not many miracles there, because of their unbelief.
Na hakuweza kufanya miujiza mingi kwa sababu hawakuwa na imani naye.

< Matthew 13 >