< Job 31 >

1 I made a covenant with my eyes, that I would not so much as think upon a virgin.
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 For what part should God from above have in me, and what inheritance the Almighty from on high?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Is not destruction to the wicked, and aversion to them that work iniquity?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Doth not he consider my ways, and number all my steps?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 If I have walked in vanity, and my foot hath made haste to deceit:
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 Let him weigh me in a just balance, and let God know my simplicity.
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 If my step hath turned out of the way, and if my heart hath followed my eyes, and if a spot hath cleaved to my hands:
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 Then let me sow and let another eat: and let my offspring be rooted out.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 If my heart hath been deceived upon a woman, and if I have laid wait at my friend’s door:
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 Let my wife be the harlot of another, and let other men lie with her.
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 For this is a heinous crime, and a most grievous iniquity.
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 It is a fire that devoureth even to destruction, and rooteth up all things that spring.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 If I have despised to abide judgment with my manservant, or my maidservant, when they had any controversy against me:
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 For what shall I do when God shall rise to judge? and when he shall examine, what shall I answer him?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Did not he that made me in the womb make him also: and did not one and the same form me in the womb?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 If I have denied to the poor what they desired, and have made the eyes of the widow wait:
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 If I have eaten my morsel alone, and the fatherless hath not eaten thereof:
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 (For from my infancy mercy grew up with me: and it came out with me from my mother’s womb: )
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 If I have despised him that was perishing for want of clothing, and the poor man that had no covering:
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 If his sides have not blessed me, and if he were not warmed with the fleece of my sheep:
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 If I have lifted up my hand against the fatherless, even when I saw myself superior in the gate:
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 Let my shoulder fall from its joint, and let my arm with its bones be broken.
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 For I have always feared God as waves swelling over me, and his weight I was not able to bear.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 If I have thought gold my strength, and have said to fine gold: My confidence:
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 If I have rejoiced over my great riches, and because my hand had gotten much.
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 If I beheld the sun when it shined, and the moon going in brightness:
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 And my heart in secret hath rejoiced, and I have kissed my hand with my mouth:
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 Which is a very great iniquity, and a denial against the most high God.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 If I have been glad at the downfall of him that hated me, and have rejoiced that evil had found him.
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 For I have not given my mouth to sin, by wishing a curse to his soul.
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 If the men of my tabernacle have not said: Who will give us of his flesh that we may be filled?
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 The stranger did not stay without, my door was open to the traveller.
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 If as a man I have hid my sin, and have concealed my iniquity in my bosom.
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 If I have been afraid at a very great multitude, and the contempt of kinsmen hath terrified me: and I have not rather held my peace, and not gone out of the door.
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 Who would grant me a hearer, that the Almighty may hear my desire; and that he himself that judgeth would write a book,
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 That I may carry it on my shoulder, and put it about me as a crown?
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 At every step of mine I would pronounce it, and offer it as to a prince.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 If my land cry against me, and with it the furrows thereof mourn:
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 If I have eaten the fruits thereof without money, and have afflicted the soul of the tillers thereof:
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 Let thistles grow up to me instead of wheat, and thorns instead of barley.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.

< Job 31 >