< Deuteronomy 16 >

1 Observe the month of new corn, which is the first of the spring, that thou mayst celebrate the phase to the Lord thy God: because in this month the Lord thy God brought thee out of Egypt by night.
Shikeni mwezi wa Abibu, na kuiadhimisha Pasaka ya Bwana Mungu wenu, kwa sababu katika mwezi wa Abibu, Mungu aliwatoa Misri usiku.
2 And thou shalt sacrifice the phase to the Lord thy God, of sheep, and of oxen, in the place which the Lord thy God shall choose, that his name may dwell there.
Mtatoa dhabihu ya Pasaka ya mnyama kwa Bwana Mungu wenu kutoka kundi lenu la mbuzi na kondoo au la ngʼombe, mahali pale ambapo Bwana atapachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake.
3 Thou shalt not eat with it leavened bread: seven days shalt thou eat without leaven, the bread of affliction, because thou camest out of Egypt in fear: that thou mayst remember the day of thy coming out of Egypt, all the days of thy life.
Msile nyama hiyo pamoja na mikate iliyotiwa chachu, lakini kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, mikate ya kujitesa, kwa sababu mliondoka Misri kwa haraka, ili kwamba siku zote za maisha yenu mpate kukumbuka wakati wenu wa kuondoka Misri.
4 No leaven shall be seen in all thy coasts for seven days, neither shall any of the flesh of that which was sacrificed the first day in the evening remain until morning.
Chachu isionekane katika mali zenu katika nchi yenu yote kwa siku saba. Nyama yoyote ya dhabihu mtakayotoa jioni ya siku ya kwanza isibakizwe mpaka asubuhi.
5 Thou mayst not immolate the phase in any one of thy cities, which the Lord thy God will give thee:
Kamwe msitoe dhabihu ya Pasaka katika mji wowote ambao Bwana Mungu wenu amewapa,
6 But in the place which the Lord thy God shall choose, that his name may dwell there: thou shalt immolate the phase in the evening, at the going down of the sun, at which time thou camest out of Egypt.
isipokuwa mahali atakapopachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake. Hapo ndipo lazima mtoe dhabihu ya Pasaka jioni, jua litakapotua, iwe kumbukumbu yenu ya kutoka Misri.
7 And thou shalt dress, and eat it in the place which the Lord thy God shall choose, and in the morning rising up thou shalt go into thy dwellings.
Okeni na mle mahali pale ambapo Bwana Mungu wenu atakapopachagua, kisha asubuhi mrudi kwenye mahema yenu.
8 Six days shalt thou eat unleavened bread: and on the seventh day, because it is the assembly of the Lord thy God, thou shalt do no work.
Kwa siku sita mtakula mikate isiyotiwa chachu na siku ya saba fanyeni kusanyiko kwa ajili ya Bwana Mungu wenu na msifanye kazi.
9 Thou shalt number unto thee seven weeks from that day, wherein thou didst put the sickle to the corn.
Mhesabu majuma saba tangu wakati mnapoanza kuchukua mundu kuvuna nafaka.
10 And thou shalt celebrate the festival of weeks to the Lord thy God, a voluntary oblation of thy hand, which thou shalt offer according to the blessing of the Lord thy God.
Kisha msherehekee Sikukuu ya Majuma kwa Bwana Mungu wenu kwa kutoa sadaka ya hiari kwa kadiri ya baraka ambayo Bwana Mungu wenu amewapa.
11 And thou shalt feast before the Lord thy God, thou, and thy son, and thy daughter, and thy manservant, and thy maidservant, and the Levite that is within thy gates, and the stranger and the fatherless, and the widow, who abide with you: in the place which the Lord thy God shall choose, that his name may dwell there:
Shangilieni mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua kama makao ya Jina lake, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi walio katika miji yenu, na wageni, yatima na wajane waishio miongoni mwenu.
12 And thou shalt remember that thou wast a servant in Egypt: and thou shalt keep and do the things that are commanded.
Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa kule Misri na mfuate amri hizi kwa uangalifu.
13 Thou shalt celebrate the solemnity also of tabernacles seven days, when thou hast gathered in thy fruit of the barnfloor and of the winepress.
Adhimisheni sikukuu ya vibanda kwa siku saba baada ya kukusanya mazao yenu ya nafaka na kukamua zabibu.
14 And thou shalt make merry in thy festival time, thou, thy son, and thy daughter, thy manservant, and thy maidservant, the Levite also and the stranger, and the fatherless and the widow that are within thy gates.
Mfurahie sikukuu yenu, ninyi, wana wenu, binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi, wageni, yatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.
15 Seven days shalt thou celebrate feasts to the Lord thy God in the place which the Lord shall choose: and the Lord thy God will bless thee in all thy fruits, and in every work of thy hands, and thou shalt be in joy.
Kwa siku saba mtaiadhimisha sikukuu ya Bwana Mungu wenu katika mahali atakapopachagua Bwana. Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki katika mavuno yenu na katika kazi zote za mikono yenu na furaha yenu itakamilika.
16 Three times in a year shall all thy males appear before the Lord thy God in the place which he shall choose: in the feast of unleavened bread, in the feast of weeks, and in the feast of tabernacles. No one shall appear with his hands empty before the Lord:
Wanaume wenu wote lazima wajitokeze mara tatu kwa mwaka mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua: kwa ajili ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma, na Sikukuu ya Vibanda. Hakuna mtu atakayejitokeza mbele za Bwana mikono mitupu:
17 But every one shall offer according to what he hath, according to the blessing of the Lord his God, which he shall give him.
Kila mmoja wenu ni lazima alete zawadi kulingana na jinsi ambavyo Bwana Mungu wenu alivyowabariki.
18 Thou shalt appoint judges and magistrates in all thy gates, which the Lord thy God shall give thee, in all thy tribes: that they may judge the people with just judgment,
Wateue waamuzi na maafisa kwa kila kabila lenu katika kila mji ambao Bwana Mungu wenu anawapa, nao watawaamua watu kwa usawa.
19 And not go aside to either part. Thou shalt not accept person nor gifts: for gifts blind the eyes of the wise, and change the words of the just.
Msipotoshe haki wala msifanye upendeleo. Msikubali rushwa kwa sababu rushwa hupofusha macho ya wenye busara na kugeuza maneno ya wenye haki.
20 Thou shalt follow justly after that which is just: that thou mayst live and possess the land, which the Lord thy God shall give thee.
Mfuate haki na haki peke yake, ili mweze kuishi na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa.
21 Thou shalt plant no grove, nor any tree near the altar of the Lord thy God:
Msisimamishe nguzo yoyote ya Ashera kando ya madhabahu mliyomjengea Bwana Mungu wenu,
22 Neither shalt thou make nor set up to thyself a statue: which things the Lord thy God hateth.
wala msisimamishe jiwe la kuabudu, kwa maana Bwana Mungu wenu anavichukia vitu hivi.

< Deuteronomy 16 >