< Jeremiah 32 >

1 The word that came to Jeremias from the Lord in the tenth year of Sedecias king of Juda: the same is eighteenth year of Nabuchodonosor.
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, katika mwaka wa kumi wa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Nebukadneza.
2 At that time the army of the king o Babylon besieged Jerusalem: and Jeremias the prophet was shut up in the court of the prison, which was in the house of the king of Juda.
Wakati huo jeshi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka mji wa Yerusalemu, naye nabii Yeremia alikuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi katika jumba la kifalme la Yuda.
3 For Sedecias king of Juda had shut him up, saying: Why dost thou prophesy, saying: Thus saith the Lord: Behold I will give this city into the hand of the king of Babylon, and he shall take it?
Basi Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga huko akisema, “Kwa nini unatabiri hivyo? Wewe unasema, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteka.
4 And Sedecias king of Juda shall not escape out of the hand of the Chaldeans: but he shall be delivered into the hands of the king of Babylon: and he shall speak to him mouth to mouth, and his eyes shall see his eyes.
Sedekia mfalme wa Yuda hataweza kuponyoka mikononi mwa Wakaldayo, lakini kwa hakika atatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atazungumza naye ana kwa ana na kumwona kwa macho yake mwenyewe.
5 And he shall lead Sedecias to Babylon: and he shall be there till I visit him, saith the Lord. But if you will fight against the Chaldeans, you shall have no success.
Atamchukua Sedekia hadi Babeli, mahali atakapoishi mpaka nitakapomshughulikia, asema Bwana. Kama utapigana dhidi ya Wakaldayo, hutashinda.’”
6 And Jeremias said: The word of the Lord came to me, saying:
Yeremia akasema, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
7 Behold, Hanameel the son of Sellum thy cousin shall come to thee, saying: Buy thee my field, which is in Anathoth, for it is thy right to buy it, being akin.
Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako atakuja kwako na kusema, ‘Nunua shamba langu huko Anathothi, kwa sababu wewe kama jamaa ya karibu ni haki na wajibu wako kulinunua.’
8 And Hanameel my uncle’s son cam to me, according to the word of the to the entry of the prison, and said me: Buy my held, which is in in the land of Benjamin: for the right of inheritance is thins, and thou art next of kin to possess it. And I understood this was the word of the Lord.
“Kisha, kama Bwana alivyosema, binamu yangu Hanameli alinijia katika ua wa walinzi na kusema: ‘Nunua shamba langu lililoko Anathothi katika nchi ya Benyamini. Kwa kuwa ni haki yako kulikomboa na kulimiliki, jinunulie.’ “Nilijua kwamba hili lilikuwa neno la Bwana.
9 And I bought the held of my uncle’s son, that is in Anathoth: and I weighed him the money, seven staters, and ten pieces of silver.
Hivyo nikalinunua shamba hilo lililoko Anathothi kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nami nikampimia shekeli kumi na saba za fedha.
10 And I wrote it in a book and sealed it, and took witnesses: and I weighed him the money in the balances.
Nikatia sahihi na kuweka muhuri hati ya kumiliki, nikaweka mashahidi, na kupima ile fedha kwenye mizani.
11 And I took the deed of the purchase that was sealed, and the stipulations, and the ratifications with the seals that were on the outside.
Nikachukua ile hati ya kununulia, nakala iliyotiwa muhuri yenye makubaliano na masharti, pia pamoja na ile nakala isiyo na muhuri,
12 And I gave the deed of the purchase to Baruch the son of Neri the son of Maasias in the sight of Hanameel my uncle’s son, in the presence of the witnesses that subscribed the book of the purchase, and before all the Jews that sat in the court of the prison.
nami nikampa Baruku mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, hati hii mbele ya binamu yangu Hanameli, na mbele ya mashahidi waliokuwa wameweka sahihi kwenye hati hii na mbele ya Wayahudi wote waliokuwa wameketi katika ua wa walinzi.
13 And I charged Baruch before them, saying:
“Nilimpa Baruku maelezo haya mbele yao:
14 Thus saith the Lord of hosts the God of Israel: Take these writings, this deed of the purchase that is sealed up, and this deed that is open: and put them in an earthen vessel, that they may continue many days.
‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Chukua hati hizi, yaani nakala zote zenye muhuri na zisizo na muhuri za hati ya kununulia, na uziweke kwenye gudulia la udongo wa mfinyanzi ili zidumu kwa muda mrefu.
15 For thus saith the Lord of hosts the God of Israel: Houses, and fields, and vineyards shall be possessed again in this land.
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nyumba, mashamba na mashamba ya mizabibu yatanunuliwa tena katika nchi hii.’
