< 1 Corinthians 5 >

1 It is absolutely heard, that there is fornication among you, and such fornication as the like is not among the heathens; that one should have his father’s wife.
Tumesikia taarifa kuwa kuna zinaa miongoni mwenu, aina ya zinaa ambayo haipo hata katikati ya watu wa Mataifa. Tuna taarifa kwamba mmoja wenu analala na mke wa baba yake.
2 And you are puffed up; and have not rather mourned, that he might be taken away from among you, that hath done this deed.
Nanyi mwajisifu! Badala ya kuhuzunika? Yule aliyefanya hivyo anapaswa kuondolewa miongoni mwenu.
3 I indeed, absent in body, but present in spirit, have already judged, as though I were present, him that hath so done,
Ingawa sipo pamoja nanyi kimwili lakini nipo nanyi kiroho, nimekwisha mhukumu yeye aliyefanya hivi, kama vile nilikuwepo.
4 In the name of our Lord Jesus Christ, you being gathered together, and my spirit, with the power of our Lord Jesus;
Mnapokutanika pamoja katika jina la Bwana wetu Yesu, na roho yangu ipo pale kama kwa nguvu za Bwana wetu Yesu, nimekwisha mhukumu mtu huyu.
5 To deliver such a one to Satan for the destruction of the flesh, that the spirit may be saved in the day of our Lord Jesus Christ.
Nimekwisha kumkabidhi mtu huyu kwa Shetani ili kwamba mwili wake uharibiwe, ili roho yake iweze kuokolewa katika siku ya Bwana.
6 Your glorying is not good. Know you not that a little leaven corrupteth the whole lump?
Majivuno yenu si kitu kizuri. Hamjui chachu kidogo huharibu donge zima?
7 Purge out the old leaven, that you may be a new paste, as you are unleavened. For Christ our pasch is sacrificed.
Jisafisheni ninyi wenyewe chachu ya kale, ili kwamba muwe donge jipya, ili kwamba mwe mkate usiochachuliwa. Kwa kuwa, Kristo, Mwana Kondoo wetu wa pasaka amekwisha kuchinjwa.
8 Therefore let us feast, not with the old leaven, nor with the leaven of malice and wickedness; but with the unleavened bread of sincerity and truth.
Kwa hiyo tusherekee karamu si kwa chachu ya kale, chachu ya tabia mbaya na uovu. Badala yake, tusherekee na mkate usiotiwa chachu wa unyenyekevu na kweli.
9 I wrote to you in an epistle, not to keep company with fornicators.
Niliandika katika barua yangu kuwa msichangamane na wazinzi.
10 I mean not with the fornicators of this world, or with the covetous, or the extortioners, or the servers of idols; otherwise you must needs go out of this world.
Sina maana wazinzi wa dunia hii, au na wenye tamaa au wanyang'anyi au waabudu sanamu kwa kukaa mbali nao, basi ingewapasa mtoke duniani.
11 But now I have written to you, not to keep company, if any man that is named a brother, be a fornicator, or covetous, or a server of idols, or a railer, or a drunkard, or an extortioner: with such a one, not so much as to eat.
Lakini sasa nawaandikia kutojichanganya na yeyote anayeitwa kaka au dada katika Kristo, lakini anaishi katika uzinzi au ambaye ni mwenye kutamani, au mnyang'anyi, au mwabudu sanamu, au mtukanaji au mlevi. Wala msile naye mtu wa namna ile.
12 For what have I to do to judge them that are without? Do not you judge them that are within?
Kwa hiyo nitajihusishaje kuwahukumu walio nje ya Kanisa? Badala yake, ninyi hamkuwahukumu walio ndani ya kanisa?
13 For them that are without, God will judge. Put away the evil one from among yourselves.
Lakini Mungu anawahukumu walio nje. “Mwondoeni mtu mwovu miongoni mwenu”

< 1 Corinthians 5 >