< Job 34 >

1 And Eliu continued his discourse, and said:
Kisha Elihu akasema:
2 Hear ye, wise men, my words, and ye learned, hearken to me:
“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
3 For the ear trieth words, and the mouth discerneth meats by the taste.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
4 Let us choose to us judgment, and let us see among ourselves what is the best.
Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
5 For Job hath said: I am just, and God hath overthrown my judgment.
“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
6 For in judging me there is a lie: my arrow is violent without any sin.
Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
7 What man is there like Job, who drinketh up scorning like water?
Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
8 Who goeth in company with them that work iniquity, and walketh with wicked men?
Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
9 For he hath said: Man shall not please God, although he run with him.
Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
10 Therefore, ye men of understanding, hear me: far from god be wickedness, and iniquity from the Almighty.
“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
11 For he will render to a man his work, and according to the ways of every one he will reward them.
Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
12 For in very deed God will not condemn without cause, neither will the Almighty pervert judgment.
Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
13 What other hath he appointed over the earth? or whom hath he set over the world which he made?
Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
14 If he turn his heart to him, he shall draw his spirit and breath unto himself.
Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
15 All flesh shall perish together, and man shall return into ashes.
wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
16 If then thou hast understanding, hear what is said, and hearken to the voice of my words.
“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
17 Can he be healed that loveth not judgment? and how dost thou so far condemn him that is just?
Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
18 Who saith to the king: Thou art an apostate: who calleth rulers ungodly?
Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
19 Who accepteth not the persons of princes: nor hath regarded the tyrant, when he contended against the poor man: for all are the work of his hands.
yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
20 They shall suddenly die, and the people shall be troubled at midnight, and they shall pass, and take away the violent without hand.
Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
21 For his eyes are upon the ways of men, and he considereth all their steps.
“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
22 There is no darkness, and there is no shadow of death, where they may be hid who work iniquity.
Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
23 For it is no longer in the power of man to enter into judgment with God.
Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
24 He shall break in pieces many and innumerable, and shall make others to stand in their stead.
Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
25 For he knoweth their works: and therefore he shall bring night on them, and they shall be destroyed.
Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
26 He hath struck them, as being wicked, in open sight.
Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
27 Who as it were on purpose have revolted from him, and would not understand all his ways:
kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
28 So that they caused the cry of the needy to come to him, and he heard the voice of the poor.
Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
29 For when he granteth peace, who is there that can condemn? When he hideth his countenance, who is there that can behold him, whether it regard nations, or all men?
Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
30 Who maketh a man that is a hypocrite to reign for the sins of the people?
ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
31 Seeing then I have spoken of God, I will not hinder thee in thy turn.
“Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
32 If I have erred, teach thou me: if I have spoken iniquity, I will add no more.
Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
33 Doth God require it of thee, because it hath displeased thee? for thou begannest to speak, and not I: but if thou know any thing better, speak.
Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
34 Let men of understanding speak to me, and let a wise man hearken to me.
“Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
35 But Job hath spoken foolishly, and his words sound not discipline.
‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
36 My father, let Job be tried even to the end: cease not from the man of iniquity.
Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
37 Because he addeth blasphemy upon his sins, let him be tied fast in the mean time amongst us: and then let him provoke God to judgment with his speeches.
Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”

< Job 34 >