< Galatians 1 >

1 Paul, apostle, not from men nor through man, but through Jesus Christ, and God [the] Father who raised him from among [the] dead,
Mimi Paulo mtume,
2 and all the brethren with me, to the assemblies of Galatia.
na ndugu wote walio pamoja nami, tunayaandikia makanisa yaliyoko Galatia. Mimi nimepata kuwa mtume si kutokana na mamlaka ya binadamu, wala si kwa nguvu ya mtu, bali kwa uwezo wa Yesu Kristo na wa Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka wafu.
3 Grace to you, and peace, from God [the] Father, and our Lord Jesus Christ,
Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
4 who gave himself for our sins, so that he should deliver us out of the present evil world, according to the will of our God and Father; (aiōn g165)
Kristo alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba, ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu mbaya wa sasa. (aiōn g165)
5 to whom [be] glory to the ages of ages. Amen. (aiōn g165)
Kwake yeye uwe utukufu milele! Amina. (aiōn g165)
6 I wonder that ye thus quickly change, from him that called you in Christ's grace, to a different gospel,
Nashangaa kwamba muda mfupi tu umepita, nanyi mnamwasi yule aliyewaita kwa neema ya Kristo, mkafuata Habari Njema ya namna nyingine.
7 which is not another [one]; but there are some that trouble you, and desire to pervert the glad tidings of the Christ.
Lakini hakuna “Habari Njema” nyingine. Ukweli ni kwamba wako watu wanaowavurugeni, watu wanaotaka kuipotosha Habari Njema ya Kristo.
8 But if even we or an angel out of heaven announce as glad tidings to you [anything] besides what we have announced as glad tidings to you, let him be accursed.
Lakini, hata kama mmoja wetu au malaika kutoka mbinguni, atawahubirieni Habari Njema tofauti na ile tuliyowahubirieni sisi, basi huyo na alaaniwe!
9 As we have said before, now also again I say, If any one announce to you as glad tidings [anything] besides what ye have received, let him be accursed.
Tulikwisha sema, na sasa nasema tena: kama mtu yeyote anawahubirieni Habari Njema ya aina nyingine, tofauti na ile mliyokwisha pokea, huyo na alaaniwe!
10 For do I now seek to satisfy men or God? or do I seek to please men? If I were yet pleasing men, I were not Christ's bondman.
Sasa nataka kibali cha nani: cha binadamu, ama cha Mungu? Au je, nataka kuwapendeza watu? Kama ningefanya hivyo, mimi singekuwa kamwe mtumishi wa Kristo.
11 But I let you know, brethren, [as to] the glad tidings which were announced by me, that they are not according to man.
Ndugu, napenda mfahamu kwamba ile Habari Njema niliyoihubiri si ujumbe wa kibinadamu.
12 For neither did I receive them from man, neither was I taught [them], but by revelation of Jesus Christ.
Wala mimi sikuipokea kutoka kwa binadamu, wala sikufundishwa na mtu. Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyenifunulia.
13 For ye have heard [what was] my conversation formerly in Judaism, that I excessively persecuted the assembly of God, and ravaged it;
Bila shaka mlikwisha sikia jinsi nilivyokuwa ninaishi zamani kwa kuzingatia dini ya Kiyahudi, na jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kupita kiasi na kutaka kuliharibu kabisa.
14 and advanced in Judaism beyond many [my] contemporaries in my nation, being exceedingly zealous of the doctrines of my fathers.
Naam, mimi niliwashinda wengi wa wananchi wenzangu wa rika langu katika kuizingatia dini ya Kiyahudi, nikajitahidi sana kuyashika mapokeo ya wazee wetu.
15 But when God, who set me apart [even] from my mother's womb, and called [me] by his grace,
Lakini Mungu, kwa neema yake, alikuwa ameniteua hata kabla sijazaliwa, akaniita nimtumikie.
16 was pleased to reveal his Son in me, that I may announce him as glad tidings among the nations, immediately I took not counsel with flesh and blood,
Mara tu alipoamua kunifunulia Mwanae kusudi niihubiri Habari Njema yake kwa watu wa mataifa mengine, bila kutafuta maoni ya binadamu,
17 nor went I up to Jerusalem to those [who were] apostles before me; but I went to Arabia, and again returned to Damascus.
na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.
18 Then after three years I went up to Jerusalem to make acquaintance with Peter, and I remained with him fifteen days;
Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.
19 but I saw none other of the apostles, but James the brother of the Lord.
Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
20 Now what I write to you, behold, before God, I do not lie.
Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.
21 Then I came into the regions of Syria and Cilicia.
Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.
22 But I was unknown personally to the assemblies of Judaea which [are] in Christ;
Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.
23 only they were hearing that he who persecuted us formerly now announces the glad tidings of the faith which formerly he ravaged:
Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: “Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza.”
24 and they glorified God in me.
Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.

< Galatians 1 >