< Job 40 >

1 And the Lord went on, and said to Job:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Shall he that contendeth with God be so easily silenced? surely he that reproveth God, ought to answer him.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Then Job answered the Lord, and said:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 What can I answer, who hath spoken inconsiderately? I will lay my hand upon my mouth.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 One thing I have spoken, which I wish I had not said: and another, to which I will add no more.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 And the Lord answering Job out of the whirlwind, said:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Gird up thy loins like a man: I will ask thee, and do thou tell me.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Wilt thou make void my judgment: and condemn me, that thou mayst be justified?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 And hast thou an arm like God, and canst thou thunder with a voice like him?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Clothe thyself with beauty, and set thyself up on high and be glorious, and put on goodly garments.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Scatter the proud in thy indignation, and behold every arrogant man, and humble him.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Look on all that are proud, and confound them, and crush the wicked in their place.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Hide them in the dust together, and plunge their faces into the pit.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Then I will confess that thy right hand is able to save thee.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Behold behemoth whom I made with thee, he eateth grass like an ox.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 His strength is in his loins, and his force in the navel of his belly.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 He setteth up his tail like a cedar, the sinews of his testicles are wrapped together.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 His bones are like pipes of brass, his gristle like plates of iron.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 He is the beginning of the ways of God, who made him, he will apply his sword.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 To him the mountains bring forth grass: there all the beasts of the field shall play.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 He sleepeth under the shadow, in the covert of the reed, and in moist places.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 The shades cover his shadow, the willows of the brook shall compass him about.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Behold, he will drink up a river, and not wonder: and he trusteth that the Jordan may run into his mouth.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 In his eyes as with a hook he shall take him, and bore through his nostrils with stakes.
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >