< Luke 21 >

1 And he looked up and saw the rich casting their gifts into the treasury;
Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
2 but he saw also a certain poor widow casting therein two mites.
Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
3 And he said, Verily I say unto you, that this poor widow has cast in more than all;
Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
4 for all these out of their abundance have cast into the gifts [of God]; but she out of her need has cast in all the living which she had.
Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
5 And as some spoke of the temple, that it was adorned with goodly stones and consecrated offerings, he said,
Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
6 [As to] these things which ye are beholding, days are coming in which there shall not be left stone upon stone which shall not be thrown down.
“Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
7 And they asked him saying, Teacher, when then shall these things be; and what [is] the sign when these things are going to take place?
Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
8 And he said, See that ye be not led astray, for many shall come in my name, saying, I am [he], and the time is drawn nigh: go ye not [therefore] after them.
Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
9 And when ye shall hear of wars and tumults, be not terrified, for these things must first take place, but the end is not immediately.
Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
10 Then he said to them, Nation shall rise up against nation, and kingdom against kingdom;
Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
11 there shall be both great earthquakes in different places, and famines and pestilences; and there shall be fearful sights and great signs from heaven.
Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
12 But before all these things they shall lay their hands upon you and persecute you, delivering [you] up to synagogues and prisons, bringing [you] before kings and governors on account of my name;
Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
13 but it shall turn out to you for a testimony.
Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
14 Settle therefore in your hearts not to meditate beforehand [your] defence,
Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
15 for I will give you a mouth and wisdom which all your opposers shall not be able to reply to or resist.
kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
16 But ye will be delivered up even by parents and brethren and relations and friends, and they shall put to death [some] from among you,
Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
17 and ye will be hated of all for my name's sake.
Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
18 And a hair of your head shall in no wise perish.
Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
19 By your patient endurance gain your souls.
Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
20 But when ye see Jerusalem encompassed with armies, then know that its desolation is drawn nigh.
Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
21 Then let those who are in Judaea flee to the mountains, and those who are in the midst of it depart out, and those who are in the country not enter into it;
Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
22 for these are days of avenging, that all the things that are written may be accomplished.
Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
23 But woe to them that are with child and to them who give suck in those days, for there shall be great distress upon the land and wrath upon this people.
Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
24 And they shall fall by the edge of the sword, and be led captive into all the nations; and Jerusalem shall be trodden down of [the] nations until [the] times of [the] nations be fulfilled.
Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
25 And there shall be signs in sun and moon and stars, and upon the earth distress of nations in perplexity [at] the roar of the sea and rolling waves,
Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
26 men ready to die through fear and expectation of what is coming on the habitable earth, for the powers of the heavens shall be shaken.
Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
27 And then shall they see the Son of man coming in a cloud with power and great glory.
Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
28 But when these things begin to come to pass, look up and lift up your heads, because your redemption draws nigh.
Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
29 And he spoke a parable to them: Behold the fig-tree and all the trees;
Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
30 when they already sprout, ye know of your own selves, [on] looking [at them], that already the summer is near.
Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
31 So also ye, when ye see these things take place, know that the kingdom of God is near.
Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
32 Verily I say unto you, that this generation shall in no wise pass away until all come to pass.
Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
33 The heaven and the earth shall pass away, but my words shall in no wise pass away.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
34 But take heed to yourselves lest possibly your hearts be laden with surfeiting and drinking and cares of life, and that day come upon you suddenly unawares;
Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
35 for as a snare shall it come upon all them that dwell upon the face of the whole earth.
kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
36 Watch therefore, praying at every season, that ye may be accounted worthy to escape all these things which are about to come to pass, and to stand before the Son of man.
Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
37 And by day he was teaching in the temple, and by night, going out, he remained abroad on the mountain called [the mount] of Olives;
Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
38 and all the people came early in the morning to him in the temple to hear him.
Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.

< Luke 21 >