< Habakkuk 3 >

1 A PRAYER OF HABACUC THE PROPHET FOR IGNORANCES.
Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.
2 O Lord, I have heard thy hearing, and was afraid. O Lord, thy work, in the midst of the years bring it to life: In the midst of the years thou shalt make it known: when thou art angry, thou wilt remember mercy.
Bwana, nimezisikia sifa zako; nami naogopa kwa matendo yako, Ee Bwana. Fufua kazi yako katikati ya miaka, katikati ya miaka tangaza habari yako; katika ghadhabu kumbuka rehema.
3 God will come from the south, and the holy one from mount Pharan: His glory covered the heavens, and the earth is full of his praise.
Mungu alitoka Temani, yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani. Utukufu wake ulifunika mbingu, na sifa zake zikaifunika dunia.
4 His brightness shall be as the light; horns are in his hands: There is his strength hid:
Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo; mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake, ambako nguvu zake zilifichwa.
5 Death shall go before his face. And the devil shall go forth before his feet.
Tauni ilimtangulia; maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.
6 He stood and measured the earth. He beheld, and melted the nations: and the ancient mountains were crushed to pieces. The hills of the world were bowed down by the journeys of his eternity.
Alisimama, akaitikisa dunia; alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke. Milima ya zamani iligeuka mavumbi na vilima vilivyozeeka vikaanguka. Njia zake ni za milele.
7 I saw the tents of Ethiopia for their iniquity, the curtains of the land of Madian shall be troubled.
Niliona watu wa Kushani katika dhiki, na makazi ya Midiani katika maumivu makali.
8 Wast thou angry, O Lord, with the rivers? or was thy wrath upon the rivers? or thy indignation in the sea? Who will ride upon thy horses: and thy chariots are salvation.
Ee Bwana, uliikasirikia mito? Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito? Je, ulighadhibikia bahari ulipoendesha farasi wako na magari yako ya ushindi?
9 Thou wilt surely take up thy bow: according to the oaths which thou hast spoken to the tribes. Thou wilt divide the rivers of the earth.
Uliufunua upinde wako na kuita mishale mingi. Uliigawa dunia kwa mito;
10 The mountains saw thee, and were grieved: the great body of waters passed away. The deep put forth its voice: the deep lifted up its hands.
milima ilikuona ikatetemeka. Mafuriko ya maji yakapita huko; vilindi vilinguruma na kuinua mawimbi yake juu.
11 The sun and the moon stood still in their habitation, in the light of thy arrows, they shall go in the brightness of thy glittering spear.
Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni katika mngʼao wa mishale yako inayoruka, na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.
12 In thy anger thou wilt tread the earth under foot: in thy wrath thou wilt astonish the nations.
Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia, na katika hasira ulikanyaga mataifa.
13 Thou wentest forth for the salvation of thy people: for salvation with thy Christ. Thou struckest the head of the house of the wicked: thou hast laid bare his foundation even to the neck.
Ulikuja kuwaokoa watu wako, kumwokoa uliyemtia mafuta. Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu, ukamvua toka kichwani hadi wayo.
14 Thou hast cursed his sceptres, the head of his warriors, them that came out as a whirlwind to scatter me. Their joy was like that of him that devoureth the poor man in secret.
Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya, wakifurahi kama walio karibu kutafuna wale wanyonge waliokuwa mafichoni.
15 Thou madest a way in the sea for thy horses, in the mud of many waters.
Ulikanyaga bahari kwa farasi wako, ukisukasuka maji makuu.
16 I have heard and my bowels were troubled: my lips trembled at the voice. Let rottenness enter into my bones, and swarm under me. That I may rest in the day of tribulation: that I may go up to our people that are girded.
Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu, midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti; uchakavu ukanyemelea mifupa yangu, na miguu yangu ikatetemeka. Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.
17 For the fig tree shall not blossom: and there shall be no spring in the vines. The labour of the olive tree shall fail: and the fields shall yield no food: the flock shall be cut off from the fold, and there shall be no herd in the stalls.
Ingawa mtini hauchanui maua na hakuna zabibu juu ya mizabibu, ingawaje mzeituni hauzai, na hata mashamba hayatoi chakula, iwapo hakuna kondoo katika banda, wala ngʼombe katika zizi,
18 But I will rejoice in the Lord: and I will joy in God my Jesus.
hata hivyo nitashangilia katika Bwana, nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.
19 The Lord God is my strength: and he will make my feet like the feet of harts: and he the conqueror will lead me upon my high places singing psalms.
Bwana Mwenyezi ni nguvu yangu; huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala, huniwezesha kupita juu ya vilima. Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.

< Habakkuk 3 >