16 And after I had delivered the deed of purchase to Baruch the son of Neri, I prayed to the Lord, saying:
“Baada ya kumkabidhi Baruku mwana wa Neria hii hati ya kununulia, nilimwomba Bwana:
17 Alas, alas, alas, O Lord God, behold thou hast made heaven and earth by thy great power, and thy stretched out arm: no word shall be hard to thee:
“Ee Bwana Mwenyezi, umeumba mbingu na nchi kwa uwezo wako mkuu na kwa mkono ulionyooshwa. Hakuna jambo lililo gumu usiloliweza.
18 Thou shewest mercy unto thousands, and returnest the iniquity of the fathers into the bosom of their children after them: O most mighty, great, and powerful, the Lord of hosts is thy name.
Wewe huonyesha upendo kwa maelfu, lakini huleta adhabu kwa ajili ya dhambi za baba mapajani mwa watoto wao baada yao. Ee Mungu mkuu na mwenye uweza, ambaye jina lako ni Bwana Mwenye Nguvu Zote,
19 Great in counsel and incomprehensible in thought: whose eyes are open upon all the ways of the children of Adam, to render unto every one according to his ways, and according to the fruit of his devices.
makusudi yako ni makuu, na matendo yako ni yenye uwezo. Macho yako yanaona njia zote za wanadamu, nawe humlipa kila mmoja kulingana na mwenendo wake, na kama yanavyostahili matendo yake.
20 Who hast set signs and wonders in the land of Egypt even until this day, and in Israel, and amongst men, and hast made thee a name as at this day.
Ulitenda ishara za miujiza na maajabu huko Misri, na umeyaendeleza mpaka leo, katika Israeli na miongoni mwa wanadamu wote, nawe umejulikana na kufahamika hivyo mpaka leo.
21 And hast brought forth thy people Israel, out of the land of Egypt with signs, and with wonders, and with a strong hand, and a stretched out arm, and with great terror.
Uliwatoa watu wako Israeli kutoka Misri kwa ishara na maajabu, kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa na kwa matisho makuu.
22 And best given them this land which thou didst swear to their fathers, to give them a land flowing with milk and honey.
Uliwapa nchi hii uliyokuwa umeapa kuwapa baba zao, nchi inayotiririka maziwa na asali.
23 And they came in, and possessed it: but they obeyed not thy voice, and they walked not in thy law: and they did not any of those things that thou didst command them to do, and all these evils are come upon them.
Waliingia na kuimiliki, lakini hawakukutii wala kuifuata sheria yako. Hawakufanya kile ulichowaamuru kufanya. Hivyo ukaleta maafa haya yote juu yao.
24 Behold works are built up against the city to take it: and the city is given into the hands of the Chaldeans, who fight against it, by the sword, and the famine, and the pestilence: and what thou hast spoken, is all come to pass, as thou thyself seest.
“Tazama jinsi tumezungukwa na jeshi ili kuuteka mji huu. Kwa sababu ya upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo ambao wanaushambulia. Ulilosema limetokea kama vile unavyoona sasa.
25 And sayest thou to me, O Lord God: Buy a field for money, and take witnesses, whereas the city is given into the hands of the Chaldeans?
Ingawa mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo, wewe, Ee Bwana Mwenyezi, uliniambia, ‘Nunua shamba kwa fedha, na jambo hilo lishuhudiwe.’”
26 And the word of the Lord came to Jeremias, saying:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
27 Behold I am the Lord the God of all flesh: shall any thing be hard for me?
“Mimi ndimi Bwana, Mungu wa wote wenye mwili. Je, kuna jambo lolote lililo gumu nisiloliweza?
28 Therefore thus saith the Lord: Behold I will deliver this city into the hands of the Chaldeans, and into the hands of the king of Babylon, and they shall take it.
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa Wakaldayo, na mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ambaye atauteka.
29 And the Chaldeans that fight against this city, shall come and set it on fire, and burn it, with the houses upon whose roofs they offered sacrifice to Baal, and poured out drink offerings to strange gods, to provoke me to wrath.
Wakaldayo ambao wanaushambulia mji huu watakuja na kuuchoma moto na kuuteketeza, pamoja na nyumba ambamo watu wamenikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba katika mapaa na kumimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine.
30 For the children of Israel, and the children of Juda, have continually done evil in my eyes from their youth: the children of Israel who even till now provoke me with the work of their hands, saith the Lord.
“Watu wa Israeli na wa Yuda hawakufanya kitu kingine ila uovu mbele zangu tangu ujana wao. Naam, watu wa Israeli hawakufanya kitu kingine ila kunikasirisha kwa kazi ambazo mikono yao imetengeneza, asema Bwana.
