< Ephesians 3 >

1 For this reason I Paul, prisoner of the Christ Jesus for you nations,
Kwa sababu ya hii mimi, Paulo, ni mfungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu Mataifa.
2 (if indeed ye have heard of the administration of the grace of God which has been given to me towards you,
Na amini ya kwamba mmesikia juu ya kazi ya neema ya Mungu aliyo nipa kwa ajili yenu.
3 that by revelation the mystery has been made known to me, (according as I have written before briefly,
Nawaandikieni kutokana na jinsi ufunuo ulivyo funuliwa kwangu. Huu ni ukweli uliyofichika ambao niliandika kwa kifupi kwenye barua nyingine.
4 by which, in reading it, ye can understand my intelligence in the mystery of the Christ, )
Usomapo kuhusu haya, utaweza kutambua busara yangu katika ukweli huu uliofichika kuhusu Kristo.
5 which in other generations has not been made known to the sons of men, as it has now been revealed to his holy apostles and prophets in [the power of the] Spirit,
Kwa vizazi vingine ukweli huu haukufanywa utambulike kwa wana wa watu. Ila kwa sasa umewekwa wazi kwa Roho kwa Mitume waliotengwa na Manabii.
6 that [they who are of] the nations should be joint heirs, and a joint body, and joint partakers of [his] promise in Christ Jesus by the glad tidings;
Ukweli huu uliofichika ni kwamba watu wa Mataifa ni washiriki wenzetu na wajumbe wenzetu wa mwili. Niwashiriki pamoja na ahadi ya Kristo Yesu kupitia injili.
7 of which I am become minister according to the gift of the grace of God given to me, according to the working of his power.
Na kwa hili nimefanyika mtumishi kwa zawadi ya neema ya Mungu iliyotolewa kwangu kupitia utendaji wa nguvu yake.
8 To me, less than the least of all saints, has this grace been given, to announce among the nations the glad tidings of the unsearchable riches of the Christ,
Mungu alitoa zawadi hii kwangu, japo kuwa mimi ni mtu mdogo wa wote katika wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu. Zawadi hii ni kwamba inanipasa kuwatangazia mataifa injili yenye utajiri usiochunguzika wa Kristo.
9 and to enlighten all [with the knowledge of] what is the administration of the mystery hidden throughout the ages in God, who has created all things, (aiōn g165)
inanipasa kuwaangazia watu wote juu ya nini ni mpango wa Mungu wa siri. Huu ni mpango ambao ulikuwa umefichwa kwa miaka mingi iliyopita, na Mungu ambaye aliviumba vitu vyote. (aiōn g165)
10 in order that now to the principalities and authorities in the heavenlies might be made known through the assembly the all-various wisdom of God,
Hii ilikuwa kwamba, kupitia Kanisa, watawala na mamlaka katika sehemu za mbingu wapate kujua pande nyingi za asili ya hekima ya Mungu.
11 according to [the] purpose of the ages, which he purposed in Christ Jesus our Lord, (aiōn g165)
Haya yangetokea kupitia mpango wa milele ambao aliukamilisha ndani ya Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn g165)
12 in whom we have boldness and access in confidence by the faith of him.
Kwa kuwa katika Kristo tuna ujasiri na uwezo wa kuingia kwa ujasiri kwa sababu ya imani yetu kwake.
13 Wherefore I beseech [you] not to faint through my tribulations for you, which is your glory.
Kwa hiyo nawaomba msikate tamaa kwasababu ya mateso yangu kwa ajili yenu. Haya ni utukufu wenu.
14 For this reason I bow my knees to the Father [of our Lord Jesus Christ],
Kwa sababu hii napiga magoti kwa Baba.
15 of whom every family in [the] heavens and on earth is named,
ambaye kwa yeye kila familia mbinguni na juu ya nchi imeitwa jina.
16 in order that he may give you according to the riches of his glory, to be strengthened with power by his Spirit in the inner man;
Ninaomba kwamba apate kuwanemesha, kutokana na utajiri wa utukufu wake, awafanye imara kwa nguvu kupitia Roho wake, ambaye yu ndani yenu.
17 that the Christ may dwell, through faith, in your hearts, being rooted and founded in love,
Ninaomba kwamba Kristo aishi ndani ya mioyo yenu kupitia imani.
18 in order that ye may be fully able to apprehend with all the saints what [is] the breadth and length and depth and height;
Ninaomba kwamba muwe na shina na msingi wa upendo wake. Muwe katika pendo lake ili muweze kuelewa, pamoja na wote waaminio, jinsi upana, na urefu na kimo na kina cha upendo wa Kristo.
19 and to know the love of the Christ which surpasses knowledge; that ye may be filled [even] to all the fulness of God.
Ninaomba Kwamba mjue ukuu wa upendo wa Kristo, ambao unazidi ufahamu. Mfanye haya ili mjazwe na ukamilifu wote wa Mungu.
20 But to him that is able to do far exceedingly above all which we ask or think, according to the power which works in us,
Na sasa kwake yeye awezaye kufanya kila jambo, zaidi ya yote tuyaombayo au tuyawazayo, kupitia nguvu yake itendayo kazi ndani yetu,
21 to him be glory in the assembly in Christ Jesus unto all generations of the age of ages. Amen). (aiōn g165)
kwake yeye kuwe utukufu ndani ya kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote milele na milele. Amina. (aiōn g165)

< Ephesians 3 >