< Deuteronomy 10 >

1 At that time the Lord said to me: Hew thee two tables of stone like the former, and come up to me into the mount: and thou shalt make an ark of mood,
Kwa wakati ule Yahwe alisema kwangu, 'Chonga mbao mbili za mawe kama zile za kwanza, na njoo kwangu huku juu ya mlima, na utengeneze sanduku la mbao.
2 And I will write on the tables the words that were in them, which thou brokest before, and thou shalt put them in the ark.
Nitaandika kwenye mbao maneno ambayo yalikuwa kwenye mbao za kwanza ulizozivunja, na utaziweka ndani ya sanduku.
3 And I made an ark of setim wood And when I had hewn two tables of stone like the former, I went up into the mount, having them in my hands.
Basi nilitengeneza sanduku la mbao za mikaratusi, na nikachonga mbao mbili za mawe kwa zile za kwanza, na nikaenda juu ya mlima, nikiwa na mbao mbili mkononi mwangu.
4 And he wrote in the tables, according as he had written before, the ten words, which the Lord spoke to you in the mount from the midst of the fire, when the people were assembled: and he gave them to me.
Aliandika kwenye mbao, kama maandishi ya kwanza, amri kumi ambazo Yahwe amesema nanyi kwenye mlima kutoka katikati mwa moto katika siku ya kusanyiko; ndipo Yahwe alilinipa mimi.
5 And returning from the mount, I came down, and put the tables into the ark, that I had made, and they are there till this present, as the Lord commanded me.
Niligeuka na kushuka chini kutoka mlimani, na kuweka mbao ndani ya sanduku nililokuwa nimetengeneza; hapo zilikaa, kama Yahwe alivyoniamuru.”
6 And the children of Israel removed their camp from Beroth of the children of Jacan into Mosera, where Aaron died and was buried, and Eleazar his son succeeded him in the priestly office.
(Watu wa Israeli walisafiri kutoka Beerothi ya Bene Jaakan kwenda Moserathi. Huko Aaroni alikufa, na huko alizikwa; Eleazar, mwana wake, alitumika katika ofisi ya ukuhani kwenye nafasi yake.
7 From thence they came to Gadgad, from which place they departed, and camped in Jetebatha, in a land of waters and torrents.
Kutokea huko walisafiri kwenda Gudgodah, na kutoka Gudgodah kwenda Jotbathah, nchi yenye mikondo ya maji.
8 At that time he separated the tribe of Levi, to carry the ark of the covenant of the Lord, and to stand before him in the ministry, and to bless in his name until this present day.
Kwa wakati huo Yahwe alichagua kabila la Lawi kubeba sanduku la agano la Yahwe, kusimama mbele ya Yahwe kumtumikia na kubariki watu kwa jina lake, kama ilivyo leo.
9 Wherefore Levi hath no part nor possession with his brethren: because the Lord himself is his possession, as the Lord thy God promised him.
Kwa hiyo Lawi hawana sehemu wala urithi wa nchi pamoja na ndugu zake; Yahwe ni urithi wao, kama Yahwe Mungu wenu alizungumza naye)
10 And I stood in the mount, as before, forty days and nights: and the Lord heard me this time also, and would not destroy thee.
“Nilibaki kwenye mlima kama ilivyokuwa mara ya kwanza, siku arobaini na usiku arobaini. Yahwe alinisikiliza wakati huo pia; Yahwe hakutaka kukuangamiza.
11 And he said to me: Go, and walk before the people, that they may enter, and possess the land, which I swore to their fathers that I would give them.
Yahwe alisema nami, “Inuka, nenda mbele ya watu uwaongoze katika safari yao; wataingia na kumiliki nchi ambayo niliapa kwa mababu zao kuwapa.'
12 And now, Israel, what doth the Lord thy God require of thee, but that thou fear the Lord thy God, and walk in his ways, and love him, and serve the Lord thy God, with all thy heart, and with all thy soul:
Sasa, Israeli, Yahwe Mungu wenu ataka nini kwenu, isipokuwa hofu ya Yahwe Mungu wenu, kutembea katika njia zake zote, kumpenda yeye, na kumwabudu Yahwe Mungu wenu kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.
13 And keep the commandments of the Lord, and his ceremonies, which I command thee this day, that it may be well with thee?
Kuzishika amri za Yahwe, na maagizo ambayo ninawaamuru ninyi leo kwa ajili ya uzuri wenu?
14 Behold heaven is the Lord’s thy God, and the heaven of heaven, the earth and all things that are therein.
Tazama, kwa Yahwe Mungu wenu mbingu ni zake na mbingu za mbingu, dunia, vyote vilivyomo.
15 And yet the Lord hath been closely joined to thy fathers, and loved them and chose their seed after them, that is to say, you, out of all nations, as this day it is proved.
Yahwe peke alichukua furaha kwa baba zenu ili kwamba awapende, na aliwachagua ninyi, wazao wao, baada yao, zaidi kuliko ya watu wengine wowote, kama afanyavyo leo.
16 Circumcise therefore the foreskin of your heart, and stiffen your neck no more.
Kwa hiyo basi wataili govi la mioyo yao, na msiwe wakaidi tena.
17 Because the Lord your God he is the God of gods, and the Lord of lords, a great God and mighty and terrible, a who accepteth no person nor taketh bribes.
Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu, ni Mungu wa miungu na Bwana wa bwana, Mungu mkuu, mwenye nguvu na wakutisha, ambaye hapendelei yeyote na hapokei rushwa-
18 He doth judgment to the fatherless and the widow, loveth the stranger, and giveth him food and raiment.
Hutekeleza haki kwa yatima na wajane, na huonesha upendo kwa mgeni kwa kumpa chakula na mavazi.
19 And do you therefore love strangers, because you also were strangers in the land of Egypt.
Kwa hiyo basi mpende mgeni; kwa kuwa mlikuwa wageni kutoka nchi ya Misri.
20 Thou shalt fear the Lord thy God, and serve him only: to him thou shalt adhere, and shalt swear by his name.
Mtamche Yahwe Mungu wenu yeye mtamwabudu. Mtashikamana kwake, na kwa jina lake mtaapa.
21 He is thy praise, and thy God, that hath done for thee these great and terrible things, which thy eyes have seen.
Yeye ni sifa yenu, ni Mungu wenu, ambaye amefanya kwa ajili yenu haya mambo makuu na kutisha, ambayo macho yenu yameyaona.
22 In seventy souls thy fathers went down into Egypt: and behold now the Lord thy God hath multiplied thee as the stars of heaven.
Baba zako walienda Misri kama watu sabini; sasa Yahwe Mungu wako amekufanya wewe kuwa wengi kama nyota za mbinguni.

< Deuteronomy 10 >