< 1 Timothy 2 >

1 I exhort therefore, first of all, that supplications, prayers, intercessions, thanksgivings be made for all men;
Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
2 for kings and all that are in dignity, that we may lead a quiet and tranquil life in all piety and gravity;
kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
3 for this is good and acceptable before our Saviour God,
Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
4 who desires that all men should be saved and come to [the] knowledge of [the] truth.
anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
5 For God is one, and [the] mediator of God and men one, [the] man Christ Jesus,
Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
6 who gave himself a ransom for all, the testimony [to be rendered] in its own times;
aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
7 to which I have been appointed a herald and apostle, (I speak [the] truth, I do not lie, ) a teacher of [the] nations in faith and truth.
Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
8 I will therefore that the men pray in every place, lifting up pious hands, without wrath or reasoning.
Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
9 In like manner also that the women in decent deportment and dress adorn themselves with modesty and discretion, not with plaited [hair] and gold, or pearls, or costly clothing,
Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10 but, what becomes women making profession of the fear of God, by good works.
bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
11 Let a woman learn in quietness in all subjection;
Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
12 but I do not suffer a woman to teach nor to exercise authority over man, but to be in quietness;
Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
13 for Adam was formed first, then Eve:
Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
14 and Adam was not deceived; but the woman, having been deceived, was in transgression.
Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
15 But she shall be preserved in childbearing, if they continue in faith and love and holiness with discretion.
Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.

< 1 Timothy 2 >