< 1 Kings 5 >

1 And Hiram king of Tyre sent his servants to Solomon: for he heard that they had anointed him king in the room of his father: for Hiram had always been David’s friend.
Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
2 And Solomon sent to Hiram, saying:
Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
3 Thou knowest the will of David my father, and that he could not build a house to the name of the Lord his God, because of the wars that were round about him, until the Lord put them under the soles of his feet.
“Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
4 But now the Lord my God hath given me rest round about: and there is no adversary nor evil occurrence.
Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
5 Wherefore I purpose to build a temple to the name of the Lord my God, as the Lord spoke to David my father, saying: my son, whom I will set upon the throne in thy piece, he shall build a house to my name.
Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
6 Give orders therefore that thy servants cut me down cedar trees out of Libanus, and let my servants be with thy servants: and I will give thee the hire of thy servants whatsoever thou wilt ask, for thou knowest how there is not among my people a man that has skill to hew wood like to the Sidonians.
“Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
7 Now when Hiram had heard the words of Solomon, he rejoiced exceedingly, and said: Blessed be the Lord God this day, who hath given to David a very wise son over this numerous people.
Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
8 And Hiram sent to Solomon, saying: I have heard all thou hast desired of me: and I will do all thy desire concerning cedar trees, and fir trees.
Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
9 My servants shall bring them down from Libanus to the sea: and I will put them together in floats in the sea, and convey them to the place, which thou shalt signify to me; and will land them there, and thou shalt receive them: and thou shalt allow me necessaries, to furnish food for my household.
Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
10 So Hiram gave Solomon cedar trees, and fir trees, according to all his desire.
Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
11 And Solomon allowed Hiram twenty thousand measures of wheat, for provision for his house, and twenty measures of the purest oil: thus gave Solomon to Hiram every year.
naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
12 And the Lord gave wisdom to Solomon, as he promised him: and there was peace between Hiram and Solomon, and they two made a league together.
Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
13 And king Solomon chose workmen cut of all Israel, and the levy was of thirty thousand men.
Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
14 And he sent them to Libanus, ten thousand every month by turns, so that two months they were at home: and Adoniram was over this levy.
Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
15 And Solomon had seventy thousand to carry burdens, and eighty thousand to hew stones in the mountain:
Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
16 Besides the overseers who were over every work, in number three thousand, and three hundred that ruled over the people, and them that did the work.
pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
17 And the king commanded, that they should bring great stones, costly stones, for the foundation of the temple, and should square them:
Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
18 And the masons of Solomon, and the masons of Hiram hewed them: and the Giblians prepared timber and stones to build the house.
Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.

< 1 Kings 5 >