< Mark 11 >

1 And when they were drawing near to Jerusalem and to Bethania at the mount of Olives, he sendeth two of his disciples,
Wakati huo walipokuja Yerusalemu, walipokaribia Besthfage na Bethania, katika Mlima wa Mizeituni, Yesu aliwatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake
2 And saith to them: Go into the village that is over against you, and immediately at your coming in thither, you shall find a colt tied, upon which no man yet hath sat: loose him, and bring him.
na aliwaambia, “Nendeni katika kijiji kinachokabiliana nasi. Mara mtakapoingia humo, mtamkuta mwanapunda ambaye hajapandwa. Mfungueni na mmlete kwangu.
3 And if any man shall say to you, What are you doing? say ye that the Lord hath need of him: and immediately he will let him come hither.
Na kama yeyote akiwaambia, 'Kwa nini mnafanya hivi'?, mnapaswa kusema, 'Bwana anamhitaji na mara atamrudisha hapa'.”
4 And going their way, they found the colt tied before the gate without, in the meeting of two ways: and they loose him.
Walikwenda na kumkuta mwanapunda amefungwa nje mlangoni kwenye mtaa ulio wazi, nao walimfungua.
5 And some of them that stood there, said to them: What do you loosing the colt?
Na baadhi ya watu walikuwa wamesimama pale na waliwaambia, “Mnafanya nini, kumfungua mwanapunda huyo?”
6 Who said to them as Jesus had commanded them; and they let him go with them.
Waliwaambia kama Yesu alivyowaambia, na watu wakawaacha waende.
7 And they brought the colt to Jesus; and they lay their garments on him, and he sat upon him.
Wanafunzi wawili walimleta mwanapunda kwa Yesu na walitandika mavazi yao juu yake ili Yesu aweze kumpanda.
8 And many spread their garments in the way: and others cut down boughs from the trees, and strewed them in the way.
Watu wengi wakatandika mavazi yao barabarani, na wengine wakatandika matawi waliyoyakata kutoka mashambani.
9 And they that went before and they that followed, cried, saying: Hosanna, blessed is he that cometh in the name of the Lord.
Wale waliokwenda mbele yake na wale waliomfuata walipiga kelele, “Hosana! Amebarikiwa anayekuja kwa jina la Bwana.
10 Blessed be the kingdom of our father David that cometh: Hosanna in the highest.
Ubarikiwe ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi! Hosana kwa aliye juu”
11 And he entered into Jerusalem, into the temple: and having viewed all things round about, when now the eventide was come, he went out to Bethania with the twelve.
Ndipo Yesu aliingia Yerusalemu na alikwenda hekaluni na alitazama kila kitu. Sasa, wakati ulikuwa umeenda, alikwenda Bethania pamoja nao kumi na wawili.
12 And the next day when they came out from Bethania, he was hungry.
Siku iliyofuata, wakati walipokuwa wakirudi kutoka Bethania, alikuwa na njaa.
13 And when he had seen afar off a fig tree having leaves, he came if perhaps he might find any thing on it. And when he was come to it, he found nothing but leaves. For it was not the time for figs.
Na akaona mti wa mtini uliokuwa na majani kwa mbali, alikwenda kutazama kama angeweza kupata chochote juu yake. Na wakati alipokwenda kwa huo, hakupata chochote isipokuwa majani, kwa kuwa haikuwa majira ya mtini.
14 And answering he said to it: May no man hereafter eat fruit of thee any more for ever. And his disciples heard it. (aiōn g165)
Aliuambia, “Hakuna yeyote atakayekula tunda kutoka kwako tena”. Na wanafunzi wake wakasikia. (aiōn g165)
15 And they came to Jerusalem. And when he was entered into the temple, he began to cast out them that sold and bought in the temple, and overthrew the tables of the moneychangers, and the chairs of them that sold doves.
Walikuja Yerusalemu, naye aliingia hekaluni na kuanza kuwatoa nje wauzaji na wanunuzi ndani ya hekalu. Alizipindua meza za wabadilishaji wa fedha na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
16 And he suffered not that any man should carry a vessel through the temple;
Hakumruhusu yeyote kubeba chochote hekaluni kilichoweza kuuzwa.
17 And he taught, saying to them: Is it not written, My house shall be called the house of prayer to all nations? But you have made it a den of thieves.