31 For this city hath been to me a provocation and indignation from the day that they built it, until this day, in which it shall be taken out of my sight.
Tangu siku ulipojengwa hadi sasa, mji huu umenikasirisha na kunighadhibisha kiasi kwamba ni lazima niuondoe machoni pangu.
32 Because of all the evil of the children of Israel, and of the children of Juda, which they have done, provoking me to wrath, they and their kings, their princes, and their priests, and their prophets, the men of Juda, and the inhabitants of Jerusalem.
Watu wa Israeli na wa Yuda wamenikasirisha kwa uovu wote waliofanya: wao, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao, watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu.
33 And they have turned their backs to me, and not their faces: when I taught them early in the morning, and instructed them, and they would not hearken to receive instruction.
Walinigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao. Ingawa niliwafundisha tena na tena, hawakupenda kusikiliza wala kuitikia adhabu.
34 And they have set their idols in the house, in which my name is called upon, to defile it.
Waliweka miungu yao ya kuchukiza sana katika nyumba iitwayo kwa Jina langu na kuinajisi.
35 And they have built the high places of Baal, which are in the valley of the son of Ennom, to consecrate their sons and their daughters to Moloch: which I commanded them not, neither entered it into my heart, that they should do this abomination, and cause Juda to sin.
Wakajenga mahali pa juu pa kuabudia miungu kwa ajili ya Baali katika Bonde la Ben-Hinomu, ambapo walitoa wana wao na binti zao kafara kwa Moleki, ingawa kamwe sikuamuru, wala halikuingia akilini mwangu, kwamba watafanya chukizo kama hilo na kumfanya Yuda atende dhambi.
36 And now, therefore, thus saith the Lord the God of Israel to this city, whereof you say that it shall be delivered into the hands of the king of Babylon by the sword, and by famine, and by pestilence:
“Mnasema kuhusu mji huu, ‘Kwa upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mkononi mwa mfalme wa Babeli,’ lakini hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli asemalo:
37 Behold I will gather them together out of all the lands to which I have cast them out in my anger, and in my wrath, and in my great indignation: and I will bring them again into this place, and will cause them to dwell securely.
Hakika nitawakusanya kutoka nchi zote nilizowafukuzia katika hasira yangu kali na ghadhabu yangu kuu, nitawarudisha mahali hapa na kuwaruhusu waishi kwa salama.
38 And they shall be my people, and I will be their God.
Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.
39 And I will give them one heart, and one way, that they may fear me all days: and that it may be well with them, and with their children after them.
Nitawapa moyo mmoja na kutenda pamoja, ili kwamba waniche daima kwa mema yao wenyewe na kwa mema ya watoto wao baada yao.
40 And I will make an everlasting covenant with them, and will not cease to do them good: and I will give my fear in their heart, that they may not revolt from me.
Nitafanya nao agano la milele: Kamwe sitaacha kuwatendea mema, nami nitawavuvia kunicha mimi, ili kamwe wasigeukie mbali nami.
41 And I will rejoice over them, when I shall do them good: and I will plant them in this land in truth, with my whole heart, and with all my soul.
Nitafurahia kuwatendea mema, na kwa hakika nitawapanda katika nchi hii kwa moyo wangu wote na roho yangu yote.
42 For thus saith the Lord: As I have brought upon this people all this great evil: so will I bring upon them all the good that I now speak to them.
“Hili ndilo asemalo Bwana: Kama nilivyoleta maafa haya makubwa kwa watu hawa, ndivyo nitakavyowapa mafanikio niliyowaahidi.
43 And fields shall be purchased in this land: whereof you say that it is desolate, because there remaineth neither man nor beast, and it is given into the hands of the Chaldeans.
Kwa mara nyingine tena mashamba yatanunuliwa katika nchi hii ambayo mlisema, ‘Imekuwa ukiwa, isiyofaa, isiyo na watu wala wanyama, kwa sababu imetiwa mikononi mwa Wakaldayo.’
44 Fields shall be bought for money, and deeds shall be written, and sealed, and witnesses shall be taken, in the land of Benjamin, and round about Jerusalem, in the cities of Juda, and in the cities on the mountains, and in the cities of the plains, and in the cities that are towards the south: for I will bring their captivity, saith the Lord.
Mashamba yatanunuliwa kwa fedha, na hati zitatiwa sahihi, zitatiwa muhuri na kushuhudiwa katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, katika miji ya Yuda na katika miji ya nchi ya vilima, sehemu za magharibi katika miji ya tambarare na katika Negebu, kwa sababu nitarudisha tena mafanikio yao, asema Bwana.”

< Jeremiah 32 >