< Matthew 22 >

1 And Jesus answering spoke to them again in parables, saying,
Yesu akasema nao tena kwa mifano, akawaambia,
2 The kingdom of the heavens has become like a king who made a wedding feast for his son,
“Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme mmoja aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi.
3 and sent his bondmen to call the persons invited to the wedding feast, and they would not come.
Akawatuma watumishi wake kuwaita wale waliokuwa wamealikwa karamuni, lakini wakakataa kuja.
4 Again he sent other bondmen, saying, Say to the persons invited, Behold, I have prepared my dinner; my oxen and my fatted beasts are killed, and all things ready; come to the wedding feast.
“Kisha akawatuma watumishi wengine akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa kwamba nimeandaa chakula. Nimekwisha kuchinja mafahali wangu na vinono, karamu iko tayari. Karibuni kwa karamu ya arusi.’
5 But they made light of it, and went, one to his own land, and another to his commerce.
“Lakini hawakuzingatia, wakaenda zao: huyu shambani mwake na mwingine kwenye biashara zake.
6 And the rest, laying hold of his bondmen, ill-treated and slew [them].
Wengine wao wakawakamata wale watumishi wake, wakawatesa na kuwaua.
7 And [when] the king [heard of it he] was wroth, and having sent his forces, destroyed those murderers and burned their city.
Yule mfalme akakasirika sana, akapeleka jeshi lake likawaangamiza wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.
8 Then he says to his bondmen, The wedding feast is ready, but those invited were not worthy;
“Kisha akawaambia watumishi wake, ‘Karamu ya arusi imeshakuwa tayari, lakini wale niliowaalika hawakustahili kuja.
9 go therefore into the thoroughfares of the highways, and as many as ye shall find invite to the wedding feast.
Kwa hiyo nendeni katika njia panda mkamwalike karamuni yeyote mtakayemwona.’
10 And those bondmen went out into the highways, and brought together all as many as they found, both evil and good; and the wedding feast was furnished with guests.
Wale watumishi wakaenda barabarani, wakawakusanya watu wote waliowaona, wema na wabaya. Ukumbi wa arusi ukajaa wageni.
11 And the king, having gone in to see the guests, beheld there a man not clothed with a wedding garment.
“Lakini mfalme alipoingia ndani ili kuwaona wageni, akamwona mle mtu mmoja ambaye hakuwa amevaa vazi la arusi.
12 And he says to him, [My] friend, how camest thou in here not having on a wedding garment? But he was speechless.
Mfalme akamuuliza, ‘Rafiki, uliingiaje humu bila vazi la arusi?’ Yule mtu hakuwa na la kusema.
13 Then said the king to the servants, Bind him feet and hands, and take him away, and cast him out into the outer darkness: there shall be the weeping and the gnashing of teeth.
“Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu mkamtupe nje, kwenye giza. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
14 For many are called ones, but few chosen ones.
“Kwa maana walioitwa ni wengi, lakini walioteuliwa ni wachache.”
15 Then went the Pharisees and held a council how they might ensnare him in speaking.
Ndipo Mafarisayo wakatoka nje wakaandaa mpango wa kumtega Yesu katika maneno yake.
16 And they send out to him their disciples with the Herodians, saying, Teacher, we know that thou art true and teachest the way of God in truth, and carest not for any one, for thou regardest not men's person;
Wakatuma wanafunzi wao kwake pamoja na Maherode. Nao wakasema, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu na unafundisha njia ya Mungu katika kweli bila kuyumbishwa na mtu wala kuonyesha upendeleo.
17 tell us therefore what thou thinkest: Is it lawful to give tribute to Caesar, or not?
Tuambie basi, wewe unaonaje? Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
18 But Jesus, knowing their wickedness, said, Why tempt ye me, hypocrites?
Lakini Yesu, akijua makusudi yao mabaya, akawaambia, “Enyi wanafiki, kwa nini mnajaribu kunitega?
19 Shew me the money of the tribute. And they presented to him a denarius.
Nionyesheni hiyo sarafu inayotumika kwa kulipia kodi.” Wakamletea dinari.
20 And he says to them, Whose [is] this image and superscription?
Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?”
21 They say to him, Caesar's. Then he says to them, Pay then what is Caesar's to Caesar, and what is God's to God.
Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Basi Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
22 And when they heard [him], they wondered, and left him, and went away.
Waliposikia hili, wakashangaa. Hivyo wakamwacha, wakaenda zao.
23 On that day came to him Sadducees, who say there is no resurrection; and they demanded of him,
Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza swali, wakisema,
24 saying, Teacher, Moses said, If any one die, not having children, his brother shall marry his wife and shall raise up seed to his brother.
“Mwalimu, Mose alisema, ‘Kama mtu akifa bila kuwa na watoto, ndugu yake inampasa amwoe huyo mjane ili ampatie watoto huyo nduguye aliyekufa.’
25 Now there were with us seven brethren; and the first having married died, and not having seed, left his wife to his brother.
Basi palikuwa na ndugu saba miongoni mwetu. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa, na kwa kuwa hakuwa na watoto, akamwachia nduguye yule mjane.
26 In like manner also the second and the third, unto the seven.
Ikatokea vivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili, na wa tatu, hadi wote saba.
27 And last of all the woman also died.
Hatimaye, yule mwanamke naye akafa.
28 In the resurrection therefore of which of the seven shall she be wife, for all had her?
Sasa basi, siku ya ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa wamemwoa huyo mwanamke?”
29 And Jesus answering said to them, Ye err, not knowing the scriptures nor the power of God.
Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu hamjui Maandiko wala uweza wa Mungu.
30 For in the resurrection they neither marry nor are given in marriage, but are as angels of God in heaven.
Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
31 But concerning the resurrection of the dead, have ye not read what was spoken to you by God, saying,
Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjasoma kile Mungu alichowaambia, kwamba,
32 I am the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob? God is not God of [the] dead, but of [the] living.
‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo’? Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”
33 And when the crowds heard [it] they were astonished at his doctrine.
Ule umati wa watu uliposikia hayo, ulishangaa sana kwa mafundisho yake.
34 But the Pharisees, having heard that he had put the Sadducees to silence, were gathered together.
Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, Mafarisayo wakakusanyika pamoja.
35 And one of them, a lawyer, demanded, tempting him, and saying,
Mmoja wao, mtaalamu wa sheria, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema,
36 Teacher, which is the great commandment in the law?
“Mwalimu, ni amri ipi katika Sheria iliyo kuu kuliko zote?”
37 And he said to him, Thou shalt love [the] Lord thy God with all thy heart, and with all thy soul, and with all thy understanding.
Yesu akamjibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’
38 This is [the] great and first commandment.
Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
39 And [the] second is like it, Thou shalt love thy neighbour as thyself.
Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’
40 On these two commandments the whole law and the prophets hang.
Amri hizi mbili ndizo msingi wa Sheria na Manabii.”
41 And the Pharisees being gathered together, Jesus demanded of them,
Wakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza,
42 saying, What think ye concerning the Christ? whose son is he? They say to him, David's.
“Mnaonaje kuhusu Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”
43 He says to them, How then does David in Spirit call him Lord, saying,
Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Kristo ‘Bwana’? Kwa maana asema,
44 The Lord said to my Lord, Sit on my right hand until I put thine enemies under thy feet?
“‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
45 If therefore David call him Lord, how is he his son?
Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”
46 And no one was able to answer him a word, nor did any one dare from that day to question him any more.
Hakuna mtu aliyeweza kumjibu Yesu neno. Tena tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu kumuuliza tena maswali.

< Matthew 22 >