< Jeremiah 12 >

1 Thou indeed, O Lord, art just, if I plead with thee, but yet I will speak what is just to thee: Why doth the way of the wicked prosper: why is it well with all them that transgress, and do wickedly?
Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana, niletapo mashtaka mbele yako. Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako: Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa? Kwa nini wasio waaminifu wote wanaishi kwa raha?
2 Thou hast planted them, and they have taken root: they prosper and bring forth fruit: thou art near in their mouth, and far from their reins.
Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.
3 And thou, O Lord, hast known me, thou hast seen me, and proved my heart with thee: gather them together as sheep for a sacrifice, and prepare them for the day of slaughter.
Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana; unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe. Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa! Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!
4 How long shall the land mourn, and the herb of every field wither for the wickedness of them that dwell therein? The beasts and the birds are consumed: because they have said: He shall not see our last end.
Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini, na majani katika kila shamba kunyauka? Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu, wanyama na ndege wameangamia. Zaidi ya hayo, watu wanasema, “Bwana hataona yatakayotupata sisi.”
5 If thou hast wearied with running with footmen, how canst thou contend with horses? and if thou hast been secure in a land of peace, what wilt thou do in the swelling of the Jordan?
“Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda, unawezaje kushindana na farasi? Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama, utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?
6 For even thy brethren, and the house of thy father, even they have fought against thee, and have cried after thee with full voice: believe them not when they speak good things to thee.
Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe: hata wao wamekusaliti; wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini, ingawa wanazungumza mema juu yako.
7 I have forsaken my house, I have left my inheritance: I have given my dear soul into the land of her enemies.
“Nitaiacha nyumba yangu, nitupe urithi wangu; nitamtia yeye nimpendaye mikononi mwa adui zake.
8 My inheritance is become to me as a lion in the wood: is hath cried out against me, therefore have I hated it.
Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba wa msituni. Huningurumia mimi, kwa hiyo ninamchukia.
9 Is my inheritance to me as a speckled bird? Is it as a bird died throughout? come ye, assemble yourselves, all the beasts of the earth, make haste to devour.
Je, urithi wangu haukuwa kama ndege wa mawindo wa madoadoa ambaye ndege wengine wawindao humzunguka na kumshambulia? Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni; walete ili wale.
10 Many pastors have destroyed my vineyard, they have trodden my portion under foot: they have changed my delightful portion into a desolate wilderness.
Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu na kulikanyaga shamba langu; watalifanya shamba langu zuri kuwa jangwa la ukiwa.
11 They have laid it waste, and it hath mourned for me. With desolation is all the land made desolate; because there is none that considereth in the heart.
Litafanywa kuwa jangwa, lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu; nchi yote itafanywa jangwa kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.
12 The spoilers are come upon all the ways of the wilderness, for the sword of the Lord shall devour from one end of the land to the other end thereof: there is no peace for all flesh.
Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani mharabu atajaa, kwa maana upanga wa Bwana utawala, kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine; hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.
13 They have sown wheat, and reaped thorns: they have received an inheritance, and it shall not profit them: you shall be ashamed of your fruits, because of the fierce wrath of the Lord.
Watapanda ngano lakini watavuna miiba; watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote. Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”
14 Thus saith the Lord against all my wicked neighbors, that touch the inheritance that I have shared out to my people Israel: Behold I will pluck them out of their land, and I will pluck the house of Juda out of the midst of them.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao.
15 And when I shall have plucked them out, I will return, and have mercy on them: and I will bring them back, every man to his inheritance, and every man to his land.
Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe.
16 And it shall come to pass, if they will be taught, and will learn the ways of my people, to swear by my name: The Lord liveth, as they have taught my people to swear by baal: that they shall be built up in the midst of my people.
Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu.
17 But if they will not hear, I will utterly pluck out and destroy that nation, saith the Lord.
Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.

< Jeremiah 12 >