< 1 Corinthians 16 >

1 Now concerning the collections that are made for the saints, as I have given order to the churches of Galatia, so do ye also.
Sasa kuhusu michango kwa ajili ya waumini, kama nilivyo elekeza makanisa ya Galatia, vivyo hivyo mwapaswa kufanya.
2 On the first day of the week let every one of you put apart with himself, laying up what it shall well please him; that when I come, the collections be not then to be made.
Katika siku ya kwanza ya wiki, kila mmoja wenu aweke kitu fulani kando na kukihifadhi, kama muwezavyo. Fanyeni hivyo ili kwamba kusiwe na michango wakati nikija.
3 And when I shall be with you, whomsoever you shall approve by letters, them will I send to carry your grace to Jerusalem.
Na nitakapofika, yeyote mtakayemchagua, nitamtuma pamoja na barua kutoa sadaka yenu huko Yerusalem.
4 And if it be meet that I also go, they shall go with me.
Na kama ni sahihi kwa mimi kwenda pia, watakwenda pamoja nami.
5 Now I will come to you, when I shall have passed through Macedonia. For I shall pass through Macedonia.
Lakini nitakuja kwenu, wakati ninapitia Makedonia. Kwa kuwa nitapitia Makedonia.
6 And with you perhaps I shall abide, or even spend the winter: that you may bring me on my way whithersoever I shall go.
Labda naweza kukaa nanyi au hata kumaliza majira ya baridi, ili kwamba muweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendako.
7 For I will not see you now by the way, for I trust that I shall abide with you some time, if the Lord permit.
Kwa kuwa sitarajii kuwaona sasa kwa muda mfupi. Kwani ninatumaini kukaa nanyi kwa muda fulani, kama Bwana ataniruhusu.
8 But I will tarry at Ephesus until Pentecost.
Lakini nitakaa Efeso mpaka Pentekoste,
9 For a great door and evident is opened unto me: and many adversaries.
kwa kuwa mlango mpana umefunguliwa kwa ajili yangu, na kuna maadui wengi wanipingao.
10 Now if Timothy come, see that he be with you without fear, for he worketh the work of the Lord, as I also do.
Sasa wakati Timotheo akija, muoneni kwamba yuko na ninyi pasipo kuogopa, anafanya kazi ya Bwana, kama ninavyofanya.
11 Let no man therefore despise him, but conduct ye him on his way in peace: that he may come to me. For I look for him with the brethren.
Mtu yeyote asimdharau. Mumsaidie katika njia yake kwa amani, ili kwamba aweze kuja kwangu. Kwa kuwa ninamtarajia aje pamoja na ndugu.
12 And touching our brother Apollo, I give you to understand, that I much entreated him to come unto you with the brethren: and indeed it was not his will at all to come at this time. But he will come when he shall have leisure.
Sasa kuhusiana na ndugu yetu Apolo. Nilimtia moyo sana kuwatembelea ninyi pamoja na ndugu. Lakini aliamua kutokuja kwa sasa. Hata hivyo, atakuja wakati ana nafasi.
13 Watch ye, stand fast in the faith, do manfully, and be strengthened.
Muwe macho, simameni imara, mtende kama wanaume, muwe na nguvu.
14 Let all your things be done in charity.
Basi yote myafanyayo yafanyike katika upendo.
15 And I beseech you, brethren, you know the house of Stephanas, and of Fortunatus, and of Achaicus, that they are the firstfruits of Achaia, and have dedicated themselves to the ministry of the saints:
Mnaijua kaya ya Stefana. Mnajua kwamba walikuwa waamini wa kwanza huko Akaya, na kwamba walijiweka wenyewe kwenye huduma ya waumini. Na sasa nawasihi, kaka na dada zangu,
16 That you also be subject to such, and to every one that worketh with us, and laboureth.
kuweni wanyenyekevu kwa watu kama hao, na kwa kila mtu anayesaidia katika kazi na watenda kazi pamoja nasi.
17 And I rejoice in the presence of Stephanas, and Fortunatus, and Achaicus, because that which was wanting on your part, they have supplied.
Na ninafurahi kwa ujio wa Stefana, Fotunato, na Akiko. Wamesimama mahali ambapo ninyi mgepaswa kuwa.
18 For they have refreshed both my spirit and yours. Know them, therefore, that are such.
Kwa kuwa wameifurahisha roho yangu na yenu. Kwa hiyo sasa, watambueni watu kama hawa.
19 The churches of Asia salute you. Aquila and Priscilla salute you much in the Lord, with the church that is in their house, with whom I also lodge.
Makanisa ya Asia wametuma salamu kwenu. Akila na Priska wanawasalimu katika Bwana, pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao.
20 All the brethren salute you. Salute one another with a holy kiss.
Kaka na dada zangu wote wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
21 The salutation of me Paul, with my own hand.
Mimi, Paulo, naandika hivi kwa mkono wangu.
22 If any man love not our Lord Jesus Christ, let him be anathema, maranatha.
Kama yeyote hampendi Bwana, basi laana iwe juu yake. Bwana wetu, njoo!
23 The grace of our Lord Jesus Christ be with you.
Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24 My charity be with you all in Christ Jesus. Amen.
Upendo wangu uwe pamoja nanyi katika Kristo Yesu.

< 1 Corinthians 16 >