Aliwafundisha na akasema, “Je haikuandikwa, 'nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote'? Lakini mmeifanya pango la wanyang'anyi”.
18 Which when the chief priests and the scribes had heard, they sought how they might destroy him. For they feared him, because the whole multitude was in admiration at his doctrine.
Makuhani wakuu na waandishi walisikia alivyokuwa amesema, nao walitafuta njia ya kumwua. Hata hivyo walimwogopa kwa sababu umati ulishangazwa na mafundisho yake.
19 And when evening was come, he went forth out of the city.
Na kila wakati jioni ilipofika, waliondoka mjini.
20 And when they passed by in the morning they saw the fig tree dried up from the roots.
Walipokuwa wakitembea asubuhi, waliuona mti wa mtini umekauka mpaka kwenye mizizi yake.
21 And Peter remembering, said to him: Rabbi, behold the fig tree, which thou didst curse, is withered away.
Petro alikumbuka na kusema, “Rabi! Tazama, mti wa mtini ulioulaani umekauka”.
22 And Jesus answering, saith to them: Have the faith of God.
Yesu aliwajibu, “Muwe na imani katika Mungu.
23 Amen I say to you, that whosoever shall say to this mountain, Be thou removed and be cast into the sea, and shall not stagger in his heart, but believe, that whatsoever he saith shall be done; it shall be done unto him.
Amini nawaambia kwamba kila auambiaye mlima huu, 'Ondoka, na ukajitupe mwenyewe baharini, 'na kama hana mashaka moyoni mwake lakini anaamini kwamba alichokisema kitatokea, hivyo ndivyo Mungu atakavyofanya.
24 Therefore I say unto you, all things, whatsoever you ask when ye pray, believe that you shall receive; and they shall come unto you.
Kwa hiyo ninawaambia: kila kitu muombacho na kuuliza kwa ajili yake, aminini kwamba mmepokea, navyo vitakuwa vyenu.
25 And when you shall stand to pray, forgive, if you have aught against any man; that your Father also, who is in heaven, may forgive you your sins.
Wakati mnaposimama na kuomba, mnapaswa kusamehe chochote mlichonacho dhidi ya yeyote, ili kwamba Baba yenu aliye mbinguni awasamehe pia ninyi makosa yenu.
26 But if you will not forgive, neither will your Father that is in heaven, forgive you your sins.
(Zingatia: Mstari huu, “Lakini msiposamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatasamehe dhambi zenu” haumo kwenye nakala za kale).
27 And they come again to Jerusalem. And when he was walking in the temple, there come to him the chief priests and the scribes and the ancients,
Walikuja Yerusalemu tena. Na Yesu alipokuwa akitembea hekaluni, makuhani wakuu, waandishi na wazee walikuja kwake.
28 And they say to him: By what authority dost thou these things? and who hath given thee this authority that thou shouldst do these things?
Walimwambia, “Kwa mamlaka gani unafanya mambo haya?” Na ni nani aliyekupa mamlaka kuyafanya haya?”
29 And Jesus answering, said to them: I will also ask you one word, and answer you me, and I will tell you by what authority I do these things.
Yesu aliwaambia, “Nitawauliza swali moja. Niambieni na mimi nitawaambia kwa mamlaka gani ninayafanya mambo haya.
30 The baptism of John, was it from heaven, or from men? Answer me.
Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au ulitoka kwa wanadamu? Nijibuni.”
31 But they thought with themselves, saying: If we say, From heaven; he will say, Why then did you not believe him?
Walijadiliana miongoni mwao na kushindana na kusema, “Kama tukisema, 'Kutoka mbinguni,' atasema, 'Kwa nini basi hamkumwamini?'
32 If we say, From men, we fear the people. For all men counted John that he was a prophet indeed.
Lakini kama tukisema, 'Kutoka kwa wanadamu,'...” Waliwaogopa watu, kwa kuwa wote walishikilia kwamba Yohana alikuwa Nabii.
33 And they answering, say to Jesus: We know not. And Jesus answering, saith to them: Neither do I tell you by what authority I do these things.
Ndipo walimjibu Yesu na kusema, “Hatujui. Ndipo Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani nayafanya mambo haya.

< Mark 11 >