< Joshua 17 >

1 And this lot fell to the tribe of Manasses (for he is the firstborn of Joseph) to Machir the firstborn of Manasses the father of Galaad, who was a warlike man, and had for possession Galaad and Basan.
Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
2 And to the rest of the children of Manasses according to their families: to the children of Abiezer, and to the children of Helec, and to the children of Esriel, and to the children of Sechem, and to the children of Hepher, and to the children of Semida: these are the male children of Manasses the son of Joseph, by their kindreds.
Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
3 But Salphaad the son of Hepher the son of Galaad the son of Machir the son of Manasses had no sons, but only daughters: whose names are these, Maala and Noa and Hegla and Melcha and Thersa.
Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
4 And they came in the presence of Eleazar the priest and of Josue the son of Nun, and of the princes, saying: The Lord commanded by the hand of Moses, that a possession should be given us in the midst of our brethren. And he gave them according to the commandment of the Lord a possession amongst the brethren of their father.
Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
5 And there fell ten portions to Manasses, beside the land of Galaad and Basan beyond the Jordan.
Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
6 For the daughters of Manasses possessed inheritance in the midst of his sons. And the land of Galaad fell to the lot of the rest of the children of Manasses.
kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
7 And the border of Manasses was from Aser, Machmethath which looketh towards Sichem: and it goeth out on the right hand by the inhabitants of the fountain of Taphua.
Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
8 For the lot of Manasses took in the land of Taphua, which is on the borders of Manasses, and belongs to the children of Ephraim.
(Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
9 And the border goeth down to the valley of the reeds, to the south of the torrent of the cities of Ephraim, which are in the midst of the cities of Manasses: the border of Manasses is on the north side of the torrent, and the outgoings of it are at the sea:
Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
10 So that the possession of Ephraim is on the south, and on the north that of Manasses, and the sea is the border of both, and they are joined together in the tribe of Aser on the north, and in the tribe of Issachar on the east.
Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
11 And the inheritance of Manasses in Issachar and in Aser, was Bethsan and its villages, and Jeblaam with its villages, and the inhabitants of Dor, with the towns thereof: the inhabitants also of Endor with the villages thereof: and in like manner the inhabitants of Thenac with the villages thereof: and the inhabitants of Mageddo with their villages, and the third part of the city of Nopheth.
Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
12 Neither could the children of Manasses overthrow these cities, but the Chanaanite began to dwell in his land.
Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
13 But after that the children of Israel were grown strong, they subdued the Chanaanites, and made them their tributaries, and they did not kill them.
Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
14 And the children of Joseph spoke to Josue, and said: Why hast thou given me but one lot and one portion to possess, whereas I am of so great a multitude, and the Lord hath blessed me?
Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
15 And Josue said to them: If thou be a great people, go up into the woodland, and cut down room for thyself in the land of the Pherezite and the Raphaims: because the possession of mount Ephraim is too narrow for thee.
Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
16 And the children of Joseph answered him: We cannot go up to the mountains, for the Chanaanites that dwell in the low lands, wherein are situate Bethsan with its towns, and Jezrael in the midst of the valley, have chariots of iron.
Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
17 And Josue said to the house of Joseph, to Ephraim and Manasses: Thou art a great people, and of great strength, thou shalt not have one lot only:
Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
18 But thou shalt pass to the mountain, and shalt cut down the wood, and make thyself room to dwell in: and mayst proceed farther, when thou hast destroyed the Chanaanites, who as thou sayest have iron chariots, and are very strong.
bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”

< Joshua 17 >