< Luke 17 >

1 And he said to his disciples: It is impossible that scandals should not come: but woe to him through whom they come.
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mambo yanayosababisha watu watende dhambi hayana budi kutukia. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha.
2 It were better for him, that a millstone were hanged about his neck, and he cast into the sea, than that he should scandalize one of these little ones.
Ingekuwa heri kama mtu huyo angefungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutoswa baharini, kuliko kumsababisha mmojawapo wa hawa wadogo kutenda dhambi.
3 Take heed to yourselves. If thy brother sin against thee, reprove him: and if he do penance, forgive him.
Kwa hiyo, jilindeni. “Kama ndugu yako akikukosea mwonye, naye akitubu, msamehe.
4 And if he sin against thee seven times in a day, and seven times in a day be converted unto thee, saying, I repent; forgive him.
Kama akikukosea mara saba kwa siku moja na mara saba kwa siku moja akaja kwako akisema, ‘Ninatubu,’ msamehe.”
5 And the apostles said to the Lord: Increase our faith.
Mitume wake wakamwambia Bwana, “Tuongezee imani.”
6 And the Lord said: If you had faith like to a grain of mustard seed, you might say to this mulberry tree, Be thou rooted up, and be thou transplanted into the sea: and it would obey you.
Bwana akawajibu, “Kama mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu, ‘Ngʼoka ukaote baharini,’ nao ungewatii.
7 But which of you having a servant ploughing, or feeding cattle, will say to him, when he is come from the field: Immediately go, sit down to meat:
“Ikiwa mmoja wenu ana mtumishi anayelima shambani au anayechunga kondoo, je, mtumishi huyo arudipo atamwambia, ‘Karibu hapa keti ule chakula?’
8 And will not rather say to him: Make ready my supper, and gird thyself, and serve me, whilst I eat and drink, and afterwards thou shalt eat and drink?
Je, badala yake, hatamwambia, ‘Niandalie chakula, nile, jifunge unitumikie ninapokula na kunywa; baadaye waweza kula na kunywa?’
9 Doth he thank that servant, for doing the things which he commanded him?
Je, huyo mtu atamshukuru mtumishi huyo kwa kutimiza yale aliyoamriwa?
10 I think not. So you also, when you shall have done all these things that are commanded you, say: We are unprofitable servants; we have done that which we ought to do.
Vivyo hivyo nanyi mkiisha kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi tu watumishi tusiostahili; tumefanya tu yale tuliyopaswa kufanya.’”
11 And it came to pass, as he was going to Jerusalem, he passed through the midst of Samaria and Galilee.
Yesu alipokuwa njiani akienda Yerusalemu, alipitia mpakani mwa Samaria na Galilaya.
12 And as he entered into a certain town, there met him ten men that were lepers, who stood afar off;
Alipokuwa akiingia kwenye kijiji kimoja, watu kumi waliokuwa na ukoma wakakutana naye. Wakasimama mbali,
13 And lifted up their voice, saying: Jesus, master, have mercy on us.
wakapaza sauti, wakasema, “Yesu, Bwana, tuhurumie!”
14 Whom when he saw, he said: Go, shew yourselves to the priests. And it came to pass, as they went, they were made clean.
Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Nao walipokuwa njiani wakienda, wakatakasika.
15 And one of them, when he saw that he was made clean, went back, with a loud voice glorifying God.
Mmoja wao alipoona kwamba amepona, akarudi kwa Yesu, akimsifu Mungu kwa sauti kuu.
16 And he fell on his face before his feet, giving thanks: and this was a Samaritan.
Akajitupa miguuni mwa Yesu akamshukuru. Yeye alikuwa Msamaria.
17 And Jesus answering, said, Were not ten made clean? and where are the nine?
Yesu akauliza, “Je, hawakutakaswa wote kumi? Wako wapi wale wengine tisa?
