< John 2 >

1 And the third day, there was a marriage in Cana of Galilee: and the mother of Jesus was there.
Baada ya siku tatu, kulikuwa na arusi huko Kana ya Galilaya na mama yake Yesu alikuwa huko.
2 And Jesus also was invited, and his disciples, to the marriage.
Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa katika arusi.
3 And the wine failing, the mother of Jesus saith to him: They have no wine.
Wakati walipoishiwa na divai, mama yake Yesu akamwambia, “Hawana divai.”
4 And Jesus saith to her: Woman, what is that to me and to thee? my hour is not yet come.
Yesu akajibu, “Mwanamke hiyo inanihusu nini mimi? Muda wangu mimi bado haujatimia.”
5 His mother saith to the waiters: Whatsoever he shall say to you, do ye.
Mama yake akawambia watumishi, “Chochote atakachowambia fanyeni.”
6 Now there were set there six waterpots of stone, according to the manner of the purifying of the Jews, containing two or three measures apiece.
Basi kulikuwa na mitungi sita ya mawe pale iliyowekwa kwa ajili ya kunawa katika sikukuu za Wayahudi, kila moja lilikuwa na ujazo wa nzio mbili tatu.
7 Jesus saith to them: Fill the waterpots with water. And they filled them up to the brim.
Yesu akawambia, “Ijazeni maji mitungi ya mawe.” Wakajaza hadi juu.
8 And Jesus saith to them: Draw out now, and carry to the chief steward of the feast. And they carried it.
Kisha akawambia wale watumishi, “Chukueni kiasi sasa na mpeleke kwa muhudumu mkuu wa meza.” Wakafanya kama walivyoagizwa.
9 And when the chief steward had tasted the water made wine, and knew not whence it was, but the waiters knew who had drawn the water; the chief steward calleth the bridegroom,
Mhudumu mkuu aliyaonja yale maji yaliyokuwa yamebadilika na kuwa divai, ila hakujua yalikotoka (lakini watumishi waliochota maji walijua yalikotoka). Kisha akamwita bwana harusi na
10 And saith to him: Every man at first setteth forth good wine, and when men have well drunk, then that which is worse. But thou hast kept the good wine until now.
kumwambia, “Kila mmoja huanza kuwahudumia watu divai nzuri na wakiishalewa huwapa divai isiyo nzuri. Lakini wewe umeitunza divai nzuri hadi sasa”
11 This beginning of miracles did Jesus in Cana of Galilee; and manifested his glory, and his disciples believed in him.
Muujiza huu wa Kana ya Galilaya, ulikuwa ndio mwanzo wa ishara za miujiza aliyoifanya Yesu, akifunua utukufu wake, hivyo wanafunzi wake wakamwamini.
12 After this he went down to Capharnaum, he and his mother, and his brethren, and his disciples: and they remained there not many days.
Baada ya hii, Yesu, mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake walienda katika mji wa Kapernaum na wakaa huko kwa siku chache.
13 And the pasch of the Jews was at hand, and Jesus went up to Jerusalem.
Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
14 And he found in the temple them that sold oxen and sheep and doves, and the changers of money sitting.
Akawakuta wauzaji wa ng'ombe, kondoo, na njiwa ndani ya Hekalu. Pia na wabadilisha fedha walikuwa wameketi ndani ya Hekalu.
15 And when he had made, as it were, a scourge of little cords, he drove them all out of the temple, the sheep also and the oxen, and the money of the changers he poured out, and the tables he overthrew.
Yesu akatengeneza mjeledi wenye vifundo, akawatoa wote walikuwemo katika hekalu, ikijumuisha ng'ombe na kondoo. Akamwaga fedha za wabadili fedha na kuzipindua meza zao.
16 And to them that sold doves he said: Take these things hence, and make not the house of my Father a house of traffic.
Kwa wauzaji wa njiwa akawambia, “Toeni vitu hivi mbali na mahali hapa, acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa soko.”
17 And his disciples remembered, that it was written: The zeal of thy house hath eaten me up.
Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa ilikuwa imeandikwa, “Wivu wa nyumba yako utanila.”
18 The Jews, therefore, answered, and said to him: What sign dost thou shew unto us, seeing thou dost these things?
Wakuu wa Kiyahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara ipi utakayoionyesha kwa sababu unayafanya mambo haya?”
19 Jesus answered, and said to them: Destroy this temple, and in three days I will raise it up.
Yesu akawajibu, libomoeni Hekalu hili nami nitalijenga baada ya siku tatu.”
20 The Jews then said: Six and forty years was this temple in building; and wilt thou raise it up in three days?
Kisha wakuu wa Wayahudi wakasema, “Iligharimu miaka arobaini na sita kujenga hekalu hili nawe unasema utalijenga kwa siku tatu?”
21 But he spoke of the temple of his body.
Ingawa, yeye aliongea hekalu akimaanisha mwili wake.
22 When therefore he was risen again from the dead, his disciples remembered, that he had said this, and they believed the scripture, and the word that Jesus had said.
Hivyo baadaye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka kuwa alisema hivyo, wakaamini maandiko na kauli hii ambayo Yesu alikuwa amekwisha kuisema.
23 Now when he was at Jerusalem, at the pasch, upon the festival day, many believed in his name, seeing his signs which he did.
Basi alipokuwa Yerusalemu wakati wa Pasaka, wakati wa sikukuu watu wengi waliamini jina lake, walipoona ishara ya miujiza aliyoifanya.
24 But Jesus did not trust himself unto them, for that he knew all men,
Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
25 And because he needed not that any should give testimony of man: for he knew what was in man.
Hakuhitaji mtu yeyote kumwambia kuhusu walivyo wanadamu kwa sababu alijua kilichokuwamo ndani yao.

< John 2 >