18 There is no one found to return and give glory to God, but this stranger.
Hakuna hata mmoja aliyeonekana kurudi ili kumshukuru Mungu isipokuwa huyu mgeni?”
19 And he said to him: Arise, go thy way; for thy faith hath made thee whole.
Yesu akamwambia, “Inuka na uende zako, imani yako imekuponya.”
20 And being asked by the Pharisees, when the kingdom of God should come? he answered them, and said: The kingdom of God cometh not with observation:
Yesu alipoulizwa na Mafarisayo Ufalme wa Mungu utakuja lini, yeye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuchunguza kwa bidii,
21 Neither shall they say: Behold here, or behold there. For lo, the kingdom of God is within you.
wala watu hawatasema, ‘Huu hapa,’ au ‘Ule kule,’ kwa maana Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.”
22 And he said to his disciples: The days will come, when you shall desire to see one day of the Son of man; and you shall not see it.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Wakati utafika ambapo mtatamani kuiona moja ya siku ya Mwana wa Adamu, lakini hamtaiona.
23 And they will say to you: See here, and see there. Go ye not after, nor follow them:
Watu watawaambia, ‘Yule kule!’ Au, ‘Huyu hapa!’ Msiwakimbilie.
24 For as the lightening that lighteneth from under heaven, shineth unto the parts that are under heaven, so shall the Son of man be in his day.
Kwa maana kama vile umeme wa radi umulikavyo katika anga kuanzia mwisho mmoja hadi mwingine, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.
25 But first he must suffer many things, and be rejected by this generation.
Lakini kwanza itampasa kuteseka katika mambo mengi na kukataliwa na kizazi hiki.
26 And as it came to pass in the days of Noe, so shall it be also in the days of the Son of man.
“Kama ilivyokuwa siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Adamu.
27 They did eat and drink, they married wives, and were given in marriage, until the day that Noe entered into the ark: and the flood came and destroyed them all.
Watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina. Ndipo gharika ikaja na kuwaangamiza wote.
28 Likewise as it came to pass, in the days of Lot: they did eat and drink, they bought and sold, they planted and built.
“Ndivyo ilivyokuwa katika siku za Loti: Watu walikuwa wakila na kunywa, wakinunua na kuuza, wakilima na kujenga.
29 And in the day that Lot went out of Sodom, it rained fire and brimstone from heaven, and destroyed them all.
Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, ikanyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni ukawaangamiza wote.
30 Even thus shall it be in the day when the Son of man shall be revealed.
“Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Adamu atakapofunuliwa.
31 In that hour, he that shall be on the housetop, and his goods in the house, let him not go down to take them away: and he that shall be in the field, in like manner, let him not return back.
Siku hiyo, mtu yeyote aliye juu ya dari ya nyumba yake, hata vitu vyake vikiwa ndani ya hiyo nyumba, asishuke kuvichukua. Vivyo hivyo mtu aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua chochote.
32 Remember Lot’s wife.
Mkumbukeni mke wa Loti!
33 Whosoever shall seek to save his life, shall lose it: and whosoever shall lose it, shall preserve it.
Mtu yeyote anayejaribu kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayeyapoteza maisha yake atayaokoa.
34 I say to you: in that night there shall be two men in one bed; the one shall be taken, and the other shall be left.
Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa wamelala kitanda kimoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
35 Two women shall be grinding together: the one shall be taken, and the other shall be left: two men shall be in the field; the one shall be taken, and the other shall be keft.
Wanawake wawili watakuwa wanasaga nafaka pamoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa. [
36 They answering, say to him: Where, Lord?
Wanaume wawili watakuwa wanafanya kazi pamoja shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.]”
37 Who said to them: Wheresoever the body shall be, thither will the eagles also be gathered together.
Kisha wakamuuliza, “Haya yatatukia wapi Bwana?” Akawaambia, “Pale ulipo mzoga, huko ndiko tai watakapokusanyika.”

< Luke 17 >